
Maamuzi yoyote makubwa na muhimu huwa yanafanywa na watu wawili mpaka watatu wenye ushawishi mkubwa na kisha kusukumwa kwa wengine wakubaliane nayo na kuonekana ni maamuzi ya wengi.
Ni vigumu kwa watu wengi kufikia maamuzi kwa pamoja kwa sababu kila mtu anakuwa na mtazamo wake ambao unatofautiana na wa wengine.
Kama kuna mabadiliko unataka kuleta au kushawishi yatokee, badala ya kuhangaika na kundi kubwa la watu, jua wachache wenye madaraka na ushawishi na hangaika na hao.
Watu wengi kwenye maisha ni rahisi kufuata mkumbo kuliko kufikiria na kufanya maamuzi yao wenyewe. Wajue wale wenye ushawishi mkubwa na wanaofikiri na kufanya maamuzi na utawezesha mengi kutokea.
Kadhalika, unapokuwa kwenye kundi au kamati yoyote jua wale wenye nguvu ya kufanya maamuzi na hakikisha unakuwa sehemu yao kama unataka kuleta matokeo fulani.
Ukurasa wa kusoma ni kuhusu kiki, propaganda na wahamisha maada, fungua; http://www.kisimachamaarifa.co.tz/2021/02/15/2238
#NidhamuUadilifuKujituma #AfyaUtajiriHekima #KaziUpendoHuduma