#SheriaYaLeo (60/366); Tumia njia ya kujaribu na kushindwa.

Katika safari yako ya kujifunza ili kufikia ubobezi, usianze na ujuzi mmoja na kukomaa nao huo mapema.
Badala yake jifunze ujuzi mwingi unaoendana na kile unachotaka kubobea.

Kadiri unavyojikusanyia ujuzi mwingi, ndivyo unakuwa na uwanja mpana wa kufanya mengi na makubwa zaidi.
Kwa sababu ni vigumu kuweza kupata mtu mwenye ujuzi wa aina nyingi ambaye unajifunza kwake, unapaswa kujifunza wewe mwenyewe.

Na njia ya kujifunza mwenyewe ni ya kujaribu na kushindwa.
Kwa kila unachokutana nacho ambacho kinaendana na eneo unalotaka kubobea, jifunze kwa kujaribu njia mbalimbali.
Utashindwa kwenye njia hizo, lakini utajifunza njia zipi hazifanyi kazi ili uweze kutumia njia sahihi.

Kwa kwenda kwa njia hii, utajifunza ujuzi mwingi ambao ukiuleta pamoja utakuwezesha kufikia ubobezi wa juu kabisa.
Hapa tambua kwamba huzururi kwenye mambo mengi kwa sababu umeshindwa kuchagua na kukomaa na kitu kimoja.
Bali unakuza wigo wako wa ujuzi kwenye kile ulichochagua ili usijifungie kwenye njia moja pekee.

Sheria ya leo; Kwenye zama hizi za maendeleo makubwa ya sayansi na teknolojia, ambapo mabadiliko yanatokea kwa kasi, kuchagua ujuzi mmoja na kukomaa nao mapema kutakuwa kikwazo kwako baadaye. Badala yake jijengee ujuzi wa aina nyingi kwenye like eneo ulilochagua ili uwe na wigo mpana wa kuweza kufanya makubwa zaidi.

#NidhamuUadilifuKujituma
#AfyaUtajiriHekima
#KaziUpendoHuduma
#UpekeeUdadisiUbunifu