Tone moja la maji halina madhara yoyote kwenye kitu chochote kile.
Lakini tone hilo moja linapojirudia kwa muda mrefu kwenye eneo moja, lina nguvu kubwa ya kuleta mabadiliko makubwa. Tone hilo likijirudia kwa muda mrefu kwenye eneo moja linaweza kuvunja mwamba mkubwa na mgumu.
Hivyo pia ndivyo ilivyo kwa nguvu zetu sisi binadamu, tunaweza kuona hatuna nguvu ya kufanya yale makubwa tunayotaka kufanya. Lakini tunapoanza kidogo kidogo na kuwa na msimamo na ung’ang’anizi, hakuna kinachoweza kutuzuia.
Msimamo ni pale unaporudia kufanya jambo kila wakati bila ya kuacha. Ung’ang’anizi ni pale unapoendelea kufanya jambo licha ya kukutana na ugumu ambao unawafanya wengine kukata tamaa na kuacha.
Wewe jijengee vitu hivi viwili, rudia kufanya na ng’ang’ana, na utashangaa jini utakavyoweza kuvunja miamba mikubwa na kufikia mafanikio makubwa ambayo kwa wengi ni ndoto.
Kufikia hayo, lazima uwe na subira, ujipe muda na kuweka kazi kweli, kazi yenye msimamo, kwa kuiweka muda wote.
Kila la Kheri Rafiki Yangu.
Rafiki na Kocha wako,
Dr. Makirita Amani,