2400; Kinachofanya mabadiliko kuwa magumu kwako…

Ni kwa sababu unahangaika na kitu kisichokuwa sahihi.
Unaweka juhudi zako eneo ambalo haliwezi kuzalisha mabadiliko.

Unahangaika na matokeo badala ya kile kinachozalisha matokeo hayo.
Unahangaika na matawi badala ya shina.

Kama unataka kuyabadili maisha yako, usihangaike na yale matokeo unayopata sasa, bali hangaika na kinachozalisha matokeo hayo.

Vile ulivyo sasa, ni matokeo ya imani kuu uliyonayo kwenye maisha yako.
Kile unachoamini ndiyo kinazalisha mtazamo, mtazamo unazalisha fikra ambazo zinachochea matendo, yanayokuwa tabia na tabia kuwa hatima yako.

Ili kubadili hatima yako, rudi kwenye chanzo kikuu ambacho ni imani uliyonayo sasa.

Kwenye kila eneo la maisha yako, kuna imani ambazo unazo juu yako na eneo hilo.
Anza kwa kubadili imani ulizonazo na hivyo ndiyo utaweza kuchochea mabadiliko kwenye maisha yako.

Usihangaike na yasiyo na nguvu ya kuleta mabadiliko. Weka nguvu zako eneo sahihi ili uweze kuzalisha matokeo sahihi.

Kocha.