3143; Kikosi cha kwanza.
Rafiki yangu mpendwa,
Kila kocha wa mchezo, huwa ana wachezaji wengi kuliko inavyohitajika.
Kwenye wachezaji hao wengi anaokuwa nao, huwa ana kikosi chake cha kwanza.
Kikosi cha kwanza huwa kinakuwa na wale wachezaji bora kabisa ambao kocha anakuwa na imani nao kwamba wanaweza kumpa ushindi mkubwa.
Hicho ndiyo kikosi ambacho kocha huwa anakipanga pale anapokuwa na mashindano makubwa na anayotaka kushinda kwa uhakika.
Wachezaji wanaokuwa kwenye kikosi cha kwanza huwa nao wanajituma sana ili kubaki kwenye kikosi hicho.
Huwa hawajisahau na kuona wameshamaliza, bali wanajua wachezaji wengine wengi waliopo na ambao pia wanapambana kupata nafasi kwenye kikosi hicho cha kwanza.
Ili kuhakikisha wanaendelea kubaki kwenye kikosi hicho cha kwanza, wachezaji huwa wanajitoa kwa kupitiliza.
Wanaweka juhudi kubwa sana ili kuleta matokeo ya tofauti kwenye timu na kuhakikisha kwamba wanategemewa kwenye timu.
Wanahakikisha kama hawapo basi pengo lao linaonekana wazi na hiyo ndiyo inakuwa njia ya kujihakikishia wanaendelea kubaki kwenye kikosi cha kwanza.
Ili kuhakikisha wanabaki kwenye kikosi cha kwanza, wachezaji bora huwa wanazingatia yafuatayo;
1. Kuwa na maandalizi bora kwa kufanya mazoezi kwa viwango vya juu kabisa.
2. Kuweka nguvu kwenye maeneo ambayo wana uimara badala ya kuhangaika na madhaifu waliyonayo.
3. Kujiwekea viwango vya juu sana na kujisukuma kuvifikia ili kuondoka kwenye mazoea.
4. Kuwa na shauku na hamasa ya hali ya juu sana muda wote kitu kinachowapa nguvu ya kuendelea kuweka juhudi.
5. Kuweka vizuri vipaumbele na kutumia muda na rasilimali nyingine kwa ufanisi mkubwa.
6. Kutunza afya ili kuweza kuwa kwenye mchezo muda wote, kuanzia afya ya mwili, akili na roho. Maana mchezo ni mkali, bila afya imara hawawezi kuhimili.
7. Kuendelea kujifunza endelevu na kukazana kuwa bora zaidi ya walivyo. Kutokuwa na kiburi cha kuona tayari wanajua kila kitu na hawana tena cha kujifunza. Kuomba maoni ya kuboresha mchezo wao na kuyafanyia kazi maono hayo.
Kuwa kwenye kikosi cha kwanza haitoshi tu mchezaji kuwa na kipaji kwenye mchezo wake, wengi wana vipaji.
Kuwa kwenye kikosi cha kwanza inahitaji mchezaji kujitoa kwa viwango vya juu sana, kwenda hatua ya ziada kuliko alivyotegemewa na kuwa na msimamo kwenye yote ambayo anayafanya.
Rafiki yangu mpendwa, una njia mbili za kutumia haya maarifa;
Moja ni kujenga kikosi cha kwanza kwenye timu unayoijenga kwenye biashara yako. Angalia wale ambao wana sifa ulizojifunza hapa na kuwaendeleza vizuri ili biashara iweze kupata mafanikio makubwa.
Mbili ni wewe kupambana ili ukae kwenye kikosi cha kwanza kwenye KISIMA CHA MAARIFA na BILIONEA MAFUNZONI.
Ni wengi sana wanaotaka kupata mafanikio makubwa kwenye maisha yao.
Lakini ni wachache pekee wanaoyapata mafanikio hayo.
Siyo kwa sababu wachache hao ndiyo wenye uwezo au bahati, bali kwa sababu ndiyo wanakuwa wamejitoa kwa hali na mali kufanikiwa.
Je wewe umejitoa kiasi gani kuhakikisha unayapata mafanikio makubwa?
Uko tayari kupambana kiasi gani ili kubaki kwenye kikosi cha kwanza?
Unamfanya Kocha wako akutegemee kwenye nini ili kila mara aendelee kukupanga kwenye kikosi cha kwanza?
Jibu maswali hayo kwa uwazi kabisa hapo chini na yafanyie kazi majibu yako ili uendelee kubaki kwenye kikosi cha kwanza cha KISIMA CHA MAARIFA NA BILIONEA MAFUNZONI.
#NidhamuUadilifuKujituma
#AfyaUtajiriHekima
#KaziUpendoHuduma
#UpekeeUdadisiUbunifu
#UshirikianoUtegemeanoUwajibikaji
#BilioneaMafunzoni
#NajengaBiashara
#HakunaKingineMuhimu
#LazimaNitoboe
#NawekaKaziNifanikiwe
Nitapambana kubaki kwenye kikosi cha kwanza kwa kuhakikisha naweka jitihada kwa asilimia 100 katika maeneo ya wateja kukuza mauzo na kuwa na wateja endelevu kwenye biashara yangu kwa wakati wote..
