3096; Mwanzo wa anguko.
Rafiki yangu mpendwa,
Watu wengi huwa wanadhani anguko la mtu kwenye maisha linaanzia kwenye kushindwa.
Lakini huo siyo ukweli.
Anguko huwa linaanzia kwenye mafanikio na siyo kwenye kushindwa.
Huwa kuna usemi kwamba kushindwa ni mwalimu mzuri sana wa mafanikio na kushinda huwa kunazalisha uzembe.
Ni pale mtu anaposhindwa ndiyo anapata msukumo wa kujifunza na kuchukua hatua za tofauti ili kupata ushindi.
Lakini mtu anaposhinda, huwa anajiona tayari anajua kila kitu na hahitaji kujifunza tena wala kuchukua hatua za tofauti.
Baada ya ushindi, watu wengi huridhika na kuenda kwa mazoea.
Ile kiu kubwa ya mafanikio ndani yao inapoa.
Wanalegeza mkazo waliokuwa wameuweka na ukawafikisha pale walipofika.
Nidhamu kali ya kazi waliyokuwa nayo wanaiweka pembeni na kwenda kama wengine.
Matokeo yake wanakaribisha anguko ambalo linawatoa pale walipokuwa wameshafika.
Kuondokana na hali hiyo, baki na njaa na kiu ya mafanikio mara zote, bila ya kujali ni matokeo gani umeyapata.
Unapopata ushindi, usiridhike na kuona umeshamaliza kila kitu.
Badala yake weka malengo mengine makubwa zaidi ya yale ambayo tayari umeshayafikia.
Kila wakati kwenye maisha yako unapaswa kuwa na kitu kikubwa unachokipambania, bila kujali umeshafanya makubwa kiasi gani.
Ushindi uliopata jana, leo hauhesabiki. Ushindi mkubwa zaidi unaoutaka kesho ndiyo unatakiwa kukunyima usingizi leo.
Hatari nyingine ya ushindi kwenye anguko inasababishwa na watu wanaokuzunguka.
Kama wanakuwa hawana mafanikio makubwa, wanatumia mafanikio unayokuwa umeyapata kukulazimisha uridhike.
Wanapokuona unaendelea kujisukuma licha ya ushindi ambao tayari umeshaupata, wanakuambia unapaswa kuridhika na ulichopata, kwa sababu ni kikubwa sana.
Na kweli ukiwaangalia wao na ukajilinganisha na wewe, unajiona umeshafika mbali na hivyo unaweza kupunguza juhudi unazoweka.
Hiyo ni hatari kubwa sana, ambayo ni vigumu kuivuka, kwa sababu wale wanaokuzunguka wana nguvu kubwa ya ushawishi kwako.
Ndiyo maana ni muhimu sana muda wote uzungukwe na watu waliofanikiwa kuliko wewe au ambao muda wote wanapambana kupata mafanikio makubwa kuliko yale ambayo tayari wameshayapata.
Watu wa aina hiyo watakupa moyo na msukumo wa kuendelea kuweka juhudi kubwa na kutokuridhika na ushindi unaokuwa umeshaupata.
Kama upo hai, muda wote unatakiwa kuwa na malengo makubwa unayoyafanyia kazi.
Malengo makubwa ambayo hujawahi kuyafikia na yanakupa msukumo wa kujituma zaidi.
Hupaswi kuwa kwenye hali ya kuridhika wakati wowote ule.
Pale tu unapoanza kuridhika ndipo anguko linapoanzia.
Wengi wanapokuwa wanaanzia chini, huwa wanaweka lengo ambalo ni kubwa na kuona wakishalifikia basi wamemaliza kila kitu.
Lengo hilo linawasukuma wajitume kwa kupitiliza.
Wakiamini ni zoezi la muda mfupi, kwani wakishafikia lengo watapumzika.
Ni pale wanapofikia lengo ndiyo wanaona kuna malengo mengine makubwa zaidi ya kufikia.
Hilo linawataka waweke malengo mengine makubwa zaidi na juhudi waongeze zaidi.
Kwa kifupi, maisha ya mafanikio hayana mapumziko.
