#SheriaYaLeo (53/366); Fyonza Nguvu Yenye Kusudi.

Katika safari yako ya kufikia ubobezi wa hali ya juu na mafanikio makubwa, unapaswa kuzungukwa na watu wenye nguvu ya kusudi na wanaopambana kufikia makubwa pia.

Watu unaojihusisha nao, wanavyonza nguvu yako na wewe unafyonza nguvu yao pia.
Kama utazungukwa na watu waliokata tamaa na ambao hakuna makubwa wanayofanya, ndivyo nawe utakavyokuwa.

Chagua kwa makini watu gani unaoshirikiana nao na unaojifunza kutoka kwao pamoja na kupokea ushauri wao.
Chagua wale ambao nguvu iliyo ndani yao ina kusudi kubwa na inakusukuma zaidi kufanya makubwa.

Epuka sana wale ambao hawajui kusudi la maisha yao, hawana ndoto kubwa na hakuna makubwa ambayo wamefanya, hawa watakurudisha nyuma.

Tengeneza timu sahihi kwako ili ikusukume kufanya makubwa.

Sheria ya leo; Tengeneza orodha ya watu kwenye maisha yako ambao wanaishi kwa kusudi. Weka kipaumbele kutumia muda wako mwingi na watu hao.

#NidhamuUadilifuKujituma
#AfyaUtajiriHekima
#KaziUpendoHuduma
#UpekeeUdadisiUbunifu