LikeLike
Nimejitoa kwa asilimia 100 kuhakikisha napambana kukaa kwenye mchakato bila kuyumba ili niweze kuwa kwenye kikosi cha kwanza cha kisima cha maarifa na bilionea mafunzoni,na hata kama nitatoka nje ya mchakato nitajikamata haraka na kurudi ili niendelee kukaa kwenye kikosi.
-Nipo tayari kupambana kwa kila hali ili niweze kuendelea kukaa kwenye kikosi cha kwanza
-Kocha nitegemeee kwenye uvumilivu na unganganizi na kukaa kwenye mchakato kwenye yale niliyochagua kuyafanya.
LikeLike
Usiahidi pekee, bali tekeleza pia.
LikeLike
Tekeleza hilo.
LikeLike
Kitu cha kwanza ninachojivunia kwanza maelekezi yote ninayopewa na kocha nayafuata maana ni kwa faida yangu na jamii husika na pia nimeona kuwa bilionea ni
Kuitumia maarifa ninayopewa na kocha bila kuweka uvivu na uzembe ili kocha pia asione katupa maarifa yake kwenye udongo usiyo na rutuba na pia aliongezea siku za karibuni kuwa huwezi kuwa na uchungu alafu usizae mtoto kama kweli unajituma na kutumia maarifa yake vizuri ntahakikisha kwa uhakika nazaa mtoto na bila shaka yoyote kwa maarifa na kujituma huko
LikeLike
Vizuri sana, tekeleza haya.
LikeLike
Nimetoa kwa hali na mali kuhakikisha nakuwa kwenye kikosi cha kwanza.
Nafanya kazi na kukaa kwenye mchakato muda wote ili nibaki kwenye kikosi cha kwanza.
Nakuwa ni tegemeo kwenye kila jukumu ninalowajibu ili kutegemewa na wengine.
LikeLike
Vizuri sana, tekeleza.
LikeLike
Sio kwa kuahidi bali kutenda.Ni kukaa kwenye mchakato kwa asilimia 100.Hiyo ndio itanifanya niwepo kwenye kikosi cha kwanza.
LikeLike
Vizuri sana, tekeleza kwa vitendo.
LikeLike
Kukaa kwenye mchakato kila siku bila ya Kuacha ndio utakaonifanya niwe kwenye kukosi cha kwanza.
LikeLike
Vizuri, tekeleza.
LikeLike
Binafsi nimejitoa kwa asilimia mia moja 💯 kupambana kuhakikisha nakuheshimu kwenye kisima cha maarifa.
_kocha wangu anitegemee kwenye kujifunza zaidi na kuwa tayari kwenda na mabadiliko yanayojitokeza .
Kwa kuwa kisima cha maarifa ndiyo sehemu ya a maisha yangu basi nipo tayari kukaa kwenye mchakato kwa uhakika.
Asante,!!
LikeLike
Vizuri sana, tekeleza kwa uhakika.
LikeLike
Nitapqmbania sana nikae kwenye kikosi cha kwanza kwenye Kisima Cha Maarifa na Bilionea Mafunzoni.
Nitajenga kikosi cha kwanza kwenye Biashara yangu kwani kwa kutekeleza hili itakua nimeboresha ufanyaji kazi wa kitimu.
LikeLike
Vizuri sana, tekeleza kwa uhakika.
LikeLike
Nimejitoa kwa hali zote kuhakikisha nayapata mafanikio makubwa.
Niko tayari kupambana kwa kukaa kwenye mchakato ili nibaki kwenye kikosi cha kwanza.
Kocha anitegemee kwenye uvumilivu na ung’ang’anizi ili kila mara aendelee kunipanga kwenye kikosi cha kwanza
LikeLike
Vizuri, tekeleza kama ulivyoahidi.
LikeLike
Nimejitoa kwa asilimia 100 kukaa kwenye mchakato wa BM Ili kufikia ubilionea
Kocha wangu anitegemee katika unganganizi,uvumilivu na kuwa tayari kujifunza na kufanyia kazi Yale yote ninayoelekezwa, nitakaa kwenye mchakato kwa juhudu zangu zote.
Asante Kocha.
LikeLike
Vizuri, tekeleza kwa uhakika.
LikeLike
Mara zote nitakuwa kwenye kikosi cha kwanza cha KISIMA CHA MAARIFA NA BILIONEA MAFUNZONI kwa sababu nimeshajitoa kwenye hili kuwa sehemu ya maisha yangu.
Asante sana Kocha Dr Makirita Amani
LikeLike
Vizuri sana, ishi humo.
LikeLike
Kwenye hili nimejilea kuwa kwenye kikosi namba Moja Cha ushindi. Nitajitahidi kubakia kwenye Mchakato wa Kila siku Ili nisiikose nafasi hii ya kikosi Cha kwanza.
LikeLike
Vizuri, tekeleza.
