Biashara zote zenye mafanikio, zinajengwa kwenye vitu viwili vikuu;
- Bidhaa au huduma nzuri.
- Wateja wanaojirudia.
Unahitaji kuwa na bidhaa au huduma nzuri, siyo nzuri kwa sura, bali nzuri kwa uhitaji wa watu. Kile unachouza lazima kiwe kinatatua tatizo au kutimiza mahitaji ya wateja wako. Kiwe na thamani kwao inayowafanya kuwa tayari kutoa fedha zao, ambazo wamezipata kwa shida, kukinunua. Bila ya bidhaa au huduma nzuri, biashara haiwezi kuwepo.
Unahitaji kuwa na wateja wanaojirudia ili kuweza kutengeneza biashara yenye mafanikio. Kupata mteja anayekuja mara moja siyo ngumu, unaweza kuwahadaa watu wakaja kwenye biashara yako mara ya kwanza, ila mteja anaporudi tena na tena, ina maana ameikubali biashara, ina thamani kwake na hivyo kurudi tena. Wateja hawa ndiyo wanaokuletea mafanikio kwenye biashara yako, kwa sababu hutumii gharama kubwa kuwaleta tena, na wao wanawaleta wengine wengi zaidi.
SOMA; Hivi Ndivyo Unavyoweza Kujenga Biashara Kubwa Ya Wateja Wanaolipa Fedha Taslimu Na Siyo Mikopo.
Kitu muhimu kuelewa ni kwamba, vitu hivi viwili vinategemeana sana. Kwa sababu bila ya bidhaa au huduma bora, wateja hawawezi kurudi tena kwenye biashara yako. Hivyo lazima bidhaa au huduma unayotoa iwe bora, ili mteja anapokuja mara moja, ashawishike kuja tena mara nyingine na nyingine.
Bidhaa/huduma bora, na wateja wanaojirudia, kumbuka haya kila siku, na nguvu zako za kukuza biashara yako, zielekeze kwenye kuboresha unachotoa, na kujenga wateja ambao wanaiamini biashara.
Kila la Kheri Rafiki Yangu.
Rafiki na Kocha wako,
Kwa kupata vitabu vya biashara na mafanikio tembelea www.kisimachamaarifa.co.tz/vitabu
Kupata blog ya kitaalamu unayoweza kuitumia kutengeneza kipato tembelea www.mtaalamu.net/patablog

Asante coach. BIDHAA + HUDUMA UNAYO TOA + MTEJA ANAYEJIRUDIA =BIASHARA YENYE MAFANIKIO MAKUBWA..kwa hiyo coach hapa basi tuseme in vitu vitatu na sio viwili tena vinavyojenga biashara yenye mafanikio kwa makala hii.
LikeLike
Asante sana Kocha nina Swali dogo Hapa, Kama bidhaa au huduma unayotoa haina marudio tena yaani mteja akishanunua bidhaa hiyo kurudi tena ni hadi bidhaa iharibike au tatizo lijirudie. Kwa Mtu kama huyu inakuwaje kwa hawa wateja wanaojirudia rudia?
LikeLike
Mfanyabiashara yeyote, anapaswa kuitengeneza biashara yake kwa mfumo ambapo mteja atarudi tena.
Iwe ni kurudi kwa bidhaa au huduma kama aliyonunua mwanzo, au kurudi kwa kupata vitu vingine.
Mfano mzuri angalia makampuni ya utengenezaji wa simu, mfano Apple, ambao wanatengeneza iPhone, mteja akinunua iphone yake, anaweza kukaa nayo muda mrefu bila kuhitaji nyingine. Sasa wanachofanya ni kuja na matoleo mapya, ambayo yameboreshwa kidogo tu na watu wanapata uhitaji wa kununua tena.
Hivyo kwa biashara yoyote, unapaswa utengeneze namna mteja atarudi tena, iwe ni kwa kile alichonunua ua kingine ambacho atahitaji.
LikeLike