3135; Utamchagua nani?
Rafiki yangu mpendwa,
Safari yetu ya mafanikio makubwa tunayoyataka inawategemea sana watu.
Hakuna namna tunaweza kufikia mafanikio makubwa kabisa sisi peke yetu.
Kadiri lengo letu la mafanikio linavyokuwa kubwa, ndivyo pia idadi ya watu tunaowahitaji inavyokuwa kubwa zaidi.
Hivyo sehemu kubwa sana ya maamuzi utakayokuwa unayafanya kila siku ni kuhusu NANI (WHO) na siyo NINI (WHAT) au VIPI (HOW).
Ili kulitafakari hilo vizuri, fikiria mifano hii mitatu;
Moja; fikiria umeambiwa hutaruhusiwa tena kufanya kazi kwa maisha yako yote. Unatakiwa umchague rafiki yako mmoja ambaye utapata asilimia 10 ya kipato chake kwa kipindi chote cha maisha yako kilichobakia.
Je utamchagua rafiki yupi ambaye una uhakika kwamba kwa mwenendo wake utaweza kufikia malengo uliyonayo?
Nini kimekufanya umchague rafiki huyo?
Kama kwa marafiki ulionao sasa huoni ambaye upo tayari kumchagua, ni mtu mwenye sifa zipi ambaye utakuwa tayari kumchagua kwenye zoezi hilo?
Majibu uliyojibu hapo, ndizo tabia ambazo wewe mwenyewe unapaswa kuwa nazo.
Kwa sababu kwa kuwa na tabia hizo, utawavutia wale wenye tabia za aina hiyo na mtaweza kuambatana kwenye safari ya mafanikio makubwa kwenye maisha.
Mbili; fikiria wateja wote ulionao kwenye biashara yako wanaondolewa na unaachiwa mteja mmoja tu.
Mteja huyo mmoja ndiyo wateja wengine wote wa biashara yako watatokea kwake.
Je utamchagua mteja yupi ambaye una uhakika kwamba kupitia yeye utaweza kupata wateja wengine bora?
Nini kimekufanya umchague mteja huyo?
Kama kwa wateja ulionao sasa huoni ambaye upo tayari kumchagua, ni mteja mwenye sifa zipi ambaye utakuwa tayari kumchagua kwenye zoezi hilo?
Utamtunzaje huyo mteja ili uweze kupata wengine wengi kupitia yeye?
Majibu uliyojibu hapo, ndizo tabia ambazo unapaswa kuziangalia kwa wateja na jinsi unavyopaswa kwenda nao.
Tatu; fikiria wafanyakazi wote ulionao kwenye biashara yako wanaondolewa na unaachiwa mfanyakazi mmoja tu.
Wafanyakazi wengine wote unaowahitaji watatoka kwa mfanyakazi huyo mmoja.
Je utamchagua mfanyakazi yupi ambaye una uhakika kwamba kupitia yeye utaweza kupata wafanyakazi wengine bora?
Nini kimekufanya umchague mfanyakazi huyo?
Kama kwa wafanyakazi ulionao sasa huoni ambaye upo tayari kumchagua, ni mfanyakazi mwenye sifa zipi ambaye utakuwa tayari kumchagua kwenye zoezi hilo?
Utamtunzaje huyo mfanyakazi ili uweze kupata wengine wengi kupitia yeye?
Majibu uliyojibu hapo, ndizo tabia ambazo unapaswa kuziangalia kwa wafanyakazi na jinsi unavyopaswa kwenda nao.
Rafiki, naamini zoezi hilo limekupa mwanga wa tofauti kabisa juu ya watu wa kushirikiana na kuambatana nao kwenye maisha yako ili kupata mafanikio makubwa unayoyataka.
Tumia zoezi hili kama msingi wako mkuu wa kuchagua watu sahihi na kujua jinsi ya kwenda nao ili uweze kupata matokeo unayoyataka.
Watu ndiyo watakaojenga au kuvunja mafanikio yako.
Lakini bado huwezi kuwalaumu watu kwa chochote kwenye maisha yako, kwa sababu ni wewe ndiye unayewachagua, iwe unajua au hujui.
Wajibu wako mkubwa ni kuwachagua watu sahihi ambao unajua kwa mwenendo wao watajenga mafanikio yako na siyo kuyabomoa.
Weka juhudi kubwa kwenye kupata na kujenga watu sahihi, huku ukijua huwezi kuwabadili watu, ndiyo maana unatakiwa kuanza na wale ambao tayari ni sahihi.
Maamuzi ya NANI yatakuwa endelevu kwa maisha yako yote.
Kuna ambao utawashusha kwenye basi, yaani kuachana nao kwa sababu umeona hawajengi bali kubomoa na kuna ambao utawapakiza kwa sababu kuna vitu umeona kwao.
Zoezi la kushusha na kupandisha watu litakuwa endelevu kwenye maisha yako.
Usilichukulie kama kushindwa.
