Kufikia ubora wa hali ya juu kabisa kwenye jambo lolote unalofanya(world class) ni kitu ambacho kila mtu anakipenda. Pamoja na kupendwa na kila mtu na bado ni watu wachache sana ambao wanaweza kufikia ubora huo wa hali ya juu. Sio kwamba watu hao wanaoweza kufikia ubora huo ndio pekee ambao wanajaribu kufanya, wanafanya wengi ila wengi wanaishia njiani.

Kufikia ubora wa hali ya juu sana sio kitu rahisi kama kusema hivyo. Lakini pia sio kitu ambacho kinashindikana. Kwa wewe kuwepo tu hapa kwenye KISIMA CHA MAARIFA tayari upo tofauti na watu wengine wanaofikiria kufikia ubora wa hali ya juu. Wewe umeshapiga hatua zaidi na hivyo njia yako inaweza kuwa rahisi zaidi ukilinganisha na njia za wengine.

Leo tutajadili maadui kumi wa ubora wa hali ya juu. Hivi ni vitu ambavyo vinawakwamisha watu ambao wamejitoa kwa ajili ya kufikia ubora wa hali ya juu. Watu wengi hawajui maadui hawa kwa sababu ni vitu ambavyo tunaishi navyo kila siku. Kwa kuwa wewe uko mbele ya wengine, utawajua maaduia hawa na utaanza kuwaepuka mara moja ili kuweza kufikia mafanikio makubwa kwa uhakika zaidi.

Yafuatayo ni mambo kumi ambayo yanawazuia watu wengi kufikia ubora wa hali ya juu.

1. Kutafuta njia rahisi ya kufanya mambo.

Katika kufikia uboa kuna wakati utapitia mambo magumu sana. Ukikimbia mambo hayo magumu na kutafuta njia rahisi kamwe hutofikia ubora. Ni katika nyakati hizi ngumu ambapo unajifunza somo bora sana kuhusu kufikia mafanikio makubwa. Hivyo unapoona mambo ni magumu furahia maana hapo unajifunza somo muhimu.

2. Kujilinganisha na wengine.

Ukishaanza kujilinganisha na wengine sahahu kuhusu ubora wa hali ya juu au mafanikio makubwa. Hakuna mtu mwenye ndoto kama zako na hakuna mtu mwenye mawazo kama yako au hata uwezo mkubwa ulioko ndani yako. Unapoanza kujilinganisha na wengine mambo mawili yanaweza kutokea; moja kujikuta unakubali mafanikio kidogo kwa sababu wanaokuzunguka hawana mafanikio makubwa, pili, kujikuta unakata tamaa kwa kuona wanaokuzunguka wamefanikiwa sana kuliko wewe. Fuata malengo na mipango yako, usipoteze muda kujilinganisha na wengine.

3. Kuogopa kuhusu watu wengine watakufikiriaje.

Kama kuna maamuzi muhimu unataka kufanya kwenye maisha yako, na unajua maamuzi hayo ndio yatakuwezesha kufikia mafanikio makubwa, yafanye bila ya kujali watu wengine watakufikiriaje. Ukianza kujali watu wengine wanakufikiriaje utajikuta unashindwa kufanya maamuzi sahihi ili uonekane mwema au wa kawaida. Ubaya ni kwamba hakuna anayejali sana kuhusu wewe, ukifanikiwa watakusema na hata ukishindwa pia watakusema zaidi. Hivyo fanya kilicho bora kwako na sio kile ambacho unafikiria kitapendwa na wengi.

4. Kupuuza mawazo yako ya ndani.

Kuna mawazo fulani yapo ndani yetu ambayo yanaweza kutusaidia sana. Unaweza kuwa kuna jambo unataka kufanya lakini mawazo yako ya ndani yanasita sana na kuona sio maamuzi mazuri, mara nyingi mawazo haya yanakuwa sahihi. Kama kuna kitu mawazo yako ya ndani yanakikata sana jaribu kuyafuata, utajiokoa kwenye matatizo mengi. Ila pia kuwa muangalifu mawazo haya yasijekuwa kizuizi kwako kwa kuhofia kila kitu.

5. Kushikilia mambo, badala ya kusonga mbele.

Hakuna kitu kinachoweza kuwa adui mkubwa wa mafanikio kama kushikilia mambo badala ya kusonga mbele. Kwa mfano umeingia kwenye biashara na mtu na kisha mtu huyo akakutapeli, unaweza kuchagua kusahau kuhusu mtu huyo na kusonga mbele kwa kufanya mambo yako kwa juhudi na maarifa zaidi au unaweza kuchagua kuwa unamlaumu mtu huyo kila siku kwamba ndio chanzo cha wewe kushindwa kufanikiwa kwenye biashara. Kuendelea kumlaumu ni kuendelea kupoteza muda wako. Na pia kusonga mbele haimaanishi kutojali yaliyotokea, bali umejifunza na hutorudia tena makosa uliyofanya.

Kuendelea kusoma na kujifunza kuhusu mambo hayo kumi jiunge na KISIMA CHA MAARIFA. Kujiunga bonyeza maandishi hayo, jaza fomu na kisha tuma fedha ya uanachama kwenye namba 0717396253/0755953887

Nakutakia kila la kheri katika safari ya kufikia mafanikio makubwa.

TUPO PAMOJA.

kitabu-kava-tangazo4322