3193; Ndiyo sababu ya kufanya.
Rafiki yangu mpendwa,
Karibu kila mtu anajua nini hasa anachotaka kwenye maisha yake.
Na pia wengi wanajua nini wanapaswa kufanya ili kupata wanachotaka.
Lakini cha kushangaza, inapokuja kwenye kufanya, wengi huwa hawachukui hatua.
Tunaweza kushangaa kwa nje, iweje watu washindwe kufanya kile wanachojua kabisa kwamba wanapaswa kufanya ili wapate wanachotaka.
Lakini kuna mengi yanayokuwa yanaendelea ndani ya mtu ambayo hatuaezi kuyajua.
Inapokuja kwa mtu mwenyewe, ambaye anajua kabisa anachopaswa kufanya ili kupata anachotaka, lakini anakwama kufanya, kile kinachomkwamisha ndiyo kinapaswa kuwa sababu ya yeye kufanya.
Yaani kile ambacho kinamzuia asifanye, ndiyo hicho hicho anapaswa kukitumia kama sababu ya kufanya, kimpe msukumo wa kufanya.
Kwa wengi kinachowazuia kufanya ni hofu. Hofu huwa zipo mbalimbali kama hofu ya kushindwa na hata hofu ya kufanikiwa.
Wengi huwa wanaingiwa na hofu kama watafanya halafu wakashindwa, wanaona watakuwa wamepoteza sana. Au kama watafanya wakafanikiwa, watakuwa wamejiongezea majukumu zaidi.
Kama mtu anakwamishwa kufanya na hofu, anatakiwa kuigeuza hofu hiyo kama sababu ya kufanya.
Yaani pale mtu anapopata hofu ya kufanya, ndiyo hapo hapo anatakiwa afanye.
Hiyo ni kwa sababu hofu ni kiashiria cha kutoka nje ya mazoea.
Huwezi kupata hofu pale unapofanya vitu ulivyozoea kufanya.
Ni pale unapotaka kufanya kitu kipya na cha tofauti ndiyo hofu kubwa huwa inakuingia.
Na hiyo ndiyo sababu kwa nini unapaswa kufanya kile unachohofia kufanya, kwa sababu ndiyo njia ya kutoka pale ulipokwama sasa.
Hivyo ukipatwa na hofu, badala ya kuacha, itumie hofu hiyo kama kichocheo cha kuanza kufanya mara moja.
Kitu kingine kinachowazuia wengi wasichukue hatua ni kujifanya ni wastaarabu kupitiliza.
Hapa watu wanaacha kufanya kwa sababu hawataki kuonekana ni wasumbufu kwa wengine.
Watu wanakuwa wanataka waonekane ni wastaarabu na hawana tatizo lolote.
Lakini pia huu ni mtego ambao unapaswa kuuvuka kama unataka kupiga hatua.
Inapokuja kwenye kupata kile hasa unachotaka, unaweza kukipata au unaweza kujifanya mstaarabu, huwezi kuwa navyo vyote kwa pamoja.
Ili uweze kupata chochote kile unachotaka, lazima uwasumbue watu wengi.
Hivyo basi, kama kinachokuzuia kufanya ni kutokutaka kuwasumbua wengine, hiyo ndiyo sababu kwa nini unatakiwa kufanya.
Kwa sababu ni kupitia kuwasumbua watu ndiyo wanakukumbuka kwa muda mrefu na kukufikiria wewe pale wanapokuwa na uhitaji.
Kwa chochote kile unachofanya, kama hakuna mtu yeyote amewahi kukuambia unamsumbua, maana yake ni hujafanya kwa ukubwa wa kutosha kukupa mafanikio unayotaka.
Unapokuwa unajikwamisha kufanya kwa sababu unataka uonekane mstaarabu, hapo hapo ndiyo unapaswa kuanza kufanya, tena kufanya kwa ukubwa ambao utawagusa wengi.
Kwenye maisha ni bora kuchukiwa kuliko kupuuzwa. Wanaokuchuki watakuwa wanakujua na wanakufikiria kwa muda mrefu, wakati wanaokupuuza hawajui hata kama upo, hivyo hakuna namna unaweza kunufaika nao.
Fanya kile unachopaswa kufanya, kwa sababu hata usipofanya, unakuwa hujatatua tatizo kuu ulilonalo.
Tatizo lolote unalokuwa nalo, litaweza kutatuliwa kwa wewe kufanya kile kinachohusisha eneo hilo.