Ni sehemu ya kawaida kabisa kwenye safari yako ya mafanikio, kwa sababu mpaka uwapate watu sahihi kabisa huwa inachukua muda.
Kitu muhimu kujua wakati wote ni watu sahihi wapo, ni vile tu unakuwa hujaamua ni watu wa aina gani unaowataka na kuweka kazi na muda katika kuwafikia na kuwashawishi kwenda nao.
#NidhamuUadilifuKujituma
#AfyaUtajiriHekima
#KaziUpendoHuduma
#UpekeeUdadisiUbunifu
#UshirikianoUtegemeanoUwajibikaji
#BilioneaMafunzoni
#NajengaBiashara
#HakunaKingineMuhimu
#LazimaNitoboe
#NawekaKaziNifanikiwe
Asante kocha.
LikeLike
Karibu
LikeLike
Watu sahihi wapo. Ni suala la muda tu kupata watu hao.
Hivyo zoezi la kupanda na kushushwa watu kwenye basi halifikia kikomo.
Asante sana Kocha Dr Makirita Amani
LikeLike
Ndiyo
LikeLike
Watu sahihi wapo, kinachotakiwa ni kuwatambua na kuwachagua kisha kuweka muda wa kutosha kuwafuatilia na kuwatunza.
LikeLike
Ndiyo.
LikeLike
Nachagua watu wenye sifa na tabia ninazozitaka ili niweze kwenda katika safari ya kujenga biashara n maisha na pale watakapoenda tofauti itabidi niachane nao na niendelee kutafuta walio bora zaidi ili wale wasio na vigezo wasinikwamishe katika safari yangu.
LikeLike
Vizuri
LikeLike
Kuwachagua watu sahihi na wateja sahihi na kuanzia hapo
LikeLike
Ndiyo
LikeLike
Watu ndio watakaojenga au kubomoa mafanikio yangu.Swali la msingi nitamchagua nani?
LikeLike
Muhimu sana.
LikeLike
ahsante
katika kushusha na kupandisha usiisikilize jamii jisikilize wewe. jamii itakuhukumu sana na kukuona wewe ndio sio sahihi. bila kujua yanayoendelea ndani
LikeLike
Ukisikiliza jamii kwenye jambo lolote lile, tayari unakuwa umeshapotea.
LikeLike
Asante kocha,Swali la msingi nitamchagua nani? Nikwenda na mfumo ndo utaweza kunipa vigezo sahihi nani nimchague.na kwenye mafanikio kuna vikwazo vingi ukisikiliza matakwa ya kila mtu.
LikeLike
Kabisa.
LikeLike
Asante sana kocha, nitachagua (Nani)watu sahihi wa kufanya nao kazi maana biashara yangu inahitaji watu sahihi.
LikeLike
Vizuri sana.
LikeLike
Nitachagua watu sahihi ambao wana sifa na tabia ninazo zitaka nakuachana na wale ambao ni mzigo kwangu
LikeLike
Vizuri sana.
LikeLike
Vizuri
LikeLike
Mzunguko wa watu sahihi na wale wasio sahihi kwenye maisha yangu unategemeana na tabia zangu mwenyewe. Tabia zangu zikiwa njema nitapata watu bora wa kuambatana nao, tabia zangu zikiwa za hovyo nitawapata watu ea hovyo. Hivyo kupanga ni kuchagua.
Asante sana Kocha.
LikeLike
Huo ndiyo ukweli.
LikeLike
Hakika.
LikeLike
Watu sahihi wapo tunatakiwa kupata ili kufikia malengo yetu makuu ambaauo mi ubilionea
Asante sana
LikeLike
Ndiyo.
LikeLike
Hakika
LikeLike
Weka juhudi kubwa kwenye kupata na kujenga watu sahihi, huku ukijua huwezi kuwabadili watu, ndiyo maana unatakiwa kuanza na wale ambao tayari ni sahihi.
LikeLike
Ndiyo.
LikeLike
Ndiyo
LikeLike
Vizuri.
LikeLike
Ni kweli kabisa. Safari ya mafanikio inahitaji watu.
Kupata watu sahihi wa kwenda nao Ni mchakato. Kupakiia na kushiusha abiria na kupakiza abiria hakuna ukomo.
Nimelijua hilo kwa hiyo halitanisumbua.
LikeLike
Vizuri sana.
LikeLike
watu sahihi wapo, ni kuendelea tu kuwatafuta bila kukata tamaa
LikeLike
Ndiyo
LikeLike
Kitu muhimu kujua watu sahihi wapo tuwatafute.
LikeLike
Ndiyo
LikeLike
Mtapambana kuweka watu sahihi mara zote
LikeLike
Vizuri
LikeLike
Nitaendelea kuwatafuta watu sahihi hadi nitakapowapata maana ndiyo watakaonifikisha kwenye malengo yangu.
LikeLike
Vizuri
LikeLike
Watu sahihi wapo
LikeLike
Ndiyo
LikeLike