KITABU; Philosophy for life and other dangerous situations : ancient philosophy for modern problems / Jules Evans
Kurasa; 197 – 206..

Kumekuwa na jitihada mbalimbali za kuchagua falsafa moja ambayo inaweza kuleta maisha mazuri na ya furaha kwa kila mtu.
Lakini kila falsafa imekuwa inawafaa watu fulani na wengine kuikataa, hata kama ni falsafa nzuri kiasi gani.

Mwanafalsafa Aristotle ambaye alikuwa mwanafunzi wa Mwanafalsafa Plato, aliamini kwamba, mtu anakuwa na maisha bora na yenye furaha pale anapotimiza kusudi lake hapa duniani.
Alisema kwamba kila mtu anapaswa kufanya kile ambacho anaweza kukifanya vizuri na kina mchango kwa wengine.

Aristotle alifundisha zaidi kuhusu umuhimu wa kuishi kijamii, kuishi kwa ajili ya wengine kwa sababu hiyo ndiyo njia pekee ya kuweza kufanya mazuri kwa ajili ya wengine.

Pamoja na falsafa hii ya Aristotle kuonekana ni nzuri kwa maisha mazuri na yenye furaha, bado haiwafai watu wote.
Hivyo tunarudi kwenye msingi kwamba, kila mtu ana falsafa yake ambayo inamwezesha kufanya kile anachofanya vizuri.
Na hivyo njia pekee ya kuwa na maisha mazuri, yenye furaha na mafanikio ni mtu kuishi ile falsafa yenye maana kwako, na kuwaruhusu na kuwavumilia wengine kuishi falsafa zenye maana kwao.

Hakuna kitu kimoja kinachowafaa wote, hata kama kitakuwa kitu kizuri kiasi gani.
Chagua kinachokufaa wewe, na waache wengine wachague kinachowafaa.

Kocha Makirita Amani,
http://www.amkamtanzania.com/kurasa