#SheriaYaLeo (175/366); Jinsi ya kuwafanya watu wawe tayari kukusaidia.
Kama unataka watu wakusaidie kitu fulani, usiwakumbushe jinsi ambavyo wewe umewahi kuwasaidia huko nyuma.
Unaweza kudhani kwa kuwakumbusha hilo wataona wanapaswa kulipa fadhila na hivyo kusukumwa kukusaidia.
Lakini siyo kinachotokea.
Unapowakumbusha watu jinsi ulivyowasaidia huko nyuma unawafanya wajione hawajiwezi na wanategemea wengine.
Watu huwa hawapendi kujisikia hali hiyo, huwa wanapenda kuona wako huru na wanajitegemea wenyewe.
Ukitaka watu wakusaidie, wakumbushe jinsi ambavyo wamewahi kukusaidia huko nyuma.
Kwa kuwakumbusha hilo, unawafanya wajione ni watu wenye kujali na wanaosaidia wengine.
Hivyo na sasa watataka kukusaidia ili kulinda sifa hao hiyo.
Watakusaidia ili waendelee kuonekana ni watu wema na wanaojali.
Hilo pia linafanya kazi kwenye kuvunja uadui.
Pale unapomfanya adui ajione ni mtu mbaya, atazidi kuwa mbaya kweli.
Lakini unapomfanya ajione ni mtu mzuri, atabadilika na kuwa mzuri ili kutunza sifa yake hiyo.
Wape watu sifa ambayo watakuwa tayari kukusaidia ili kuendelea kutunza sifa hiyo. Kwa njia hiyo utapata kirahisi msaada wowote unaotaka kutoka kwa wengine.
Sheria ya leo; Ukitaka watu wakusaidia, usiwakumbushe ulivyowasaidia huko nyuma, bali wakumbushe walivyowahi kukusaidia huko nyuma. Wafanye wajione ni wakarimu kuliko kuwafanya wajione wanapaswa kulipa fadhila.
#NidhamuUadilifuKujituma
#AfyaUtajiriHekima
#KaziUpendoHuduma
#UpekeeUdadisiUbunifu
#UshirikianoUtegemeanoUwajibikaji