Inapokuja kwa wewe kufanya unachopaswa kufanya ili kupata unachotaka, jua unapaswa kufanya hasa.
Na chochote kile kinachokuzuia usifanye, hicho hicho ndiyo kinakuwa sababu ya wewe kufanya.
Kila kikwazo kinachokuzuia, unapaswa kukigeuza kuwa njia ya kufika kule unakotaka.
Hatupaswi kuruhusu chochote kituzuie kupata kile hasa tunachotaka.
Ipo ndani ya uwezo wa kila mmoja wetu kuweza kupata chochote kile anachotaka.
Kinachohitajika ni mtu kuwa tayari kuendelea kufanya bila ya kuruhusu kumwamishwa na chochote kile.
Kama utafanya kilicho sahihi na ukakifanya kwa muda mrefu zaidi, lazima utafanikiwa.
#NidhamuUadilifuKujituma
#AfyaUtajiriHekima
#KaziUpendoHuduma
#UpekeeUdadisiUbunifu
#UshirikianoUtegemeanoUwajibikaji
#BilioneaMafunzoni
#NajengaBiashara
#HakunaKingineMuhimu
#LazimaNitoboe
#NawekaKaziNifanikiwe
Fanya kile unachphofia na utafanikiwa kugundua kuwa wala hakina maana ya kuhofia wasumbue watu ili wakuweke kwenye akili zao na pia fanya kwa ukubwa ili uguse maisha ya wengi
LikeLike
Hakika.
LikeLike
ahsante
1, hofu inaondoka kwa kufanya unacho hofia
2. kuhusu ustarabu – ustarabu pekee ni kuuza na kuhakikisha maisha ya wengine yana kuwa bora kupitia kile unachofanya.
ahsante
LikeLike
Hakika, hakuna ustaarabu kama una kitu ambacho wengine wanakihitaji sana halafu huhakikishi wanakipata.
LikeLike
Ni bora kuchukiwa kuliko kupuuzwa.
LikeLike
Kupuuzwa ni sawa na kifo.
LikeLike
Ni kweli kabisa kuwa tunaiondoa hofu kupitia kufanya!
LikeLike
Tufanye na hofu itakimbia yenyewe.
LikeLike
Asante kocha ni kweli kabisa ukihofia kitu kifanye na hofu itakimbia
LikeLike
Ndiyo.
LikeLike
Dawaya ya hofu ni kufanya kile ninachohofia.
Asante sana Kocha
LikeLike
Ndiyo
LikeLike
Asante Kocha,
Kile chema ninachokihofia nitakifanya ili kuiondoa hofu.
Ninaacha ustaarabu ili shughuli ziwe bora na kuzifanya kwa ukubwa.
LikeLike
Vizuri, tekeleza hivyo.
LikeLike
Ukiwa mstaarabu wa kutokuchukua hatua utakuja kuchekwa na wale ambao unataka wakuone mstaarabu.
Asante sana
LikeLike
Kabisa, ustaarabu bila hatua ni uvivu.
LikeLike
Kile unachohofia kuKifanya ndio unachopaswa kukifanya tena Kwa ukubwa sana na tuache ustaarabu uliopitiliza
Asante sana
LikeLike
Kabisa, kilicho muhimu ni kufanya.
LikeLike
Kile kinachonizuia kufanya ndio kiwe sababu ya mimi kufanya
Mfano, ninapokuwa na hofu ya kufanya kitu natakiwa kufanya maana Ni kiashiria kuwa ndio natoka kwenye mazoea na kwenda kufanya kwa utofauti.
LikeLike
Kabisa, hofu inakuonyesha unatoka kwenye mazoea yako, kitu ambacho ni kizuri.
LikeLike
Hofu yako ya kufanya ndiyo sababu yako kubwa ya kufanya. Nashukuru kwa ujumbe huu Kocha maana Hofu miehuwa inanitawala Sana kwenye baadhi ya mambo ninayoyaka kufanya, kumbe nimekuwa nikijikwamisha mwenyewe. Nitaitumia Hofu yangu kufanya maamuzi na Kufanya kwa shauku kubwa.
LikeLike
Hofu inapaswa kuwa kiashiria cha njia sahihi kwako na siyo kikwazo cha kufanya.
LikeLike
Hofu ndiyo inapaswa kunipa msukumo wa kufanya zaidi
LikeLike
Ndiyo, unapopatwa na hofu ndiyo unapaswa kufanya zaidi.
LikeLike