
Maoni ni kitu rahisi kila mtu kuwa nacho, lakini wengi walio na maoni hawajayatengeneza wao wenyewe, badala yake wamechukua ya wengine.
Wachache wanaotengeneza maoni yenye maslahi kwao, huwa wanayasambaza kwa kasi kama propaganda kwa kuwa wanajua wengi ni wavivu wa kujifunza, kuujua ukweli na kuwa na maoni sahihi.
Kwa kuwa mambo ni mengi, usijisumbue kuwa na maoni kwenye kila kitu, badala yake chagua yale maeneo machache na muhimu kabisa kwako, jifunze kwa ndani na kuyaelewa kwa kina, kisha jenga maoni yako.
Maoni hayo ndiyo yatakayokusaidia kwenye kufanya maamuzi kwenye eneo hilo. Kama unataka kufanya maamuzi, lazima kwanza uanze na maoni sahihi, ujiyojijengea mwenyewe.
Ukurasa wa kusoma ni kuhusu kufanya kila kitu kwa kusudi, fungua; http://www.kisimachamaarifa.co.tz/2021/02/08/2231
#NidhamuUadilifuKujituma #AfyaUtajiriHekima #KaziUpendoHuduma