Karibu sana kwenye mazungumzo yetu ya leo ambapo mimi na wewe tunakwenda kujadili mambo muhimu kuhusu maisha bora, yenye furaha na mafanikio makubwa. Haya ndiyo matarajio ya kila mmoja wetu, na ndiyo yanayotusukuma kufanya kile ambacho tunakifanya. Japo mwisho wa siku, ni wachache wanaofikia matarajio hayo, na hii inatokana na wengi kukosa msingi sahihi wa kuyaendea maisha yao.
Kuna vitu vingi unaweza kuona wengine wanafanya na ukaona ni rahisi sana kufanya, lakini kila ukijaribu kufanya wewe unashindwa.
Unapowaona wengine wanafurahia kufanya na wanafanya kama sehemu ya maisha yao, unajaribu wewe unashindwa, ndipo unapoweza kupata hisia kwamba huenda wale wanajua kitu ambacho wewe hujui.
Na nikuambie tu kitu rafiki yangu, hisia zile ni za kweli, ni kweli kwamba wanajua vitu ambavyo wewe hujui, na wanajua misingi ya kuyaendea maisha yao. Wewe unaweza kuona wakifanya, ukajaribu na kushindwa kwa sababu huna msingi.
Leo hii nataka kuongea na wewe kama kweli maisha bora, yenye furaha na mafanikio ndiyo hitaji lako. Kama huna hitaji hilo unaweza usiendelee kusoma kwa sababu hutapata manufaa yoyote.
Ninachokwenda kukuambia leo ni sehemu sahihi ya wewe kuwepo, kama kweli unataka kuishi maisha ya mafanikio, na siyo tu mafanikio ya kawaida, bali yenye furaha kubwa.
SOMA; Maswali Manne (4) Yakujiuliza Ili Uweze Kuongeza Ustawi Wa Biashara Yako.
Kila siku huwa napokea email za aina hii;
“Nina mtaji wa shilingi laki nne, naomba unishauri nifanye biashara gani?”
“Nina watu wa kunisapoti kwa mtaji, lakini sijui biashara gani nikifanya itaniletea faida nzuri.”
“Nataka kuacha kazi na kujiajiri, nimekaa kwenye ajira miaka mingi sioni mbele, tafadhali nishauri njia bora za kufuata.”
“Sina kazi na sina mtaji, nyumbani uwezo ni mdogo, naomba unishauri nawezaje kutoka kimaisha?”
Hayo ni baadhi tu ya maombi ambayo napokea kila siku kutoka kwa wasomaji na marafiki wenzetu ambao wanakuwa wamekwama kwa namna moja au nyingine.
Naweza kuwapenda sana marafiki zangu hawa na kuwaandikia kipi wafanye, lakini nitakuwa sijawasaidia, kwa sababu tatizo lao si ni nini wafanye, bali tatizo lao ni kukosa msingi wa maisha ambao wanaweza kuufuata mpaka wakafanikiwa.
Tatizo siyo kukosa wazo la biashara, bali tatizo ni kukosa mfumo bora wa maisha na kibiashara utakaomwezesha mtu kuanzisha biashara inayomfaa yeye na itakayomletea faida kubwa.
Hivyo njia pekee ambayo naweza kuwasaidia marafiki zangu hawa, ni kuwakaribisha kwenye KISIMA CHA MAARIFA. Kwa kuwa ndani ya KISIMA, kila siku tunajifunza hatua bora za kuchukua ili kuimarisha aisha yetu ya mafanikio. Ndani ya KISIMA mafanikio siyo mali na fedha pekee, bali mafanikio ni kwenye maeneo matano muhimu ya maisha yetu.
Na hii ndiyo sababu nasema kama kweli una kiu ya maisha ya mafanikio, basi sehemu sahihi ya wewe kuwepo ni kwenye KISIMA CHA MAARIFA. Kwenye KISIMA, unayajenga yale maisha yanayokufaa wewe. Kwenye KISIMA unakutana na watu mbalimbali, waliopo sehemu mbalimbali na wanaojua ni wapi wanakwenda na watafikaje pale.
Nitumie nafasi hii kukukaribisha kwenye KISIMA CHA MAARIFA kama bado hujawa mwanachama. Ndani ya KISIMA CHA MAARIFA kila siku ni kujifunza, kila siku ni kupiga hatua.
SOMA; Una Mtaji Lakini Hujui Ni Biashara Gani Ufanye? Soma Hapa Kujua.
Na misingi yetu kwenye KISIMA CHA MAARIFA ni hii. NIDHAMU, UADILIFU na KUJITUMA. Kwenye kila jambo tunalofanya kwenye maisha yetu, misingi hiyo mitatu inatuongoza. Hii ni misingi muhimu sana kwa mafanikio yetu.
Mwaka huu 2017 tuna maneno matatu yanayotuongoza kwenye maisha yetu ya mafanikio.
Maneno hayo ni KUTHUBUTU, USHINDI NA SHUKRANI. Ni maneno matatu rahisi kutamka lakini yana uzito mkubwa sana kwenye maisha yetu. Kwa kuzingatia maneno hayo matatu kila siku, na kutumia misingi mitatu ya maisha, chochote unachofanya, lazima utafanikiwa.
Utaacha kuuliza nifanye nini ili kufanikiwa na utaanza kuchukua hatua kwa kila kinachokuzunguka.
Nawezaje kujiunga na KISIMA CHA MAARIFA?
Kama bado hujajiunga na KISIMA CHA MAARIFA basi utaratibu wa kujiunga uko hivi; unalipa ada ya mwaka ambayo ni tsh elfu 50 (50,000/=) ada hii inaisha pale mwaka unapoisha , tangu siku uliyojiunga. Kwa ada hii kila siku utajifunza kupitia makala na shuhuda za wengine. Pia utapata mafunzo mbalimbali ya semina kwa njia ya mtandao. Na muhimu zaidi, inakuwa rahisi kwako kuwasiliana na mimi moja kwa moja, kwa changamoto yoyote unayokutana nayo.
Kujiunga, tuma ada yako tsh 50,000/= kwa TIGO PESA 0717 396 253 au MPESA 0755 953 887 Kisha tuma ujumbe kwenye wasap namba 0717396253 wenye majina yako kamili na email yako na utaunganishwa kwenye KISIMA CHA MAARIFA.
Karibu sana rafiki, tusafiri pamoja kwenye safari hii ya mafanikio.
Kila la Kheri Rafiki Yangu.
Rafiki na Kocha wako,
Makirita Amani,
Kama umejifunza kupitia makala hii karibu tujifunze zaidi kupitia KISIMA CHA MAARIFA, ambapo utaingia kwenye kundi la wasap na kupata mafunzo kila siku. Bonyeza maandishi haya kujiunga na KISIMA CHA MAARIFA.
Kwa kupata vitabu vya biashara na mafanikio tembelea MOBILE UNIVERSITY (bonyeza hayo maandishi.)
Pata kitabu BIASHARA NDANI YA AJIRA ujifunze jinsi unavyoweza kuanzisha na kukuza biashara yako, pia utajifunza mifereji nane(08) ya kipato unayopaswa kuwa nayo ili kufikia uhuru wa kifedha. Bonyeza maandishi haya kupata kitabu.