#SheriaYaLeo (348/366); Jinsi ya kuiangalia dunia.
Watu wengi huwa wanaiangalia dunia kwa mazoea.
Wanatumia yale waliyoyazoea kutafsiri yanayotokea na kufanya maamuzi.
Wanapenda uhakika wa mazoea, hata kama hayaleti matokeo yaliyo bora.
Wewe hupaswi kuwa hivyo, badala yake unapaswa kuiangalia dunia kama mchunguzi.
Unapaswa kuiangalia dunia ukiwa tayari kujifunza na kujaribu vitu vipya.
Unapaswa kuweka mazoea yako pembeni na kuwa na udadisi kama wa mtoto.
Ni kupitia udadisi na utayari wa kujifunza mambo mapya ndiyo utaweza kuona mengi mazuri yaliyopo duniani.
Ndiyo utaweza kuona uwezekano wa chochote unachokitaka kwenye maisha yako.
Unapoiangalia dunia kama mchunguzi, ukiwa tayari kujifunza na kujaribu vitu vipya unaondoa ukomo wowote unaokuwa umejiwekea.
Ni kwa njia hiyo ndiyo unaweza kufanya makubwa kwenye maisha yako.
Sheria ya leo; Kwa kufungua akili yako kwa namna hiyo, utaweza kufikia uwezo mkubwa wa kibunifu ulio ndani yako na kuweza kufanya makubwa.
#NidhamuUandilifuKujituma
#AfyaUtajiriHekima
#KaziUpendoHuduma
#UpekeeUdadisiUbunifu
#UshirikianoUtegemeanoUwajibikaji