Kila mmoja wetu anapenda kuwa na fedha zitakazomtosheleza mahitaji yake na kuweza kumuondoa kwenye umasikini. Pamoja na kupenda fedha na kuuchukia umasikini bado matendo yako hayaonyehi hivyo. Matendo yako yanakwenda kinyume kabisa na mapenzi au mawazo yako.

Matendo yako yanaonesha kwamba hupendi fedha na hutaki kuondoka kwenye umasikini. Ni vipi matendo yako yanaonesha hivi? Leo tutajadili tabia kumi zinazoonesha kwamba hupendi fedha na unataka kuendelea kuukumbatia umasikini.

Kwa wiki nne zilizopita haka kwenye KISIMA CHA MAARIFA tumemekuwa tunajadili kuhusu kujenga tabia ya matumizi mazuri ya fedha. Kama ulifuatilia makala zote kwa makini nina imani utakuwa umejifunza mambo mengi sana. Na kama umeanza kuyatumia mambo haya kwenye maisha yako utaona mabadiliko makubwa sana. Ila kama umeendelea kugoma na kuendelea kung’ang’ania tabia zako mbaya kuhusu fedha utaendelea kulalamika kila siku.

100_7560 ED1

Hizi hapa ni tabia kumi mbaya kuhusu fedha zinazokurudisha nyuma kila siku, kukufanya uwe na maisha magumu na kuendelea kuwa masikini.

1. Kutumia fedha bila ya bajeti.

Kuna sababu kubwa sana kwa nini kila serikali, kampuni au taasisi duniani inakuwa na bajeti ya matumizi ya fedha. Ni kwa sababu inajulikana kwamba fedha yoyote ambayo haijapangiwa matumizi itatumika hovyo tu. Na wewe kwa kuwa huna mpango wa matumizi ya fedha zako unajikuta unazitumia hovyo na zikishakwisha unajiuliza zimekwenda wapi aua nani kakuibia. Kujua zaidi kuhusu tabia zako mbaya kifedha soma; tatizo sio fedha, tatizo ni wewe.

2. Kutokuweka akiba.

Tabia ya kutokujiwekea akiba ni moja ya tabia ambazo zinakufanya uendelee kuwa na maisha magumu na kushindwa kuondoka kwenye umasikini. Kushindwa kujiwekea akiba ni tabia yako mbaya tu kifedha na huna sababu nyingine ya msingi. Kama unafikiri unashindwa kujiwekea akiba kwa sababu kipato chako ni kidogo unajidanganya mwenyewe. Soma; Anza kujijengea tabia ya kujiwekea akiba na uone ni jinsi gani unavyoweza kuanza kuweka akiba hata kama kipato chako ni kidogo.

3. Kununu vitu bila ya mpangilio.

Ni mara ngapi umekutana na mtu njiani anauza kitu na ukashawishika kukinunua japo hukuwa na mahitaji ya kukinunua? Ni mara ngapi umenunua kitu cha aina hii na baadae ukawa huna matumizi nacho au kikawa sio muhimu kama ulivyofikiri? Hii ni tabia mbaya kwenye matumizi ya fedha na inakurudisha sana nyuma. Usinunue tu kitu kwa sababu anayeuza amekushawishi ununue, nunua kitu ambacho umepanga kununua na unamahitaji nacho kweli.

4. Kununua vitu vya bei rahisi.

Kununua vitu vya bei rahisi ni tabia mbaya kifedha na inachangia kwa kiasi kikubwa sana kukurudisha nyuma na kuendelea kubaki kwenye umasikini. Bado hujaelewa vizuri? Mara nyingi unafikiri kununua vitu vya bei rahisi ndio kutunza fedha, ila unapofikiri vizuri vitu vya bei rahisi vina ubora hafifu na hivyo kukufanya ununue mara nyingi. Kwa upande mwingine kuna vitu vinakuwa vinauzwa bei ghali ila vina ubora mkubwa na vinadumu kwa muda mrefu.  Kwa mfano mtu anayenunua gari kwa bei rahisi kutoka kwa mtu anaweza kupata usumbufu mkubwa sana baadae kwenye matengenezo au kuimudu gari hiyo. Ila yule anayenunua gari ambayo bado ni mpya au haijatumika sana ataitumia muda mrefu kabla ya kuanza kugharamia matengenezo.

5. Kutegemea chanzo kimoja cha mapato.

Kama unategemea chanzo kimoja tu cha mapato hasa kwa wale walioajiriwa unajijengea mazingira magumu sana. Unapokuwa na chanzo kimoja tu cha mapato ambacho ni ajira ni rahisi sana kwako kuendelea kubaki kwenye umasikini. Jijengee utaratibu wa kujiwekea akiba na tumia akiba hiyo kuwekeza sehemu mbalimbali ambapo unaweza kuwa na vipato vingine. Wiki zijazo tutajadili kwa kina kuhusu sehemu mbalimbali za kuwekeza hapa Tanzania, usikose kuwepo kwenye KISIMA CHA MAARIFA.

Kuendelea kusoma tabia nyingine tano zilizobaki jiunge na KISIMA CHA MAARIFA. Kwa kujiunga na kisima cha maarifa utaweza kujifunza mambo mengi sana yatakayokuwezesha kufikia mafanikio makubwa kwenye maisha yako.

Kujiunga na KISIMA CHA MAARIFA tuma fedha tsh elfu kumi kwenye namba 0717396253/0755953887 na kisha unatuma email yako ya gmail na unatumiwa mwaliko wa kujiunga na KISIMA.

Nakutakia kila la kheri katika harakati za kuboresha maisha yako.

TUKO PAMOJA.