3123; Chini ya kumi ni sifuri.
Rafiki yangu mpendwa,
Maisha yetu hapa duniani huwa yanaendeshwa kwa kanuni nyingi sana za asili.
Ni kwa kufuata kanuni hizo ndiyo tunapata yale tunayoyataka kwenye maisha yetu.
Moja ya kanuni muhimu sana kwenye safari ya mafanikio ni kanuni ya wastani.
Kanuni hiyo inaeleza kwamba kuna wastani wa kila kitu kwenye maisha.
Ili uweze kupata chochote unachotaka, unapaswa kwanza kuijua kanuni hiyo ya wastani na kuitimiza ndiyo uweze kupata unachotaka.
Kwa urahisi, kanuni ya wastani inaeleza uwiano wa kumi kwa moja, kati ya juhudi zinazowekwa na matokeo yanayopatikana.
Kwa mfano, ili uweze kuuza kwa mteja mmoja, inabidi uwafikie wateja wasiopungua 10 wenye uhitaji wa kile unachouza.
Kwa kanuni hiyo ya wastani, matokeo yoyote unayotaka kupata, zidisha juhudi mara 10 kisha tekeleza juhudi hizo.
Wateja unaohitaji ili biashara yako ijiendeshe vizuri, zidisha mara 10 na hiyo inakuwa idadi ya unaopaswa kuwafikia.
Ili kupata faida unayotaka, unatakiwa uuze mara 10 yake.
Tukiendelea kuirahisisha kanuni hiyo ya wastani, tunaona namba ya chini kabisa inayoweza kuleta matokeo ni 10.
Chochote kinachofanyika chini ya 10 ni sawa na hakijafanyika kabisa.
Ni vigumu sana kupata matokeo yoyote unayoyataka kama juhudi unazoweka ni chini ya namba 10.
Na hapo ndipo ninaposema kufanya chini ya 10 ni sawa na sifuri, yaani hujafanya kabisa.
Fikiria kufanya kwa viwango vya makumi na siyo mamoja.
Pia fikiria kwa kuzidisha badala ya kujumlisha.
Hivyo ndivyo unavyopaswa kuziendea namba zako ili upate kile unachotaka.
Epuka sana kufanya chochote kile kwa viwango vidogo na kukata tamaa haraka pale matokeo yanapokuwa tofauti na mategemeo uliyokuwa nayo.
Jua unapofanya mara 10 ndiyo inahesabika kama mara 1, hivyo chini ya hapo ni sawa na haijafanyika kabisa.
Utakuwa mahali pazuri sana kama kila juhudi unazopaswa kuweka utazidisha mara kumi kisha kutekeleza kweli.
Ukiweza kwenda na mpango huo, hakuna chochote kitakachoweza kukushinda kwenye maisha yako.
Fanya kwa ukubwa, wingi na msimamo chochote ulichopanga kufanya na utaweza kuzalisha matokeo makubwa sana na yanayokupa mafanikio makubwa pia.
Mara zote kumbuka kanuni ya wastani ya moja kwa kumi na fanya mara kumi ili kupata matokeo unayoyataka.
#NidhamuUadilifuKujituma
#AfyaUtajiriHekima
#KaziUpendoHuduma
#UpekeeUdadisiUbunifu
#UshirikianoUtegemeanoUwajibikaji
#BilioneaMafunzoni
#NajengaBiashara
#HakunaKingineMuhimu
#LazimaNitoboe
#NawekaKaziNifanikiwe
Ni kweli ni sawa na haijafanyika tukienda na kanuni ya wasta kuwa wateja tarajiwa idadi tuliyyotaka kuwapata kwa kugeuza tuzidishe mara 10 nataka kupata wateja 200 inamaana tuzidishe mara 10ikiwa na maana tutembelee wateja 2000 hii kanuni ni nzuri sana
LikeLike
Hakika
LikeLike
Asante kocha hili nimekuwa nalitumia kwenye kusaka wateja na usambazaji yaani mauzo yanapimwa kwa de namba ya wateja ambao nimewatembelea
LikeLike
Vizuri sana.
