Ni rahisi sana kwetu kuyaona makosa ya wengine,

Ni rahisi kuyaonesha na hata kuyaelezea,

Ni rahisi pia kuyacheka na kukejeli makosa ya wengine,

Kwa sababu tunafikiri sisi hatuwezi kufanya makosa kama hayo, hatuwezi kuwa wajinga kiasi hicho.

Lakini huku kote ni kujidanganya.

Kosa lolote analoweza kufanya mwingine, wewe pia unaweza kufanya.

Hivyo badala ya kuyacheka makosa ya wengine, badala ya kujiona wewe ni bora sana kwa sababu makosa yako hayajaonekana, jifunze kupitia makosa hayo ya wengine.

Kila unapomwona mwingine anakosea, jua hata wewe unaweza kukosea kama yeye, na wakati mwingine kukosea zaidi.

Hivyo angalia kipi cha kujifunza kutoka kwenye makosa ya wengine, namna gani ya kutokurudia makosa waliyofanya wengine na jinsi ya kuepuka kuingia kwenye makosa hayo kwenye maisha yako.

Kwa kujifunza hivi utaweza kuwa bora zaidi na pia hutaingia kwenye matatizo na wengine kwa kucheka au kusema zaidi matatizo yao, ila utajifunza na kuwa bora.

Kila la Kheri Rafiki Yangu.

Rafiki na Kocha wako,

Dr. Makirita Amani,

www.amkamtanzania.com/kocha