3177; Nidhamu na hamasa.
Rafiki yangu mpendwa,
Watu wengi kwenye maisha wamekuwa wanahangaika sana na hamasa.
Wamekuwa wanatafuta vitu vya kuwapa hamasa ili kuendelea na safari yao ya kuelekea kwenye mafanikio makubwa.
Kwa bahati mbaya sana, hamasa haijawahi kuwa na manufaa makubwa kwa mtu, hasa kwenye safari ya mafanikio makubwa.
Hiyo ni kwa sababu hamasa ni hisia na hisia huwa zina tabia ya kuyumba yumba kila mara.
Kama unasubiri uongozwe na hisia, kuna wakati utajisikia kufanya na kuna wakati hutajisikia.
Hamasa ni nzuri kwenye kuanza kitu chochote, ni kama kuwasha kitu.
Lakini ili kuendelea kufanya mpaka matokeo makubwa yapatikane, hamasa pekee haitoshi.
Badala yake unahitaji nidhamu.
Nidhamu ndiyo ufunguo mkuu wa mafanikio.
Nidhamu ni kuweza kujisukuma kufanya kile ulichopanga kufanya iwe unajisikia kufanya au la.
Sehemu kubwa ya mafanikio ambayo watu wanayapata kwenye maisha yao, yanatokana na nidhamu kali wanayokuwa nayo.
Pale mtu anapojijengea nidhamu kali ya kupanga na kufanya bila kuacha, ndiyo unajua mtu wa aina hiyo amedhamiria kweli na lazima atafanikiwa.
Wale wanaokimbizana na hamasa kila wakati, hakuna makubwa wanayofanya.
Hiyo ni kwa sababu wanakuwa wanatumia muda mwingi kwenye kuhangaika na hamasa kuliko kufanya.
Wanakuwa na mlolongo wa vitu vingi vya kutimiza ndiyo waweze kufanya wanachopaswa kufanya.
Lakini kwa upande wa pili wa watu wenye nidhamu kali, kipaumbele chao cha kwanza ni kufanya.
Wanakuwa hawana milolongo mirefu. Wanapanga na kutikiza kama walivyopanga.
Hamasa kwa sehemu kubwa ipo kwenye maneno.
Wakati nidhamu kwa sehemu kubwa ipo kwenye vitendo.
Unaweza kuelezea hamasa vyovyote utakavyo.
Lakini inapokuja kwenye nidhamu, unahitaji kuonyesha.
Kwa sababu kusema ni rahisi na kufanya ni vigumu, nenda na ugumu.
Unapopanga kufanya kitu kwenye muda fulani, na muda huo unafika na ukawa hujisikii kukifanya, hupaswi kwenda na hizo hisia.
Bali unapaswa kwenda na nidhamu.
Ulipanga utafanya, basi fanya kama ulivyopanga bila kuangalia ni hisia gani unazo juu ya kitu.
Hamasa inaweza kufundishwa, ndiyo maana kumekuwa na mafunzo mengi sana kuhusu hamasa, ambayo pia bado yamekuwa hayana uhakika.
Nidhamu haiwezi kufundishwa, ni kitu ambacho mtu anakijenga ndani yake mwenyewe.
Hamasa inaanza na matamanio, hasa ya nje, yanayochochewa na wengine.
Lakini nidhamu inaanza na hasira ambazo mtu anakuwa nazo, kwa mabadiliko yanayotakiwa kufanyiwa kazi.
Nidhamu huwa inajengwa kwa matendo madogo madogo yasiyokuwa na madhara yoyote.
Kadiri unavyokuwa unafanya kwa juhudi kubwa chochote unachokuwa umepanga, ndivyo unavyozidi kuimarisha nidhamu yao ya ufanyaji.
Mwisho ni kupoteza kuna nguvu ya kumjengea mtu nidhamu kali kuliko kupata.
Kwa mfano pale kitu kinapokuwa kimefikia ukomo, watu huwa wanafanya kwa nidhamu kali hata kama hawajisikii kufanya.
Hivyo basi, kama umekuwa na tatizo la kukosa nidhamu, chagua kuwa na mtu atakayehakikisha kuna kitu kikubwa unachopoteza kama hutafanya kama ulivyopanga kufanya.
Kwa kuwa na mtu anayekuwajibisha, ambaye hatasikiliza sababu na visingizio vyako, utaweza kujenga nidhamu kali ya kufanya kwa msimamo bila kuacha.
Ukipanga, fanya.
Wakati wa kufanya unapofika na ukawa hujisikii kufanya, hapo hapo anza kufanya.
Ukiahidi, timiza.
Wakati wa kutekeleza unapofika na ukawa unatafuta sababu na visingizio, hapo hapo anza utekelezaji.
Ukiweza kujenga nidhamu kali ya kuamua na kufanya kwa msimamo bila kuacha, hakuna kitakachoweza kukuzuia usipate chochote unachotaka.
#NidhamuUadilifuKujituma
#AfyaUtajiriHekima
#KaziUpendoHuduma
#UpekeeUdadisiUbunifu
#UshirikianoUtegemeanoUwajibikaji
#BilioneaMafunzoni
#NajengaBiashara
#HakunaKingineMuhimu
#LazimaNitoboe
#NawekaKaziNifanikiwe
Ukiweza kuwa na nidhamu kali ya kuamua na kufanya utaweza kufanikisha chochote unachotaka.
