Kila mmoja wetu ana masaa 24 pekee kwenye siku yake, hakuna mwenye uwezo wa kuongeza hata sekunde moja kwenye siku yake.

Ni katika masaa hayo hayo ndiyo kila mtu anayatumia kufanya yale muhimu kwake.

Kama hupati muda wa kufanya kitu, siyo kwa sababu muda haupo, bali kwa sababu hujakipa kitu hicho kipaumbele, siyo kitu muhimu kabisa kwako.

Kama kitu ni muhimu unatenga muda wa kukifanya na siyo kusubiri mpaka upate muda.

Ukurasa wa kusoma leo ni hupati muda; http://www.kisimachamaarifa.co.tz/2021/08/06/2410

#NidhamuUadilifuKujituma #AfyaUtajiriHekima #KaziUpendoHuduma