Watu wengi wa enzi za roma, watu waliamini ya kwamba, hatima ya mtu imeshapangwa. Yaani hata ufanye nini, hakuna namna unavyoweza kubadili hatima ya maisha yako. Na hii ilipelekea wengi kutokuhamasika kuchukua hatua kubwa kwenye maisha yao.

Lakini wastoa walijua namna bora ya kutumia hilo, badala tu ya kukubali na kutochukua hatua, wao walichukua hatua, lakini walikubali matokeo ambayo wanayapata.
Wastoa wamekuwa ni watu ambao hawalazimishi mambo yaende kama wanavyotaka wao, bali wao wanaweka juhudi kubwa lakini wanakubali matokeo wanayopata.

Wastoa wanasema kufikiria juu ya yale yaliyopita, iwe tu ni kwa kujifunza lakini siyo kutamani kubadili, maana huwezi. Na pia kufikiria kubadili wakati ulionao sasa nako pia ni kupoteza muda.
Unachopaswa kufanya, ni kupokea yale matokeo uliyopata, na kuona namna gani unayatumia vizuri zaidi.

Usilazimishe mambo yaende kama unavyotaka mwenyewe, kila mara utaumia. Badala yake pokea mambo kama yanavyotokea na angalia unawezaje kuyatumia vizuri, na hapo utakuwa na maisha bora kila siku.