LikeLike
Hilo halina ubishi.
LikeLike
Ili upate chochote ambacho unakipata ni lazima uwe na Nidhamu kubwa. Binafsi nitahakikisha nakuwa na Nidhamu kubwa ili kufikia malengo makubwa..
LikeLike
Kila la kheri.
LikeLike
Nidhamu inajengwa Ila hamasa ni hisia na matamanio ya nje. Ninajenga nidhamu binafsi ya kufanya nilichopanga. Muda ukifika nisifanye kitu kingine Bali kitu hicho tu au hapana.
Kuwa na mbadala wa kitu Cha kufanya ndiyo inayonifanya kuzembea na kuahirisha nikicho jipangia kufanya.
LikeLike
Vizuri.
LikeLike
Asante kocha nitajijengea nidhamu takupanga nakufanya
LikeLike
Vizuri
LikeLike
Hamasa ni tiba ya muda mfupi kwenye maradhi ya muda mfefu, nidhamu ndio inayohitajika sana
Asante sana
LikeLike
Hakika
LikeLike
Nidhamu ndiyo msingi mkuu wa kufanikiwa.
LikeLike
Hakika
LikeLike
Nitaendelea kupambana na kuchukua ili kuifanya hamasa kuwa na maana zaidi
LikeLike
Vizuri
LikeLike
Ahsnate sana kocha, kila nikipanga nitafanya bila visingizio vyovyote
LikeLike
Kila la kheri.
LikeLike
Hongera sana Kocha kwa makala hii. Hakika umeeleza vizuri sana tofauti ya nidhamu na hamasa. Wengi tunatamani kuwa na maisha yenye mafanikio ila nidhamu ya kutekeleza yale majukumu yakutuwezesha kupata mafanikio hayo ndo tatizo kwa walio wengi. Nitaendelea kujisukuma kahakikisha nakuwa na nidhamu kwa kila ninachopanga kufanya.
Asante sana.
LikeLike
Kila la kheri
LikeLike
Asante Kocha,
Mafanikio makubwa yanahitaji nidhamu Kali, hamasa ni kichocheo(trigger) tu
LikeLike
Kabisa.
LikeLike
Nidham ni matendo na hamasa ni maneno
LikeLike
Ndiyo
LikeLike
Ninajenga nidhamu kali ya kuamua na kufanya kwa msimamo bila kuacha, Kuanzia Sasa sitasubiri hamasa katika kuamua.
Nikipanga nitafanya
Nikiahidi nitatimiza
LikeLike
Kila la kheri
LikeLike
Kwa siku hizi hamasa ni bidhaa inayopatikana kila mahali, hasa katika mitandao yq kijamii
Nidhamu imekuwa bidhaa adimu sana, nikitambua kuwa huwezi kufanya makubwa bila ya kuwa na nidhamu natambua mchango mkubwa wa mchakatoo huu kuniweka katika nidhamu ya juu sana.
LikeLike
Hakika
LikeLike
Shukrani kocha tujenge nidhamu kali Sana, na
Hasira ya kutimiza uliyopanga,hata Kama ujisikii kufanya.
LikeLike
Ndiyo
LikeLike
Nidhamu kila mara ni bora kuliko hamasa
LikeLike
Ndiyo
LikeLike
Nidhamu huwa inajengwa Na matedo madogo madogo yasiyokuwa Na madhara yoyote
LikeLike
Hakika
LikeLike
Asante kocha,Nitajitahidi kuwa na nidhamu na kufanya bila kuyumba.
LikeLike
Kila la kheri.
LikeLike
Kitu kinapokuwa kimefikia ukomo, watu huwa wanafanya kwa nidhamu kali hata kama hawajisikii kufanya.mfano huu ni kama dawa ya mswaki,kadiri unavyoitumia na kupungua kuna nidhamu flani kali ya kubana matumizi inajengeka. Asante Kocha.
LikeLike
Mfano sahihi kabisa.
LikeLike
Nahitaji kujenga nidhamu kubwa na siyo hamasa ambayo ni hisia tuu
LikeLike
Vizuri
LikeLike
Hamasa inabembeleza kufanya lakini nidhamu inakulazimisha kufanya iwe unajisikia kufanya au la.
Asante sana Kocha Dr Makirita Amani.
LikeLike
Hakika
LikeLike
Nidham huwa inajengwa na matendo madogo madogo yasiokua na madhara yeyote.
LikeLike
Ndiyo
LikeLike
Ni kweli inatokana na hasira ya kufanya ili kupata mabadiliko
LikeLike
Ndiyo.
LikeLike
Nidhamu ni kuweza kujisukuma kufanya kile ulichopanga kufanya iwe unajisikia kufanya au la.
LikeLike
Sahihi.
LikeLike
Nidhamu,kwa kweli Nidhamu binfsi ni muhimu sana,hasa kwenye kujiongoza na kujisimamia.
LikeLike
Hakika
LikeLike
Nidhamu Kali na kuamua inakupa kile unachotaka
LikeLike
Ndiyo
LikeLike
Nitajenga nidhamu kali dhidi ya hamasa katika kuyaendea mafanikio makubwa.
LikeLike
Kila la kheri
LikeLike