LikeLike
Nitaendelea kupambana kukuza viwango vyangu vya usakaji Ili kupata wastani mzuri wa wateja.
LikeLike
Kila la kheri
LikeLike
Asante sana kocha kwa kanuni hii ya asili.
Mara zote nitajitahidi kumbuka kanuni ya wastani ya moja kwa kumi na kufanya mara kumi ili kupata matokeo ninayoyataka.
LikeLike
Vizuri sana.
LikeLike
Hii ni alarm muhimu ya kunisukuma kufanya Kwa viwango vya juu, chini ya kumi ni sifuri, hakuna kujitia moyo
Asante Kocha
LikeLike
Kila la kheri
LikeLike
Ni kweli Kocha, kama 10 ni moja na chini ya moja ni sifuri basi pia chini ya kumi ni sifuri.
LikeLike
Hesabu imebalansi.
LikeLike
Chochote kile mara 10.Chini ya hapo ni sawa na sijafanya.Asante kocha.
LikeLike
Ndiyo
LikeLike
Mara zone nitafanya kwa kuzidisha zaidi ya mara 10
LikeLike
Vizuri
LikeLike
Asante Kocha,
Nitaweka juhudi kwenye shughuli zangu kwa kuzidisha na siyo kwa kujumlisha.
LikeLike
Vizuri
LikeLike
Fanya kwa ukubwa wingi na msimamo chochote ulichopanga kufanya ili kupata mafanikio makubwa. Nitafanya kwa msimamo kwa kuifuata kanuni ya mara kumi 10x rule.
LikeLike
Vizuri
LikeLike
Mara zote kumbuka kanuni ya wastani ya moja kwa kumi na fanya mara kumi ili kupata matokeo unayoyataka.
Asante sana Kocha Dr Makirita Amani.
LikeLike
Vizuri
LikeLike
Kumbe Chini ya 10 ni kazi bure. Faida Mara 10, wateja zaidi ya mara10. 10..10…10…10..10
LikeLike
Mwendo wa 10.
LikeLike
Asante kocha,
Mara zote nitazingatia kanuni ya wastani ya moja kwa kumi na kufanya mara kumi ili kupata matokeo ninayoyataka
LikeLike
Kila la kheri
LikeLike
Asante kocha,Mara zote nitajitahidi kufanya kanuni ya wastani ya moja kwa kumi na kuzidisha zaidi ya mara kumi ili nipate matokeo.
LikeLike
Kila la kheri
LikeLike
Epuka sana kufanya chochote kile kwa viwango vidogo na kukata tamaa haraka pale matokeo yanapokuwa tofauti na mategemeo uliyokuwa nayo.
Jua unapofanya mara 10 ndiyo inahesabika kama mara 1, hivyo chini ya hapo ni sawa na haijafanyika kabisa.
Asante sana
LikeLike
Kabisa.
LikeLike
Chochote Ninachotaka nitazidisha mara kumi ili kukipata.
LikeLike
Vizuri
LikeLike
Ili kupata faida unayotaka unatakiwa uuze mara 10 yake.
LikeLike
Ndiyo
LikeLike
Mara kumi ndio uhesabie kama mara moja,
fanya kwa ukubwa, wingi na msimamo.
LikeLike
Ndiyo
LikeLike
Mara zote ntafanya mara kumi ili kupata matokeo ninayoyataka. ✍️
LikeLike
Vizuri
LikeLike
Sure. Let us think big.
LikeLike
Yes
LikeLike
Kwa kanuni hiyo ya wastani, matokeo yoyote unayotaka kupata, zidisha juhudi mara 10 kisha tekeleza juhudi hizo.
LikeLike
Ndiyo
LikeLike
Mtapambana siku zote kufanya zaidi na kuzidisha mara kumi kwa kila ninachofanya
LikeLike
Kila la kheri
LikeLike
Asante sana
LikeLike
Karibu
LikeLike