Habari za leo rafiki?
Ni matumaini yangu kwamba upo vizuri na unaendelea kuweka juhudi kubwa kwenye kile ambacho umechagua kufanya kwenye maisha yako. Napenda nikukumbushe ya kwamba mafanikio yako, yapo hapo ulipo sasa, kwenye hicho ambacho umechagua kufanya sasa.
Unaweza kuniuliza kama ndivyo kwa nini mpaka sasa sifanikiwi? Kama mafanikio yapo hapo ulipo, kwenye hicho unachofanya, mbona mpaka sasa maisha yako yapo vile vile? Na hapa ndipo nitakapokupa siri kubwa, ambayo imewarudisha wengi nyuma licha ya juhudi ambazo wamekuwa wanakazana kuweka.

Unahitaji maarifa sahihi na mbinu sahihi ili uweze kupatumia hapo ulipo sasa kufanikiwa. Unahitaji mtazamo mpya wa kuangalia hapo ulipo na mazingira yanayokuzunguka ndiyo uweze kupatumia vizuri kwa mafanikio yako. Kumbuka macho hayawezi kuona kile ambacho akili yako haijui. Ili uweze kuziona fursa, ni lazima kwanza akili yako iwe inajua kuhusu fursa hizo. Ndiyo maana kuna watu wanazaliwa eneo fulani lenye fursa, lakini hawawezi kuzitumia, wanatoka watu mbali na kuja kunufaika nazo.

Hivyo basi rafiki yangu, una kazi kubwa ya kufanya. Una kazi kubwa ya kubadili mtazamo wako kuhusu maisha, kuhusu kile unachofanya na kuhusu mazingira ambayo upo. Una kazi kubwa ya kufanya ili kuzijua fursa mbalimbali zinazokuzunguka hapo ulipo, na jinsi unavyoweza kuzitumia kwa mafanikio yako.

Ni kazi ambayo unaweza kuichagua kuwa fupi au kuwa ndefu.
Kuichagua kuwa ndefu.
Kazi hii ya kupata maarifa na taarifa zitakazokuwezesha kubadili mtazamo wako na kuziona fursa unaweza kuichagua kufanya mwenyewe kwa kujaribu na kukosea. Hapa itakuchukua muda mrefu wa kujaribu mengi na kukosea mengi ili upate machache ya kufanyia kazi.

Kuichagua kuwa fupi.
Lakini pia unaweza kuchagua kazi hii iwe ya muda mfupi, kwa kujifunza kupitia wengine na kupata maarifa bora. Kwa njia hii utaepuka yale makosa ya wengine na hivyo kupunguza muda ambao ungeupoteza kujaribu na kukosea.

Otto von Bismarck  alipata kusema Only a fool learns from his own mistakes. The wise man learns from the mistakes of others. Akimaanisha kwamba wajinga hujifunza kwa makosa yao wenyewe. Werevu hujifunza kwa makosa ya wengine.
Je wewe unataka kuwa upande upi? Kujifunza kwa makosa yako mwenyewe pakee, au kujifunza kupitia wengine? Kama ni mwerevu utapenda kujifunza kupitia wengine, na hapa nina habari njema sana kwako;

Karibu kwenye semina ya MILIONI YA ZIADA.
Tumekuandalia semina ya MILIONI YA ZIADA ambapo kupitia semina hii tutakushirikisha maarifa na taarifa za kukuwezesha kuongeza kipato chako kwa milioni ya ziada kila mwezi hata kama huna mtaji wa kuanzia kwa sasa. Taarifa kamili kuhusu semina hii zipo hapo chini;
Jina la Semina – Inaitwa “MILIONI YA ZIADA”
Itafinyika lini? – Itafanyika Jumapili ya tarehe 30 Octoba, 2016.
Itafanyika kwa muda gani? – Semina itaanza saa 3.45 asubuhi hadi saa 10.27 Jioni
Itafanyika wapi? – Itafanyika Blue Pearl Hotel, Ubungo Plaza, Dar Es Salaam.
Ada ni Tshs ngapi? – utalipia Tshs 35,000 tu na utapata yafuatayo:
1.     Chakula kwa mtu mmoja
2.     Notibuku ya kuandika
3.     Kalamu ya kuandikia
4.     Mafunzo ya biashara kwa njia ya email na sms
5.     Utaingia kwenye kundi maalumu la wafanyabiashara ndani ya FaceBook
6.     Utakuwa ukipatiwa taarifa mbalimbali zitakazo kusaidia kukuza au kuanzisha biashara.
7.     Fursa ya ku network na wafanyabiashara wenzako.
8.     Utapata mafunzo ya jinsi ya kuingiza angalau “Milioni Ya Ziada” kila mwezi
Unalipia wapi? – Utalipa kwa njia ya simu kwenye namba 0755 953 887 au 0717 396 253. Majina ni Amani Makirita. Ukishafanya malipo tuma ujumbe wenye majina yako kamili, namba ya simu na email yako kisha utatumiwa au kuletewa tiketi yako.

Kuwa mwerevu na jifunze kupitia wengine. Karibu sana kwenye semina hii ili uweze kupata maarifa sahihi ya kuongeza kipato chako kwa kuanzia hapo ulipo sasa.
Pata tiketi yako sasa, nafasi ni chache sana.
Kila la Kheri Rafiki Yangu.
Rafiki na Kocha wako,
Makirita Amani,
Kwa ushauri na Coaching bonyeza maandishi haya kupata utaratibu.
Kwa kupata vitabu vya biashara na mafanikio tembelea MOBILE UNIVERSITY (bonyeza hayo maandishi.)
Kupata blog ya kitaalamu unayoweza kuitumia kutengeneza kipato tembelea MTAALAMU NETWORK