3057; Kwa nini nataka uuze.
Rafiki yangu mpendwa,
Kama ambavyo nimeshakuandikia mara kwa mara, una malengo makubwa matatu kwenye biashara yako.
Malengo hayo ni kujenga mfumo wa kuiendesha biashara, kujenga timu imara na kujenga wateja waaminifu.
Ili uweze kutekeleza malengo hayo, kuna majukumu makuu mawili ambayo unapaswa kuyatekeleza. Na majukumu hayo yanakutaka uvae kofia kuu mbili.
Ya kwanza ni uwe meneja mzuri wa biashara yako ili uweze kujenga mfumo na timu. Na ya pili ni uwe muuzaji namba moja kwenye biashara yako ili utengeneze wateja waaminifu watakaokaa kwenye biashara yako kwa muda mrefu.
Kwenye ukurasa huu tunaenda kuangalia zaidi eneo la mauzo.
Ninataka sana wewe uwe muuzaji kwa sababu ndiyo eneo ambalo lina njia ya wazi ya kukuza biashara na kufikia lengo la ubilionea.
Mauzo ni mchezo wa namba na ukishazielewa namba zako na kuzifanyia kazi vizuri, unaweza kuyatabiri matokeo kabisa.
Kama ukiweza kutengeneza wateja 100 wapya kila mwezi na kila mteja akawa ananunua kwa angalau Tsh laki 1 kila mwezi, kwa miaka mitano utakuwa na wateja wasiopungua 5000 na mauzo yasiyopungua Tsh milioni 500 kwa mwezi au Tsh bilioni 5 kwa mwaka.
Huu ni mfano rahisi wa idadi ya wateja 100, ambayo kila mtu anayejitoa kweli anaweza na mauzo ya Tsh laki 1 kila mwezi, ambapo mtu akiweka juhudi kuwafikia wateja sahihi anaweza pia.
Hizo ni namba ambazo zinawezekana hata kwa mtu mmoja tu akiwa amejitoa kweli kweli kujenga biashara kupitia kujenga mauzo.
Sasa namba hizo zinaweza kuwa kubwa zaidi kama kukiwa na timu kubwa ya mauzo.
Na ili kufikia namba hizo na kuendelea kukua zaidi, kuna vitu viwili vikubwa vinatakiwa kufanyika.
Cha kwanza ni kujenga timu imara ambayo itaweza kuendelea kuwafikia wateja wengi zaidi na kufanya mauzo makubwa zaidi kwa wateja hao.
Ujengaji wa timu imara unakutaka wewe kuwa mfano bora kwenye mauzo na kuwa meneja mzuri pia.
Kitu cha pili ni uweze kutoa bidhaa na huduma bora kabisa kiasi cha wateja kutokukuacha na kwenda kwingine.
Ukishampata mteja na akanunua kwa mara ya kwanza, anatakiwa kuendelea kununua kwako kwa kipindi chote cha maisha yake.
Kama umeweza kumuuzia kwa mara ya kwanza, utaweza pia kuendelea kumuuzia kama mambo yote yatafanyika kwa usahihi.
Namba tulizoona hapa siyo mwisho, ni mwanzo tu na kuna fursa kubwa sana ya ukuaji ukishaweza kufikia namba za aina hiyo.
Lakini yote hayo yanakutaka sana wewe uwe muuzaji bora na meneja mzuri.
Unahitaji kuwa mfano bora sana kwa watu wote unaowaajiri na kuwaweka kwenye mauzo.
Unaweza kuona wewe hulazimiki kuuza kama tayari umeshaajiri watu wa mauzo.
Lakini kumbuka hakuna mtu anayeweza kuyabeba maono makubwa ya kibiashara uliyonayo.
Na hakuna mtu anayeweza kujisukuma kuliko unavyojisukuma wewe.
Watu hata wawe sahihi kiasi gani, huwa wanaathiriwa sana na mazingira yanayowazunguka.
Kwa kuwa muuzaji bora na meneja mzuri, utaweza kujenga utamaduni bora kwenye biashara yako na kuigeuza kuwa mashine ya mauzo.
Biashara ikishakuwa mashine ya mauzo, yaani inazalisha matokeo ya uhakika kupitia timu inayokuwepo, hakuna kinachoweza kuizuia biashara hiyo kukua.
Uza na simamia vizuri, kuna hazina kubwa sana ipo ndani ya biashara yako.
Lakini hazina hiyo inataka kazi kubwa ifanyike ili kuiibua.
Kazi hiyo ndiyo wajibu wako namba moja kwenye biashara yako.
#NidhamuUadilifuKujituma
#AfyaUtajiriHekima
#KaziUpendoHuduma
#UpekeeUdadisiUbunifu
#UshirikianoUtegemeanoUwajibikaji
#BilioneaMafunzoni
#NajengaBiashara
#HakunaKingineMuhimu
#LazimaNitoboe
#NawekaKaziNifanikiwe
Asante nitafanyia kazi ya kuwa meneja mzuri na na muuzaji bora kuwahi kutokea, kwani nilikuwa najitofautisha na majukumu hayo hasa kwenye upande wa mauzo nilijitoa kabisa.
LikeLike
Ni muhimu kuwa mstari wa mbele ili kuhakikisha timu inaiga kwa kufanya kwa viwango vya juu kabisa.