LikeLike
nitapambana kuhakikisha najenga sifa Saba ambazo zitanipa nafasi ya kuendelea kuwa katika kikosi cha Kwanza kwenye KISIMA CHAAARIFA na BILIONEA MAFUNZONI. Pia kusimamia miongozo Bora itokanayo na mafunzo Bora ambayo Kocha anaendelea kuyatoa kila mara ili kuhakikisha walio na sifa ya kibaki katika kikosi cha Kwanza kwenye timu yangu ya mauzo siwapotezi Bali kuwafanya kuwa imara kuweza kulikabili pambano. Hii safari sio nyepesi inahitaji kujitoa kusiko kwa kawaida, ninapolegea nitaendelea kujitathmini kuhakikisha siishii njiani. Asante Sana Kocha
LikeLike
Vizuri sana, yaishi haya kwa uhakika.
LikeLike
Mimi ninajitoa kwa kufuata mafunzo na maelekazo yote
Ninayofundishwa. Na pia ninapambana kuyaweka katika vitendo yote ninayofundishwa Ili niweze kutoa matokeo Bora kitu kitakachosababisha nitegemewe na kocha
Wangu na kumfanya aendelee kunipanga na kunitegemea muda wote.
LikeLike
Vizuri, tekeleza.
LikeLike
Asante sana,
Kocha anitegemee kwenye kujenga timu imara sana na ambayo italeta matokeo ninayoyataka na kwenye kisima Cha maarifa na bilionea mafunzoni nahakikisha nakuwa kikosi Cha kwanza
Asante
LikeLike
Vizuri tekeleza.
LikeLike
Nimejitoa kwa asilimia 100 ili niwe kikosi cha kwanza
LikeLike
Vizuri, tekeleza.
LikeLike
Asante kocha,
Nimejitoa kwa nguvu zangu zote ili niwe kikosi cha kwanza.
Ni kusimamia sheria zote na kukaa kwenye mchakato kila siku.
Nataka kocha unisimamie na kuendelea kubaki kikosi cha kwanza.
LikeLike
Vizuri sana, tekeleza hayo.
LikeLike
Ili niwe kwenye kikosi cha kwanza,,
Nahakikisha nakaa kwenye mchakato wa BM bila kukosa.
Nasikiliza ,kujifunza na kuyafanyia kazi yote kutoka kwa kocha na kuyafanya kwa kujituma kwa 100%.
LikeLike
Vizuri, tekeleza.
LikeLike
Ili niweze kupata mafanikio makubwa niko tayari kupambana ili nibaki kwenye kikosi cha kwanza kwa kuweka juhudi katika kile ninachofanya kwa kutumia maarifa sahihi ninayopata na sitaridhika na mafanikio kidogo ninayopata.
Ili niendelee kubaki kwenye kikosi cha kwanza nitapambana kuhakikisha naacha Uvivu, uzembe na mazoe kwenye maisha yangu.
Ili kocha aendelee kunipanga kwenye kikosi cha kwanza ategemee kuona natekeleza yale ninayoahidi.
Asante Kocha.
LikeLike
Vizuri, tekeleza.
LikeLike
Nitajituma kwa nguvu zangu zote kutekeleza yote ninayotakiwa kufanya ili nibaki kikosi cha kwanza.
LikeLike
Vizuri, tekeleza.
LikeLike
Nitapambana ili nikae kwenye kikosi Cha kwanza kwenye KISIMA CHA MAARIFA na BILIONEA MAFUNZONI
1. Nitakuwa na maandalizi Bora na kuweka viwango vya juu kabisa
2. Kuweka nguvu maeneo ambayo nina uimara nayo
3. Nitajiwekea viwango vya juu na kupambana kuvifikia na kuondokana na mazoea
4. Nitakuwa na shauku na hamasa ya hali ya juu sana.
5. Nitaweka vipaumbele na kutumia muda na rasilimali nyingine kwa ufanisi mkubwa
6. Nitaendelea kujifunza endelevu na kukazana kuwa bora zaidi Mara kwa mara
LikeLike
Vizuri sana, tekeleza haya.
LikeLike
Nakutumia na kupambania lengo kuu Kwa kujisukuma zaidi ili.kuweza kutekeleza mchakato mzima wa bilionia mafunzoni
LikeLike
Kila la kheri.
LikeLike
Asante kocha,
Kwanza, nitapambania kwenye timu yangu ninayoijenga kuwa kikosi cha kwanza; yaani watu wenyesifa za mchezaji wa kikosi cha kwanza. Pili, nitahakikisha ninabaki kwenye kikosi cha kwanza kwenye KCM na BM kwa kukaa kwenye mchakato kwa 100%.
LikeLike
Vizuri, fanya hivyo.
LikeLike
Nimejitoa Kwa Hali na mali Ili niweze kubaki kwenye kikosi Cha kwanza
LikeLike
Vizuri, tekeleza.
LikeLike
Ninaenda kukaa kwenye mchakato Kwa asilimia 100
LikeLike
Tekeleza.
LikeLike