3078; Maji yanayoizamisha meli.
Rafiki yangu mpendwa,
Sote tunajua ya kwamba meli huwa inaelea kwenye maji.
Pamoja na uzito wake mkubwa, meli hiyo huwa inaendelea kuelea vizuri tu.
Lakini hiyo yote ni kama maji yataendelea kubaki nje ya meli.
Ni pale maji yanapoingia ndani ya meli ndiyo meli inapoanza kuzama.
Kumbe basi, maji yanayoizamisha meli ni yale yanayoingia ndani ya meli na siyo yanayobaki nje ya meli.
Na hata kwa kiwango, maji yanayoingia ndani ya meli na kuizamisha, siyo mengi kama yale yanayobaki nje.
Hivyo kiasi kidogo cha maji yanayoingia ndani ya meli huwa yana madhara makubwa sana.
Tunajifunza nini hapo?
Somo kubwa la kutoka nalo hapo ni chanzo cha wengi kushindwa kwenye maisha kinakuwa ndani ya mtu kuliko nje yake.
Kwa nje mtu anaweza kuzungukwa na vitu vingi vinavyochochea ashindwe, lakini havitakuwa na nguvu mpaka pale vinapoingia ndani.
Ni vitu vinavyoingia ndani ya watu ndiyo vinawafanya washindwe kwenye maisha.
Kuna mazingira mengi hasi ambayo mtu unakutana nayo kwenye maisha.
Lakini mazingira hayo hayawezi kuwa na madhara kwa mtu kama hajaruhusu mambo hayo hasi kuingia ndani yake.
Ni pale mtu anapoingiza fikra hasi kwenye akili yake ndiyo anapoanza kushindwa.
Kadhalika kwenye biashara, kuna changamoto nyingi sana ambazo huwa zinaathiri biashara, lakini changamoto hizo huwa hazina nguvu kama ni za nje ya biashara.
Changamoto zenye nguvu na madhara makubwa ni zile zinazoanzia au zinazoingia ndani ya biashara.
Biashara huwa inaanza kwa kushindwa ndani kwanza ndiyo baadaye kushindwa kunaoneoana dhahiri nje.
Watu wamekuwa wakiona ushindani mkali unaua biashara, lakini hilo ni kwa baadaye sana.
Biashara inafanywa kuwa dhaifu na mambo yanayokuwa yanaendelea ndani yake kiasi cha kupelekea ishindwe kuhimili mikiki mikiki ya nje.
Hivyo pia ndivyo ilivyo kwa mahusiano yanayovunjika.
Wengi hukimbilia kulaumu sababu za nje au upande mmoja kwenye mahusiano hayo.
Lakini ukweli ni kwamba kuna sababu za ndani ambazo zimefanya mahusiano hayo kuwa dhaifu kiasi cha kushindwa kuhimili mikiki mikiki ya nje.
Maisha hayawezi kukosa changamoto kabisa.
Kwa hakika changamoto ndiyo zinafanya maisha yawe na maana.
Kama ambavyo maji ndiyo yanafanya meli iendelee.
Changamoto zenye nguvu ya kuleta madhara kwenye maisha ya mtu ni zile ambazo zinaanzia au zinaingia ndani ya watu.
Changamoto zozote zile zilikabiliwa vizuri kwa nje, huku ndani mtu akibaki na utulivu mkubwa, ataweza kuzivuka na kuwa imara zaidi.
Kwenye maeneo yote ambayo unakwama kwenye maisha yako, jiulize ni vitu gani vya ndani yako mwenyewe vinakukwamisha kwenye maeneo hayo.
Wakati wengine wanakimbilia kulaumu mambo ya nje, wewe chimba ndani yako kupata majibu sahihi.
Tuchukue mfano wa biashara zinazoshindwa.
Huwa ni rahisi sana watu kulaumu mambo ya nje kama ushindani, uchumi mbaya, sera mbovu za serikali, wateja wagumu n.k.
Lakini hutasikia watu wakilaumu mambo ya ndani kama kukosekana kwa mfumo mzuri, kukosekana kwa timu imara na kutokuwepo kwa mchakato sahihi wa mauzo. Usimamizi wa fedha na watu kuwa mdogo pia huwa hautajwi.
Kwa mambo yote ambayo tunakwama au kukutana na ugumu, tukianza kwa kuchimba ndani yetu, tutaweza kuzuia ya ndani yasipelekee kushindwa kabisa.
Hivyo basi, kwa magumu na changamoto zozote unazopitia kwenye maisha yako, kabla hujakimbilia mambo ya nje, anza kwanza na ya ndani.
Ukiweza kuyatatua vizuri ya ndani, ya nje yanakosa nguvu ya kuleta madhara makubwa.
#NidhamuUadilifuKujituma
#AfyaUtajiriHekima
#KaziUpendoHuduma
#UpekeeUdadisiUbunifu
#UshirikianoUtegemeanoUwajibikaji
#BilioneaMafunzoni
#NajengaBiashara
#HakunaKingineMuhimu
#LazimaNitoboe
#NawekaKaziNifanikiwe
Sababu za ndani ndiyo zinaleta madhara kwa mtu. Kabla ya kuangalia sababu za nje, angalia KWANZA sababu za ndani.
Asante sana Kocha Dr Makirita Amani
LikeLike
Ukiweza kuvuka ndani, nje ni rahisi zaidi.
LikeLike
Maji yanayoizamisha meli ni yale yanayoingia ndani, sio ya nje.
LikeLike
Kabisa.
LikeLike
Hakika ni sahihi sana
LikeLike
Vizuri.
