Katika makala za nyuma hapa kwenye KISIMA CHA MAARIFA kwenye kipengele cha kujijengea tabia za mafanikio tumeshajadili sana kuhusu matumizi mazuri ya fedha. Tulijadili mengi sana na hatua kwa hatua jinsi ya kuongeza kpato, jinsi ya kupunguza matumizi na hata jinsi ya kuwekeza ili fedha zako ziweze kukuzalia zaidi na zaidi na zaidi.

Lakini kama wote tunavyojua, matumizi ya fedha bado ni changamoto kubwa kwa wengi. Na ndio maana fedha inabaki kuwa msingi wa matatizo karibu yote duniani. Kuna ambao wanayo na hawajui waitumieje na kuna ambao hawana na hawajui waipateje.

Changamoto zote ambazo unapitia kuhusu fedha zinatokana na kitu kimoja kilichopo ndani yako; TABIA. Tabia zako kuhusu fedha ndio zinakufanya ujikute kwenye wakati mgumu kifedha kila mara. Na kama utakuwa na tabia nzuri basi utaweza kuondokana na sehemu kubwa ya matatizo haya ya kifedha.

Leo hapa kwenye WORLD CLASS tutakumbushana machache kuhusu fedha ili isiendelee kuwa kikwazo kwetu katika kufikia yale malengo yetu makubwa kwenye maisha. Hivi hapa ni vitu kumi muhimu vya kujifunz akw aharaka kuhusu matumizi yako ya fedha na maisha yako kwa ujumla.

1. Ondokana na madeni yote.

Hasa kama madeni haya hayazalishi. Madeni ni sumu kubwa sana kwako kufikia uhuru w akifedha. Kama bado unaingia kwenye madeni ambayo hayazalishi maana yake umeamua kupoteza fedha mwenyewe. Yaani ni sawa na kuweka maji kwenye kikapu, yataingia ila yatavuja na kuisha yote. Unapokuwa mtu wa madeni mifuko yako inaanza kuvujisha fedha, kila fedha utakayoweka itaondoka haraka na kwenda kulipa deni. Ukishalipa deni unaanza tena kukopa. Ondokana na mchezo huu wa kukopa kwa kuanza kupunguza matumizi ambayo sio ya msingi. Angalia kila njia ya kufanya ila kwepa sana kukopa fedha ambayo huendi kuitumia kuzalisha, utakuw aunapoteza fedha zako mwenyewe.

2. Kama ukinunua kitu kilipie mara moja.

Ili kuepuka kuingia kwenye madeni mapya ambayo yataendelea kukupotezea fedha, pale unaponunua kitu kilipie mara moja. Kama huwezi kukilipia jiulize je kitu hiko ni muhimu sana na hakiwezi kusubiri? Kama ni muhimu sana umiza kichwa chako ni jinsi gani utapata fedha ya kulipia kitu hiko. Uzuri ni kwmaba ukiamua kuumiza akili yako ni lazima utapata majibu ya kile unachotaka, ila ukiamua kuilegeza itakupeleka kwenye njia rahisi ambayo ni kukopa.

3. Weka akiba kipato chako, usikitumie hovyo.

Nafikiri huu ndio msingi muhimu sana kuhusu fedha ambao utajifunza kila mara. Weka akiba, tena kabla hujafanya matumizi yoyote yale. Weka sehemu ya kipato chako kama akiba na baadae akiba hii unawez akuiwekeza kwenye miradi mbalimbali inayowez akukuzalishia baadae. Matumizi siku zote huwa hayaishi, hasa pale unapokuwa na fedha, Hivyo kuepuka kuona kila kitu ni muhimu unapokuwa na fedha, hebu anza kuweka kiasi cha fedha pembeni kwanza, kiasi kidogo utakachobaki nacho utalazimika kukitumia vizuri na hii itakuondolea kufanya vitu ambavyo sio muhimu saa kwako.

4.  Sahau kuhusu dili za kutajirika haraka.

Sahau kabisa na wala usitake kusikiliza huu ujinga. Unataka njia ya kuwa tajiri haraka? Haipo. Kama huamini nenda kacheze kamari, utaishia kuliwa fedha zako zote na kuwatajirisha wengine. Wazo lolote la kazi au biashara ambalo halioneshi thamani halisi inayotengenezwa sio wazo zuri na likimbie haraka sana. Ukion amtu anaanza kukushawishi kwamba kuna njia rahisi ya kupata utajiri, kimbia sana maana anataka kukuingiza kwenye shimo baya sana. Kwa binadamu wanavyopenda urahisi, kungekuwa na njia ya kweli ya haraka ya kupata utajiri, kila mtu angeshaijua na angeshaitumia, njia ya aina hii haipo ila ni njia rahisi kwa matapeli kupata fedha zao kutoka kw awajinga. Sasa wewe ni mjanja, usikubali kuingia kwneye hili.

5. Kuwa makini sana kwa unaowakopesha fedha.

Kama hukopeshi kibiashara, basi nawez akukuambia usikopeshe fedha. Kama kuna mtu ana shida sana ya fedha unawez akumsaidia, lakini sio kukopesha. Unapokopesha hasa kwa watu ambao ni wa karibu, unatengeneza nafasi kubwa sana ya kutokurudishowa fedha zako. Unaweza kukataa hili lakini fikiria kw amakini ni watu wangapi wamewahi kukukopa fedha ila ilipofikia kulipa ikawa tatizo. Tena wakati mwingine mnaweza hata kuvunja mahusiano mazuri mliyokuwa nayo awali. Narudia tena kwa msisitizo, kama hukopeshi kibiashara, ambapo utatumia sheria kudai deni lako, na mtu ataheshimu kwa sababu ni biashara, epuka sana kukopesha hasa kw awatu ambao ni wa karibu kwako. Kama mtu ana shida msaidie, vinginevyo, epuka kukopesha. Kukopesha fedha hovyo ni njia rahisi sana ya wewe kujitengenezea umasikini.

Kusoma mambo mengine matano muhimu yaliyobaki jiunge na KISIMA CHA MAARIFA. Kwa kujiunga na KISIMA utapata makala za biashara na ujasiriamali, kujijengea tabia za mafanikio, makala za uchambuzi wa vitabu na makala za jinsi ya kufikia mafanikio makubwa sana (world class). Pia utapata nafasi ya kujiunga na GROUP LA WHATSAPP ambapo utakutana na watu wanaoelekea kwenye mafanikio ambao watakushirikisha mbinu mbalimbali za mafanikio. Bonyeza haya maandishi KUJIUNGA NA KISIMA CHA MAARIFA na utapata maelekezo.

Karibu ujiunge sasa ili uweze kuchukua hatua ya kuboresha maisha yako mara moja. Kumbuka kwamba kadiri unavyochelewa kujiunga na kupata maarifa sahihi ndivyo unavyozidi kuchelewa kufanikiwa kwenye maisha yako. Chukua hatua leo, Jiunge na KISIMA CHA MAARIFA.

Nakutakia kila la kheri katika safari yako ya mafanikio.

TUPO PAMOJA.

Makirita Amani,

makirita@kisimachamaarifa.co.tz

kitabu-kava-tangazo4322