Kujiambia ukifikia malengo uliyojiwekea utapumzika, ni kukaribisha anguko baada ya kuwa umepiga hatua.
Ukishafikia malengo uliyokuwa umejiwekea, unatakiwa kuweka malengo mengine makubwa zaidi.
Unaweza kuwa unajiuliza vipi hali ya uchoshi (burnout) inayoletwa na kuweka juhudi kwa muda mrefu bila kupumzika?
Jibu ni hali hiyo ya uchoshi huwa inaletwa na juhudi zisizokuwa na kusudi.
Kwa mfano nikikuambia ubebe mfumo wa sementi wenye kilo 50 na ukimbie nao, utalalamika ni mzito sana.
Lakini ikitokea mtu wako wa karibu, mwenye kilo zaidi ya 50, ameumwa na kuanguka ghafla, utaweza kumbeba na kumkimbiza eneo sahihi bila ya kuchoka.
Hivyo uchoshi hautokani na kila unachofanya, bali unatokana na sababu ya kufanya.
Kama huna sababu ya msingi ya kufanya, uchoshi unakuwa mkubwa.
Lakini unapokuwa na kwa nini kubwa ya kufanya kitu, uchoshi haupati nafasi.
Hivyo basi, tunajifunza umuhimu wa kuwa na kwa nini kubwa kwenye mafanikio makubwa tunayotaka kuyafikia.
Ikiwa tunachotaka ni fedha pekee, tukishazipata tutaridhika haraka na kuacha kuweka juhudi.
Ila tunapokuwa na kusudi kubwa zaidi ya fedha, tunapata nguvu ya kuendelea kujisukuma zaidi bila ya kuridhika wala kuchoka.
Haijalishi umefika wapi na kupata nini, kama bado upo hai, unapaswa kuendelea kujisukuma zaidi.
Kamwe usiridhike na kuzoea popote ulipofika, panga kwenda mbali zaidi ya popote unapokuwa umefika.
Hali hiyo ndiyo itakupa mafanikio makubwa na kukuacha kwenye kilele cha mafanikio.
#NidhamuUadilifuKujituma
#AfyaUtajiriHekima
#KaziUpendoHuduma
#UpekeeUdadisiUbunifu
#UshirikianoUtegemeanoUwajibikaji
#BilioneaMafunzoni
#NajengaBiashara
#HakunaKingineMuhimu
#LazimaNitoboe
#NawekaKaziNifanikiwe
Kamwe usiridhike na kuzoea popote ulipofika, panga kwenda mbali zaidi ya popote unapokuwa umefika.
LikeLike
Hakika
LikeLike
Kabisa kocha mafanikio mengi ndiyo anguko la wengi.
Huwezi kuanguka kama hauko juu.
LikeLike
Kabisa
LikeLike
Kama upo hai, muda wote unatakiwa kuwa na malengo makubwa unayoyafanyia kazi.
Malengo makubwa ambayo hujawahi kuyafikia na yanakupa msukumo wa kujituma zaidi.
Hupaswi kuwa kwenye hali ya kuridhika wakati wowote ule.
Pale tu unapoanza kuridhika ndipo anguko linapoanzia.
Asante sana Kocha Dr. Makirita Amani
LikeLike
Kabisa
LikeLike
Uwe na lengo kubwa na ukifikia uende kwenye lengo la juu na ukifikia uongeze kutokua na lengo inaleta uchoshi lakini ukijua unaenda aapi uchoshi haupo
Kuridhika na ulichopata baada ya kufika hapo ulipo ni mwanzo wa anguko
LikeLike
Malengo yaendelee kukua.
LikeLike
Sipaswi kiridhika na mafanikio kidogo ninayopata bali napaswa kuendelea kupambana mana mafanikio hayana kupumzika,pale nitakapojaribu kumpumzika kw amafanikio ninayokua nimeyapata ndipo hapo lilipoa anguko langu,safari ya mafanikio ni safari endelevu.
Asante kocha.
LikeLike
Vizuri
LikeLike
Kama upo hai mara zote kuwa na malengo makubwa unayofanyia kazi.
