Habari za leo rafiki?
Nachukua nafasi hii kukukumbusha ya kwamba imebaki siku moja pekee ili kujipatia tiketi yako ya kushiriki semina ya MILIONI YA ZIADA. Mwisho w akupata tiketi za semina hii ni kesho tarehe 28/10/2016, hivyo kama bado hujapata tiketi yako, chukua hatua leo ili usikose nafasi hii ya kipekee.
Kwenye makala hii ya leo nakuletea wasifu wa watakaofundisha kwenye semina hii, pamoja na mada watakazofundisha kwenye semina ya MILIONI YA ZIADA. Jisomee mwenyewe sifa za watu hawa wanne, na uone kama kuna kitu kikubwa unaweza kujifunza kutokana na ujuzi na uzoefu wa watu hawa kwenye biashara mbalimbali wanazofanya.

Kabla hatujaingia kwenye wasifu wa walimu wa semina ya milioni ya ziada, naomba nijibu maswali mawili muhimu ambayo sikuyajibu kwenye makala ya jana. Jana nilitoa makala yenye maswali na majibu kuhusu semina, lakini kuna haya mawili nimeona ni muhimu ila sikuwa nimeyajibu, naomba niyajibu hapo chini ili kuweka mambo sawa.

Swali; Ahsante coach ni sahihi kama nitalipia siku ile  ya semina (mlangoni)
Hapana, kusubiri ulipe mlangoni utaikosa nafasi. Kuna maandalizi muhimu yanapaswa kufanywa kabla ya siku ya semina, mfao vifaa vya kia mshiriki wa semina kuandikia, pia maandalizi ya chakula. Hivyo tunahitaji kuwa na idadi kamili ili kufanya maandalizi mazuri. Ndiyo maana mwisho wa kufanya malipo ya semina ni ijumaa tarehe 28/10/2016. Chukua hatua sasa ya kulipia tiketi yako ili usikose nafasi hii nzuri.

Swali; Habari kaka Amani, nikushukuru kwa jitihada zako za kutuelimisha, nina swali moja kuhusiana na semina hii, hakuna uwezekano wa kupata audio ya semina hio kwa watu walioko mikoani pengine kwa gharama ileile ya 35? 
Hapana, uwezekano wa kuandaa audio haupo, kama nilivyoelekeza kwenye maswali na majibu yaliyopita, kuandaa hizi audio au video na kuzisambaza ni kazi nyingine inayohitaji muda wa kutosha, kitu ambacho kwa sasa hatutaweza kufanya. Tutaandaa webinar, maelekezo muhimu kuhusu webinar hii tutayatoa baadaye.

Karibu kwenye wasifu wa walimu watakaofundisha kwenye semina ya MILIONI YA ZIADA.

Wasifu wa Faithvictory Kivea
Ni mfanyabiashara wa kusindika vyakula, matunda na mboga mboga kwa muda mrefu.  Pia Mrs Kivea hufundisha na kushauri wafanyabiashara wenye mtaji mdogo kuwawezesha wakuze mitaji yao. Kingine ni kuwa anajihusisha na kutoa mikopo kwa wafanyabiashara wadogo maeneo ya Kibamba, Dar Es Salaam. Amekuwa akifanya hivi kwa mafanikio makubwa.
Mrs Kivea, atafundisha mada zinazohusu kugeuza mtaji mdogo na kuwa mtaji mkubwa. Timu yetu inaamini kwa kiasi kikubwa utamfurahia na kujifunza vitu muhimu sana kuelekea kujitengenezea angalau milioni ya ziada kila mwezi. Karibu ujifunze kutoka kwake.

Wasifu wa Michael Mwakilasa.
Yeye ni mfanyabiashara aliyebobea katika uzalishaji wa mafuta ya diseli kutumia mabaki ya mafuta migahawani na mahotelini. Mr Mwakilasa ni Mtanzania wa kwanza kabisa kuanzisha kiwanda cha kuzalisha diseli.
Mr Mwakilasa, ameishi nchini Marekani kwa zaidi miaka 23, kwa hiyo, Mbali na uzoefu na utaalamu wa kuzalisha mafuta ya Diseli, Mr Mwakilasa ana uzoefu mkubwa wa biashara kwa kufanya kazi katika mashirika makubwa nchini Marekani na Canada.
Mr Mwakilasa atazungumzia mambo muhimu ya uanzishaji viwanda vidogo. Atachangia uzoefu wake na pia kuwapa mbinu kwa wale wafanyabiashara wadogo wanaotaka kuanzisha viwanda vidogo. Pia atatoa mbinu mbali mbali ambazo zitakusaidia kukupeleka kwenye lengo lako la kutengeneza angalau Milioni Moja ya Ziada kwa Mwezi.

