3294; Onekana, weka kazi na sikiliza.
Rafiki yangu mpendwa,
Kwa kipindi ambacho nimekuwa natoa hii huduma ya mafunzo na ukocha, nimejifunza mengi sana kuhusu watu.
Nimejifunza hayo kwa nadharia na kwa vitendo pia kutoka kwenye tabia halisi za watu.
Kwenye nadharia nimekuwa najifunza mara kwa mara vitu vitatu vinavyohitajika ili huduma ya ukocha iweze kuwa na manufaa kwa mtu.
Na hapo kuna mambo matatu ambayo lazima yawepo.
Moja ni lazima mtu aonekane, hapa ni sawa na kusema ahudhurie mafunzo na kufuata taratibu zote zilizopo.
Kama mtu haonekani au mahudhurio yake siyo mazuri, hawezi kunufaika.
Mbili ni lazima mtu aweke kazi sana, hapa mtu anapaswa kutekeleza yale anayojifunza ili kupata matokeo. Kwa sababu matokeo hayawezi kuja kimiujiza, lazima kazi kubwa iwekwe.
Tatu ni kusikiliza, hapa mtu anapaswa kuweka ujuaji pembeni na kusikiliza kile anachoelekezwa na kukifanyia kazi. Bila usikivu mtu hawezi kunufaika na huduma ya ukocha.
Kwenye uhalisia, nimekuwa naona jinsi watu wanavyoenenda na mambo hayo matatu na kudumu kwenye huduma na mara zote imekuwa ikileta matokeo ya uhakika.
Wengi wanapoanza huduma wanakuwa wanatekeleza mambo yote matatu, hata kama hawajaambiwa.
Wanaonekana mara zote kwa kushiriki mambo yote yanayohusu mafunzo.
Wanaweka kazi kubwa kwa kufanyia kazi yote wanayojifunza.
Na wanakuwa na usikivu, wakielekezwa cha kufanya wanakifanya.
Hayo matatu yanawawezesha watu kupiga hatua kubwa sana kuliko ambavyo wamewahi kupiga kwenye maisha yao.
Na baada ya mtu kupiga hatua na kupata mafanikio kiasi, ndipo mambo huanza kubadilika.
Kwa ambao wanaendelea na mambo hayo matatu bila kuacha, wanadumu kwenye huduma na kuendelea kupiga hatua kubwa sana.
Mafanikio yanaendelea kuwa makubwa kwao na huduma inazidi kuwa ya thamani.
Lakini hawa ni wachache sana.
Wengi wakishapata mafanikio kiasi, wanaanza kulega kwenye mambo hayo matatu ya msingi.
Wanaanza kutokuonekana, hawahudhurii mafunzo kama awali. Wanaweza kuwa na visingizio mbalimbali, lakini mafanikio wanayokuwa wamepata ni kama yanawatinga na wanaona mafunzo siyo muhimu tena kwao.
Wanapunguza kuweka kazi kwa kuona wameshavuka hatua ya kujituma sana. Kwa mafanikio wanayokuwa wamepata na kuwa na watu wanaowasaidia kwenye mambo mengi, wanajiona wameshavuka ngazi ya wao kuhangaika kuweka kazi. Hilo linapunguza kasi yao ya mafanikio.
Halafu sasa, wanaacha kusikiliza. Wanakuwa na ujuaji mwingi. Baada ya kupiga hatua fulani, wanaona mafunzo ni ya chini kwao kwa hatua ambazo wamepiga. Wengine kwa kuona wameshafanikiwa kifedha kuliko Kocha, wanaona hana tena cha kuwaambia.
Mara zote, wale ambao hawazingatii mambo makuu matatu, huwa hawadumu kwenye huduma kwa muda mrefu.
Wengi hupotea. Na kwenye upotevu huo kuna ambao huweza kuendeleza mafanikio waliyoyapata. Lakini wengi huyapoteza mafanikio hayo.
Na pale wanapoanguka na kurudi tena, hawawi kama walivyokuwa awali.
Nimekuwa naona hili kwa muda mrefu na nimekuwa najidanganya mwenyewe kwa kuwapa watu muda nikidhani wataweza kubadilika.
Lakini hali imekuwa inaenda hivyo. Wanaozingatia yote matatu wanadumu na wasiozingatia hata moja tu wanapotea.
Baada ya kupingana na asili kwa muda mrefu bila ya mafanikio, nimeamua kukubaliana nayo.
Hivyo basi, nitafanya kazi na mtu pale tu atakapotekeleza mambo hayo matatu; KUONEKANA, KUWEKA KAZI na KUSIKILIZA.
Pale mtu anapoacha hata kimoja tu, hapo hapo naacha mara moja kufanya naye kazi.
Sitapoteza muda zaidi kusubiri mtu abadilike.
Ni anazingatia mambo yote matatu na kuwepo au anayaacha na kuondoka.
Hili halina ugumu wowote, ni unaonekana kwa kuhudhuria mafunzo yote, unaweka kazi kwa kutekeleza unauojifunza na kusikiliza kwa kuacha ujuaji.
Anayetaka hasa anafanya bila kuchoka.
Asiyetaka hatafanya, hata iweje.
Je wewe upo tayari kuzingatia hayo matatu, mara zote bila kuacha?
Shirikisha kwenye maoni hapo chini.
