#SheriaYaLeo (347/366); Maisha na kifo.
Tunaweza kuelezea tofauti kati ya maisha na kifo kwa namna ifuatayo;
Kifo ni utulivu kamili, bila ya mwendo au mabadiliko, isipokuwa kuharibika.
Kwenye kifo tunatenganishwa na wengine na kuwa wapweke.
Kwa upande mwingine, maisha ni mwendo, muunganiko na viumbe wengine na utofauti wa maisha.
Kwa kukataa na kukandamiza mawazo ya kifo, tunachochea wasiwasi wetu na kufikiria zaidi kuhusu kifo.
Kujaribu kukikimbia kifo kunafanya tukifikirie zaidi kifo na kuathiri ubora wa maisha yetu.
Lakini kwa kukikubali na kukipokea kifo, unayathamini maisha na kuishi kwa ukamilifu.
Sheria ya leo; Kwa kuungana na uhalisia wa kifo, unakuwa umeungana na maisha kwa ujumla wake. Kwa kutenganisha kifo na maisha inatuzuia kuyaishi maisha kwa ukamilifu.
#NidhamuUandilifuKujituma
#AfyaUtajiriHekima
#KaziUpendoHuduma
#UpekeeUdadisiUbunifu
#UshirikianoUtegemeanoUwajibikaji