3249; Maarifa pekee hayatoshi.
Rafiki yangu mpendwa,
Moja ya mapingamizi ya watu wasiopenda kusoma vitabu ni kwamba hata waandishi na wauzaji wa vitabu hivyo hawajaweza kunufaika na kile kilichoandikwa kwenye vitabu hivyo.
Huwa kuna utani kwamba mtu aliandika kitabu cha jinsi ya kupata mtaji wa kuanza biashara. Lakini akashindwa kuchapa kitabu hicho kutokana na kukosa mtaji.
Wanachofikiri wengi ni kwamba ukishapata maarifa basi kimiujiza unabadilika kupitia maarifa hayo.
Hicho ni kitu ambacho hakina hata chembe ya ukweli.
Ni kweli maarifa ni muhimu ili mtu aweze kufanikiwa.
Lakini ni sehemu ndogo sana ya yale yanayohitajika ili kufanikiwa.
Ili maarifa yalete matunda, lazima yawekwe kwenye vitendo.
Ndiyo maana kanuni kuu ya KISIMA CHA MAARIFA NI MAARIFA + VITENDO = MAFANIKIO.
Kupitia kanuni hiyo na hata uelewa wa mawaida, tunakubaliana kwamba maarifa pekee hayamtoshi mtu kufanikiwa.
Lazima mtu ayaweke maarifa hayo kwenye vitendo ndiyo yaweze kumpa matokeo mazuri.
Wengi kwa kusikia kinachohitajika ni kuweka maarifa kwenye vitendo ndiyo kunaleta mafanikio, wanakazana kufanya hivyo.
Lakini bado hawapati mafanikio wanayokuwa wanayataka.
Kinachokuwa kimetokea ni wengi kukata tamaa haraka kabla ya kupata mafanikio.
Wanapochukua hatua na kuona mafanikio waliyoyataka hayaji, wanakata tamaa na kuacha.
Ili mtu kuweza kuvuka hayo na kujenga mafanikio makubwa kwenye maisha yake kupitia maarifa anayopata, anahitaji vitu viwili; Kocha na Uwajibikaji.
Kocha anakusimamia kwenye utekelezaji wa yale yote uliyojifunza.
Kocha hatakuachia ukate tamaa na kuacha pale mambo yanapokuwa magumu.
Badala yake atahakikisha unaendelea kuchukua hatua mpaka unapata matokeo unayokuwa unayata.
Uwajibikaji unafanya gharama ya kutokufanya kuwa kubwa kuliko ya kufanya.
Yaani inakuwa ina gharama kubwa kwako kama utaacha kufanya, kuliko ukifanya.
Hilo linakusukuma ufanye hata kama bado huoni matokeo.
Hivyo rafiki yangu mpendwa, kama unayataka mafanikio makubwa kwenye maisha yako, unahitaji kuwa na Kocha ambaye atahakikisha unafanya bila ya kuruhusu sababu zozote zikukwamishe.
Pia unahitaji mfumo wa uwajibikaji ambao unakusukuma kufanya bila kuacha hata kama matokeo ni tofauti na ulivyopanga.
Vitu hivyo viwili vina nguvu kubwa ya kumwezesha mtu kufanya makubwa kwenye maisha yake.
Na kwa bahati nzuri sana, kama unasoma hapa, tayari unavyo vitu hivi.
Tayari unaye Kocha aliye tayari kukusimamia kuweka kwenye matendo yale unayojifunza.
Lakini pia upo mfumo wa uwajibikaji unaokulazimisha ufanye ili usiingie gharama kubwa.
Mfumo huo ni wa kuchukua hatua kidogo kidogo kwa kushirikisha kwa wengine.
Ukishapata maarifa, jipongeze maana hapo umekamilisha hatua moja kati ya hatua 100.
Hatua 99 zilizobaki ni za kuchukua hatua kwenye yale ambayo umejifunza.
Tekeleza hatua hizo 99 ili uweze kupata mafanikio unayoyataka.
#NidhamuUadilifuKujituma
#AfyaUtajiriHekima
#KaziUpendoHuduma
#UpekeeUdadisiUbunifu
#UshirikianoUtegemeanoUwajibikaji
#BilioneaMafunzoni
#NajengaBiashara
#HakunaKingineMuhimu
#LazimaNitoboe
#NawekaKaziNifanikiwe
No kweli maarifa pekee hayaishi ni lazima kuweka kwenye matendo na Nitahakikisha kila ninachojifunza naweka kwenye matendo hadi nitoke kwenye group la wale wanaouza lakini hawaitendeo kazi
LikeLike
Kila la kheri.
LikeLike
Kweli kupata maarifa ni hatua moja, bado hatua nyingine 99 kuyafikia mafanikio.
LikeLike
Ndiyo
LikeLike
Maarifa na uwajibikaji yanaleta msimamo wa matokeo.
LikeLike
Hakika
LikeLike
Maarifa na vitendo ndio mpango mzima katika mafanikio tunayotaka
Asante sana
LikeLike
Hakika.
LikeLike
Asante Kocha,
Umenikumbusha kuwa ni gharama kubwa kwangu kutokufanya (kutowajibika ipasavyo). Gharama ni ndogo ninapoendelea kufanya hata kama matokeo ni nnje ya matarajio.
LikeLike
Kabisa
LikeLike
Ili maarifa yalete matunda, lazima yawekwe kwenye vitendo.
Ili kuweza kujenga mafanikio makubwa kwenye maisha kupitia maarifa mtu anayapata anayoyapata, anahitaji vitu viwili, Kocha na Uwajibikaji
Noted with thanks Kocha.
LikeLike
Karibu
LikeLike
MAARIFA + VITENDO = MAFANIKIO.
LikeLike
Hiyo ndiyo kanuni.
LikeLike
_Maalifa yanamchango mdogo Sana katika mafanikio
_Ili kupata mafanikio unapaswa maalifa kuyaweka ktk
vitendo
_ Na ili kupata mafanikio makubwa na ya uhakika basi
huna budi utimize Mambo haya matatu ambayo ni
Uwe na maalifa, uyaweke maalifa hayo ktk vitendo
pia uwe na kocha atakaekupa miongozo pia kukusimamia kuhakikisha unatimiza wajibu wako.
LikeLike
Hakika
LikeLike
Maarifa pekee hayatoshi kunipa mafanikio ninayoyataka, ni lazima niweke kwenye matendo maarifa hayo.
LikeLike
Kabisa
LikeLike
Naenda kutekeleza Kwakuchukua hatua
LikeLike
Vizuri
LikeLike
No kweli maarifa peke yake hayaishi ni vema kufanya kwa vitendo ili kuendana na maarifa hayo
LikeLike
Hakika
LikeLike