LikeLike
Hazina hiyo inataka kazi kubwa ifanyike ili kuiibua.
LikeLike
Siyo kazi ndogo.
LikeLike
Asante Kocha, nitajenga timu na kutoa au kuuza bidhaa bora sana. Lakini pia nitakuwa muuzaji mkuu na msimamizi wa timu yangu.
LikeLike
Kila la kheri.
LikeLike
Asante sana, kwakuwa meneja mzuri, nitakuwa mfano kwa timu yangu, mauzo ndiyo Kila kitu kwenye biashara.
LikeLike
Vizuri sana.
LikeLike
Jukumu kubwa nilililonalo kwenye biashara yangu ni kuwa meneja mzuri na kuwa muuzaji bora kuwahi kutokea huu ni utamaduni ninaoujenga kwenye biashara yangu il kila anakuja kwenye biashara kama msaidizi aweze kuuishi utamaduni huu.
Asante kocha
LikeLike
Tuwe mfano mzuri.
LikeLike
hakuna mwenye maono makubwa ya ukuaji wa biashara yako kama wewe meneja wa hiyo biashara.
kuwa meneja mzuri ongoza timu wape maono wateke.
LikeLike
Kabisa.
LikeLike
Asante sna kocha. Lengo ni wateja 100 kila mwezi. Asante sana
LikeLike
Na linawezekana kabisa, kinachohitajika ni kazi kubwa.
LikeLike
Nakwenda kuwa muuzaji bora na meneja mzuri kwa kutumia muda wangu kwenye kujenga biashara, Kujenga timu na kukuza mauzo.
LikeLike
Kila la kheri.
LikeLike
Naenda kuwa meneja mzuri kwenye biashara yangu kwa kujenga timu na mfumo mzuri.
LikeLike
Kila la kheri.
LikeLike
Watu hata wawe sahihi kiasi gani, huwa wanaathiriwa sana na mazingira yanayowazunguka.
Kwa kuwa muuzaji bora na meneja mzuri, utaweza kujenga utamaduni bora kwenye biashara yako na kuigeuza kuwa mashine ya mauzo
Asante sana
LikeLike
Karibu.
LikeLike
Ahsante sana Kocha Dr M. Amani napambana kila siku na nitahakikisha nakuwa muuzaji Bora kuliko chochote kwenye biashara yangu maana Mimi ndo mwenye maono makubwa.
🔥✅🤝
LikeLike
Kila la kheri.
LikeLike
Nitakuwa meneja mkuu na muuzaji bora kuwahi kutokea kwenye biashara yangu.
Asante sana Kocha Dr Makirita Amani
LikeLike
Kila la kheri.
LikeLike
Nitakuwa Meneja mzuri wa Mauzo kwa wakati eote ili team yangu iwe bora zaidi ..
LikeLike
Kila la kheri.
LikeLike
Asante sana Kocha, nitakua Meneja Bora na mfano mzuri kwa timu yangu.
LikeLike
Kila la kheri.
LikeLike
Nitauza na kufuatilia wateja ili kuibua hazina kubwa iliyoko kwenye biashara yangu.
LikeLike
Kila la kheri.
LikeLike
Natakiwa kuuza na kusimamia vizuri biashara yangu. Kazi hiyo ndiyo wajibu wangu namba moja kwenye biashara yangu.
LikeLike
Hakika
LikeLike
Mauzo Ni mchezo wa namba.
Ni kuwa na timu imara na kuuza bidhaa bora kabisa.
LikeLike
Hakika
LikeLike
KUWA MUUZAJI BORA NA MENEJA MZURI KUJENGA TIMU YA IMARA
ASANTE KOCHA.
LikeLike
Karibu.
LikeLike
Kuwa Muuzaj bora kuwahi kutokea ndio jukumu langu kuu na kuhakikisha napandisha mauzo
LikeLike
Safi sana.
LikeLike
Natakiwa niwe meneja mzuri wa biashara yangu.
Na natakiwa niwe muuzaji namba moja kwenye biashara yangu.
LikeLike
Hakika.
LikeLike
Asante sana kocha nitalifanyia kazi kwa kuwa wa kwanza kufanya vyovyote kwenye biashara yangu nitakuwa mfano muzuri kwenye biashara yangu nitakuwa meneja muzuri na pia kuwa Muuzaji bora kuwahi kutokea
LikeLike
Kila la kheri.
LikeLike
Naendelea kujijenga kuwa meneja mzuri na muuzaji bora kabisa wa biashara yangu.
LikeLike
Vizuri sana.
LikeLike
Mimi ni meneja na Muuzaji bora kuwahi kutokea!
LikeLike
Vizuri sana.
LikeLike
Ili kuwa Meneja bora ni muhimu kuendelea kuuza kila mara ili kuwa mfano kwa timu kuchukua hatua kila mara
LikeLike
Kila la kheri.
LikeLike
Hakika ni Muhimu na Lazima kuwa msimamo na msitari wa Mbele zaidi katika Mauzo ili kupata Matokeo makubwa
LikeLike
Hakika
LikeLike
kuuza na kusimamia vizuri tutaiyona hazina iliyomo ndani yake
LikeLike
Vizuri.
LikeLike