Kama mvua itanyesha kesho, haina msaada wowote kulowa leo.
Badala yake unaweza kuitumia leo kufanya maandalizi bora ya kesho, ili mvua inaponyesha, usilowe.
Tumekuwa tunaruhusu mambo ambayo hayajatokea yatuumize, na baadaye mambo hayo huwa hayatokei kama tulivyotegemea.
Usikubali hofu ya jambo lolote linaloweza kutokea kesho ikusumbue leo.
Chagua kuiishi leo, kwa yale unayokabiliana nayo leo, na kama kuna jambo unafikiri litatokea kesho, usiruhusu likusumbue leo.
Mambo mengi unayohofia kuhusu kesho hayatatokea kama unavyoyahofia, hivyo usiyaruhusu yaharibu leo yako.
Ishi leo, ishi kwenye wakati uliopo, fanya kilicho sahihi na hapo utaweza kuwa na maandalizi mazuri ya chochote kinachoweza kutokea kesho.
Kila la Kheri Rafiki Yangu.
Rafiki na Kocha wako,
Dr. Makirita Amani,