Hebu fikiria ni kitu kikubwa kiasi gani unachoweza kutengeneza kama hutaacha kufanya.

Fikiria kama utaweka kazi kwenye biashara yako kila siku bila kuacha hata siku moja, ni biashara kubwa kiasi gani ambayo utaijenga.

Fikiria kama utafanya mazoezi kila siku bila kuacha, ni afya bora na mwili imara kiasi gani ambao utajijengea.

Fikiria kama utaendelea kujifunza vitu vipya kila siku bila ya kuacha, ni uelewa kiasi gani ambao utajijengea, na utakaokuwezesha kupiga hatua kubwa.

Hakuna chochote utakachofanya mara moja pekee kikakupa matokeo makubwa, lakini kile ambacho utafanya kila siku bila ya kuacha, lazima kitakupa matokeo makubwa.

Hivyo usiangalie sana ni matokeo gani unayapata kwa kufanya mara moja, bali angalia matokeo utakayotengeneza kwa kufanya kila siku, kisha amua kufanya kila siku bila kuacha hata siku moja.

Fanya kila siku na utapata matokeo bora sana.

Kila la Kheri Rafiki Yangu.

Rafiki na Kocha wako,

Dr. Makirita Amani,

www.amkamtanzania.com/kocha