LikeLike
Hakika
LikeLike
Asante Kocha,
Maisha ya mafanikio hayana mapumziko. Nitabaki na njaa na kiu ya mafanikio mara zote bila kujali ni matokeo gani nimeyapata.
LikeLike
Vizuri
LikeLike
Maisha ya mafanikio hayana mapumziko, kwani ukipumzika ni lazima uanguke. Kuanzia sasa nimeondoa kabisa dhana ya mapumziko. Asante sana kocha
LikeLike
Hakika
LikeLike
”KWA KILA MAFANIKIO NINAYOYAFIKIA NATAKIWA KUKUA ZAIDI,KWA KUJIWEKEA MALENGO MAKUBWA. HAKUNA KUPUMZIKA”
Natakiwa nibaki na njaa na kiu ya mafanikio mara zote. Asante sana.
LikeLike
Hakika
LikeLike
Ushindi wa jana leo hauhesabiki, unatakiwa utupe hamasa ya kuendelea kushinda na si vinginevyo
LikeLike
Hakika
LikeLike
Mafanikio ndio kila kitu
LikeLike
Ndiyo
LikeLike
Kila wakati kwenye maisha yako unapaswa kuwa na kitu kikubwa unachokipambania, bila kujali umeshafanya makubwa kiasi gani.
Asante sana
LikeLike
Hakika
LikeLike
Mwanzo wa anguko ni mafanikio makubwa ambayo mtu anakuwa ameyafikia.
Usiuhesabu ushindi ulioupata jana leo, bali kila wakati weka malengo mengine makubwa zaidi.
Kila wakati kwenye maisha yako unapaswa kuwa na kitu kikubwa unachokipambania, bila kujali umeshafanya makubwa kiasi gani.
Ukweli ni kwamba, Maisha ya mafanikio huwa hayana mapumziko, Ukishafikia malengo uliyokuwa umejiwekea unatakiwa kuweka malengo mengine makubwa zaidi.
LikeLike
Ukipumzika tu, umepotea.
LikeLike
Kushindwa ni mwalim mzuri Sana kwenye mafanikio na kushindwa ktk Maisha. Pale mtu anaposhindwa ndipo anapata msukumo wa kujifunza na kuchukua hatua
za tofauti ili kupata ushindi.
Shuklani kocha.
LikeLike
Vizuri
LikeLike
Asante kocha,Sipaswi kuridhika na hatua nilionayo ila inabidi nijisukume mbele zaidi ili kupata mafanikio.
LikeLike
Hakika
LikeLike
Asante kocha,Inabidi kujisukuma mbele zaidi ili nifanikiwe sio kuridhika na hatua niliyonayo kwa sasa.
LikeLike
Vizuri
LikeLike
Anguko huja pale mtu anaporidhika baada ya kufikia lengo flani na kujiona amemaliza na anajua kila kitu kuhusu kitu hicho. Mimi nitakupa malengo makubwa kila nitakapofikia lengo la kawaida la mafanikio flani ili kuendelea kuwa na shauku, hamasa na kiu ya kusonga mbele
LikeLike
Vizuri sana.
LikeLike
Sitaridhika na mafanikio madogo ninayopata kwani ndiyo chanzo cha Anguko.
LikeLike
Vizuri
LikeLike
Siku zote natakiwa kuwa kwenye haratakati za kutafuta maisha.
LikeLike
Vizuri
LikeLike
Jitahidi uzungukwe na watu waliofanikiwa kuliko wewe.
LikeLike
Kabisa
LikeLike
Haijalishi umefika wapi na kupata nini, kama bado upo hai, unapaswa kuendelea kujisukuma zaidi.
LikeLike
Kabisa.
LikeLike
Hakuna kuridhika, as long as nipo hai nitaweka lengo kubwa zaidi
LikeLike
Vizuri
LikeLike
Kwenye maisha hakuna kuridhika kila mara ni kujisukuma kusonga mbele mpaka mwisho wa uhai
LikeLike
Kweli
LikeLike
Pale Tu unapoanza kiridhika ndipo anguko linapoanzia
LikeLike
Haraka sana.
LikeLike