Wasifu wa Makirita Amani.
Makirita Amani ni mwandishi, mshauri na mjasiriamali. Ni mwanzilishi na mwendeshaji wa mitandao ya AMKA MTANZANIA na KISIMA CHA MAARIFA, mitandao ambayo inatoa elimu, maarifa na hamasa ya kujitambua na mtu kuchukua hatua juu ya maisha yake mwenyewe.
Makirita ni mkurugenzi wa kampuni ya uwekezaji inayoitwa KICHAMATA INVESTMENT COMPANY, kampuni inayowekeza kwenye kilimo biashara. Kampuni hii ina wawekezaji kutoka sehemu mbalimbali Tanzania.
Makirita ni mwandishi wa kitabu, BIASHARA NDANI YA AJIRA, Jinsi ya kuanzisha na kukuza biashara yako ukiwa bado umeajiriwa. Amekuwa akitoa ushauri na kufundisha kuhusu biashara, utambuzi binafsi na mafanikio.
Kwenye semina hii Makirita atafundisha jinsi ya kuanza biashara kutokea sifuri hata kama huna mtaji. Atafundisha mambo muhimu ya kuzingatia pale unapoanza biashara yako ili uweze kuikuza na kukuletea mafanikio.
Pia Makirita atakushirikisha hatua sita muhimu za kufuata ili uweze kuanza biashara na kufikia faida ya zaidi ya milioni moja kila mwezi.
Usikose nafasi hii ya kujifunza jinsi unavyoweza kuanza biashara yako ukiwa hapo ulipo sasa.

Wasifu wa Felix Maganjila
Ni mmoja wa washauri na walimu wenye uzoefu wa muda mrefu katika biashara za ndogo na za kati hapa Afrika Mashariki. Yeye anamiliki blogu ya www.napendabiashara.co.tz na pia ni mmiliki wa mfumo kabambe  wa kumsaidia mfanyabiashara kuongeza mauzo bila kuwekeza pesa nyingi. Mfumo huu unapatikana www.makeyoursalesgrow.com
Kabla ya kuanza kutoa ushauri na mafunzo kwa wafanyabiashara, yeye mwenyewe pia amefanya biashara mbalimbali hapa Tanzania. Pia amefanya biashara wakati akiishi Nairobi, Kenya kabla hajarudi Tanzania moja kwa moja.
Katika uzoefu wake wa miaka 20 wa kushauri na kufundisha, ameshaweza kuwasaidia wafanyabiashara wengi kupata mafanikio.
Mfano, aliweza kuisaidia kampuni Fulani kukuza mauzo kutoka Tshs Milioni 200 kwa mwezi hadi milioni 800 katika kipindi kisichozidi miezi 6. Pia aliweza kusaidia kampuni nyingine kuongeza mauzo kutoka Tshs milioni 8 kwa mwezi hadi Milioni 30 kwa Mwezi ndani ya mwezi 3.
Kwa kampuni ndogo, aliweza kumsaidia mfanyabiashara kukuza mtaji kutoka Tshs 300,000 hadi milioni 5 ndani ya miezi 5
Katika semina hii Maganjila atakufundisha yafuatayo yatakayokusaidia kukuza pato lake:
·        Kanuni kuu ya kukuza mtaji wako hata kama ni mdogo
·        Utajifunza mbinu ya kuweka akiba ambayo haifundishwi mahali popote.
·        Mfumo bora kabisa duniani wa kutumia, kutunza na kusimamia pesa zako. Hii ni siri ambayo watu wengi waliofanikiwa hawataki uijue kwani wanaogopa na wewe kutajirika.
·        Hatua sita za kufuata zitakazokuza kipato chako na kukuacha unashangaa kwa nini hujaijua siri kwa muda mrefu. Kufahamu siri hii, itakufanya uwe tofauti sana kimapato.
·        Mambo 9 ya kufanya kuweza kuongeza pato lako haraka na kwa kiasi kikubwa
Pata tiketi yako sasa uweze kugundua siri za kukubadilisha maisha yako.

Imabeki siku moja pekee kupata tiketi yako, kesho ndiyo siku ya mwisho kwako kupata tiketi ya kushiriki semina ya MILIONI YA ZIADA. Kupata tiketi yako leo, ili uweze kupata maarifa haya mazuri kutoka kwa walimu hawa wanne, chukua hatua sasa.
Kupata  tiketi tuma ada ya kushiriki semina tsh 35,000/= kwenda namba 0717 396 253 au 0755 953 887 kisha tuma ujumbe wenye majina yako kamili, namba ya simu na sehemu ulipo ili uweze kuandaliwa na kuletewa tiketi.

Chukua hatua sasa rafiki, hii ni nafasi ambayo hupaswi kuikosa kabisa kwenye maisha yako.
Karibu sana kwenye semina ya MILIONI YA ZIADA.
Rafiki na Kocha wako,
Makirita Amani,
makirita@kisimachamaarifa.co.tz