#SheriaYaLeo (338/366); Kiangalie kifo chako.

Wengi wetu huwa tunatumia muda mwingi wa maisha yetu kujaribu kukiepuka kifo.
Kifo ni kitu ambacho hakuna namna tunaweza kukikwepa, hivyo tunapaswa kukifikiria muda wote.

Kwa kuelewa ufupi wa maisha yetu hapa duniani, inatufanya tuishi kwa kusudi na kuyaharakishia malengo yetu.
Kujifunza kukubaliana na uhalisia huu, inatuwezesha kukabiliana na vikwazo mbalimbali tunavyokutana navyo kwenye maisha.
Inatusaidia kuweka vipaumbele vyetu kwa usahihi, kujua kipi muhimu zaidi kwenye maisha yetu mafupi ya hapa duniani.

Watu wengi hukazana kujitenga na wengine na kujiona wapo juu yao.
Tunachopaswa kukumbuka ni wote tunafanywa sawa kwenye kifo, wote tutakufa.
Kwa kutulinganisha, kifo kinatuunganisha pamoja.

Sheria ya leo; Kwa kuwa na uelewa mpana wa ukomo wa maisha yetu, tunaweza kuyaishi kwa ukamilifu zaidi.

#NidhamuUandilifuKujituma
#AfyaUtajiriHekima
#KaziUpendoHuduma
#UpekeeUdadisiUbunifu
#UshirikianoUtegemeanoUwajibikaji