
Kueleweka au kukubalika na watu wote ni kitu ambacho hakiwezi kutokea.
Hata kama unafanya jambo lenye manufaa kiasi gani, kuna ambao wataona ni bora ungefanya jambo jingine wanaloona lina manufaa zaidi.
Hivyo msingi wako kwenye yale unayofanya haupaswi kuwa kukubalika na kila mtu, badala yake unapaswa kuwa ni kufanya kilicho sahihi na kuwalenga wale wanaokubaliana nacho na ambao kinawanufaisha.
Kufanya kilicho sahihi na kutoa thamani kwa wengine ni jambo lililo ndani ya uwezo wako. Kutaka kumridhisha kila mtu ni jambo lisilo ndani ya uwezo wako.
Hangaika na lililo ndani ya uwezo wako na achana na lililo nje ya uwezo wako.
Ukurasa wa kusoma ni kuweka sifa pembeni ili kufanya makubwa; http://www.kisimachamaarifa.co.tz/2021/04/14/2296
#NidhamuUadilifuKujituma #AfyaUtajiriHekima #KaziUpendoHuduma