#SheriaYaLeo (19/366); Sikiliza Mamlaka Yako Ya Ndani.

Upo hapa duniani siyo tu kwa ajili ya kutimiza tamaa zako na kutumia vile wengine wametengeneza, bali pia kuchangia, kutimiza kusudi kubwa.
Ili kuweza kutimiza kusudi hilo, lazima utengeneze kile cha kipekee ndani yako.

Acha kusikiliza sana maneno na maoni ya wengine wanaokuambia unapaswa kuwaje na nini ufanye na usifanye.
Hukumu vitu wewe mwenyewe, hoji kila unachofikiria na kila hisia unazokuwa nazo.

Jijue wewe mwenyewe kiundani, yale unayopendelea na kazi zinazokuvutia.
Weka juhudi kila siku kuwa bora zaidi kwenye maeneo hayo ya kipekee kwako na yanayotimiza kusudi lako.
Ongeza utofauti ili kutengeneza kitu kinachokuwa cha kipekee sana kwako na kwa wengine.

Kubali kile kinachokufanya wewe kuwa wa tofauti na kukifanyia kazi.
Kutokufuata njia hiyo ndiyo chanzo cha msongo na sonona kwa wengi.
Unapokuwa na msongo au sonona ni wito wa kusikiliza mamlaka yako ya ndani.

Sheria ya leo; Kumbuka nyakati za maisha yako ulipokuwa unajisikia hai kwa kufuata njia yako na nyakati ulizokuwa unajisikia mfu kwa kufuata njia za wengine. Linganisha hisia hizo na utaona jinsi ilivyo muhimu kusikiliza mamlaka yako ya ndani ili ujisikie hai muda wote na kufanya makubwa.

#NidhamuUadilifuKujituma
#AfyaUtajiriHekima
#KaziUpendoHuduma