LikeLike
Napaswa kuchimba ndani ya baishara yangu na maisha yangu ili kuona ni yapi ninayosababisha mwenyewe na kusababisha biashara kutokufanya vizuri au maisha yangu kutokwenda vizuri kabla sijaanza kufikiria mambo ya nje na kuyalaumu hayo,nikishaweza kurekebisha yale ninayosababisha mwenyewe na kukwama hakika mambo ya nje hayatanikwamisha kamwe.
Asante sana kocha kwa kunikumbusha hili.
LikeLike
Tatua ya ndani ba ya nje yatakaa sawa.
LikeLike
Ahsante sana kocha, nitajichimba ndani yangu zaidi na siyo kuangalia sababu za nje
LikeLike
Vizuri
LikeLike
Nashukuru Kocha kwa makala hii imenisaidia kutafakari zaidi changamoto ninazopitia na kupata mtazamo chanya kwenye haya yote. Hakika maji yaliyo nje japokuwa ni mengi sana hayawezi kuzamisha meli yangu ya mafanikio
LikeLike
Vizuri na kila la kheri.
LikeLike
Kweli Kila kitu kiwe kizuri au kibaya kinaanzia ndani yetu. Matokeo ya kushindwa Kwa nje ni picha tuu mchakato mzima ulikuwa ndani.
LikeLike
Kabisa.
LikeLike
Kwenye magumu au changamoto yoyote ninayopitia kabla sijaanza kukimbilia mambo ya nje nitaanza na ya ndani kwanza.
LikeLike
Vizuri
LikeLike
Asante kocha,Changamoto zote zinazojitokeza kwenye maisha yangu na biashara kwa ujumla ni lazima nijitathimini kwanza kabla ya kulaumu na kutafuta sababu kutoka nje.
LikeLike
Vizuri.
LikeLike
Changamoto zenye nguvu ya kuleta madhara kwenye maisha ya mtu ni zile ambazo zinaanzia au zinaingia ndani ya mtu mwenyewe.
LikeLike
Kabisa
LikeLike
Ahsante sana kocha kwa makala nzuri
Nitaweka nguvu kuangalia ndani kabla ya kulalamikia matokeo nayopata.
LikeLike
Vizuri
LikeLike
Hakika ni kweli kabisa kocha kuwa ndani ya mtu, biashara ama familia pakishakuwa imara changamoto zozote za nje haziwezi kufanya chochote. Asante sana kwa somo hili.
LikeLike
Karibu
LikeLike
Wakati wengine wanakimbilia kulaumu mambo ya nje, wewe chimba ndani yako kupata majibu sahihi.
Asante Kocha.
LikeLike
Kabisa.
LikeLike
Sababu za ndani ndiyo zinaleta maradha makubwa kuliko za nje
LikeLike
Hakika.
LikeLike
Mambo ya ndani yanaua zaidi biashara kuliko mambo ya nje.
LikeLike
Kabisa.
LikeLike
Ni pale mtu anapoingiza fikra hasi kwenye akili yake ndipo anapoanza kushindwa
Asante sana
LikeLike
Hilo lipo wazi.
LikeLike
Mambo ya ndani tuyatatue kwanza ya nje hayana nguvu hata kwenye ndoa tukishindwa kuelewana sisi wawili hata ije boma nzima haitaweza na tukipatana sisi wawili hata waje wote hawawezi kutubadilisha na kwenye biashara swala la msingi tuweke mambo yetu ya ndani vizuri na ya nje hayawezi kutusumbua yatatatuka tu
LikeLike
Umetoa mfano mzuri sana hapo kwenye ndoa,
Tukae humo katika mambo yote.
LikeLike
Sintaruhusu Mambo ya nje yaigie ndani na kuvuruga m chakato . Asante kocha
LikeLike
Vizuri
LikeLike
Nikweli kinachoingia ndani ndio chenye madhara
LikeLike
Hakika
LikeLike
Ndani sio nje.Ni kweli tukiweza kuyakabili vizuri ya ndani ya nje hayana madhara.
LikeLike
Hakika
LikeLike
Asante sana kocha kwa somo zuri la utambuzi/kujitambua, muhimu ni kujitafuta mwenyewe,maana kinachoua hakitoki nje,kipo ndani yako,yangu hakika maji yanayozamisha meli siyo yaliyoko nje bali yanayoingia ndani.”funzo kubwa Sana”
LikeLike
Karibu
LikeLike
Kweli kabisa. Changamoto binafsi na sababu za ndani ndiyo hatari zaidi kuliko za nje.
LikeLike
Kabisa
LikeLike
Maji yanayozamisha meli ni yale yanayoingia ndani yake na sio yale yanayoizunguka.
Changamoto zenye nguvu na madhala makubwa ni zile zinazoanzia au zinazoingia ndani ya biashara.
Ni vizuri kuanza kutatua changamoto zinazoingia au kuanzia ndani yetu kabla hatujarusha lawama kwenye changamoto za nje.
LikeLike
Kabisa
LikeLike
Naaamini
LikeLike
Vizuri
LikeLike
Kwa mambo yote ambayo tunakwama au kukutana na ugumu, tukianza kwa kuchimba ndani yetu, tutaweza kuzuia ya ndani yasipelekee kushindwa kabisa.
Hivyo basi, kwa magumu na changamoto zozote unazopitia kwenye maisha yako, kabla hujakimbilia mambo ya nje, anza kwanza na ya ndani.
Ukiweza kuyatatua vizuri ya ndani, ya nje yanakosa nguvu ya kuleta madhara makubwa.
LikeLike
Hakika
LikeLike