#NidhamuUadilifuKujituma
#AfyaUtajiriHekima
#KaziUpendoHuduma
#UpekeeUdadisiUbunifu
#UshirikianoUtegemeanoUwajibikaji
#BilioneaMafunzoni
#NajengaBiashara
#HakunaKingineMuhimu
#LazimaNitoboe
#NawekaKaziNifanikiwe
Matokeo makubwa hayawezi kuja kimiujiza,lazima kazi kubwa iwekwe,
LikeLike
Ndiyo.
Zingatia hayo matatu mara zote na kwa uhakika.
LikeLike
Kuonekana, kuweka kazi na kusikiliza nitayazingatia bila kuacha kwa sababu nimegundua kwa kuchelewa kwamba kupuuzia hayo kumenichelewesha na kutaendelea kunichelewesha sana kama nitaendelea kutozingatia.
LikeLike
Vizuri sana,
Yazingatie haya mara zote, yataleta matokeo mazuri sana.
LikeLike
Onekana,
Weka kazi na
Usikivu.
Nitazingatia 🙏🙏🙏
LikeLike
Vizuri
LikeLike
KUONEKANA, KUWEKA KAZI na KUSIKILIZA.
Haya nimejitahidi Sana kuyatekeleza. Na sababu ni rahisi, nimechagua kujifunza katika kila siku ya maisha yangu nikiwa hai. Nitaboresha katika maeneo kadhaa ya kimchakato. Kila siku ni siku ya kuweka KAZI Zaidi.
LikeLike
Ndiyo, unajitahidi sana KUONEKANA.
Na ndiyo, unakazana sana kuweka KAZI.
Lakini HUSIKILIZI na hilo ndiyo litakuangusha vibaya sana.
Kwa sababu wengi walipita njia unayopita sasa na matokeo yao hayakuwa mazuri.
Kila la kheri.
LikeLike
Anayetaka hasa anafanya bila kuchoka.
Asiyetaka hatafanya, hata iweje.
Mimi Nitaonekana, nitaweka kazi na ntasikiliza bila kuacha mpk nitoboe
LikeLike
Vizuri, kaa humo.
LikeLike
Nipo tayari kuzingatia mara zote bila kuacha
LikeLike
Vizuri, zingatia.
LikeLike
Ili kuendelea kupata matokeo makubwa ni kuendelea kuonekana kuweka kazi na kusikiliza
Asante
LikeLike
Vizuri, fanya hivyo.
LikeLike
KUONEKANA+KUWEKA KAZI+KUSIKILIZA
Hayo nitayafanyia kazi kwa sababu ni mchezo nilioamua kuucheza na una USHINDI ndani yake.
Asante
LikeLike
Vizuri sana, kaa humo.
LikeLike
Kuonekana
Kuweka kazi na kusikiliza. Asante Kocha Dr Makirita Amani kwa mafundisho mazuri.
LikeLike
Karibu
LikeLike
Nitazingatia haya kikamilifu
LikeLike
Vizuri
LikeLike
Kuonekana kuweka kazi na kusikiliza nitahakikisha ninafanya hivyo siku zote.💪
LikeLike
Vizuri
LikeLike
Ni kweli hata kwenye team zetu utaona tu anayetaka anafanya bila kusukumwa sana mimi nitafanya ,nitasikiliza na nitaonekana bila kuacha nitaweka kazi zaidi
LikeLike
Vizuri
LikeLike
naweka kazi,kusikiliza na kuonekana
LikeLike
Unakwama sana kwenye kusikiliza.
Ukiweza kusikiliza, utafanya makubwa sana.
LikeLike
Nitaonekana, nitasikiliza na kuweka kazi katika huduma ya ukocha.
LikeLike
Vizuri
LikeLike
Kwa kuzingatia haya matatu,Kuonekana,kuweka kazi na kusikiliza nitafanikiwa malengo yangu.
LikeLike
Vizuri
LikeLike
Nitaonekana,nitasikiliza na kuweka kazi
LikeLike
Vizuri
LikeLike
Napenda sana kujifunza nitajitahidi haya mambo matatu niyafanyie KAZI nitaoneka,na kusikiliza,pia nitaweka kazi
LikeLike
Vizuri
LikeLike
Hii vitu vitatu ndio nguzo kuu ya mafanikio kutoka kwenye huduma ya ukocha, ukienda kinyume utabadirisha sana makocha lakini hutopata matokeo.
Shut up and Listen.
LikeLike
Kabisa.
LikeLike
Asante sana Kocha ni kweli kwenye haya tunajisahau na kubadilika ni jambo zuri kutukumbhsha haya nipo tayari kuzingatia mambo 3 kwa ukamilifu. ASANTE
LikeLike
Vizuri
LikeLike
KUONEKANA, KUWEKA KAZI na KUSIKILIZA.
Mimi nipo tayari kuzingatia hayo mambo matatu.
Nitahakikisha Ninaonekana, Ninaweka kazi na Kusikiliza.
Ahsante sana Kocha.
LikeLike
Onekana, unafeli sana kwenye kuonekana. Sababu zako zinakuwa nyingi.
LikeLike
KUONEKANA, KUWEKA KAZI NA KUSIKILIZA,
Sio mara zote nafanikisha haya , lakini naahidi kujirekebishsha na kuanzia utekelezaji, nitajitahidi kadri ya iwezo wangu
LikeLike
Kila la kheri.
LikeLike
Kuwepo,. Kusililiza pia kuweka kazi , hivyo vyote viko ndani ya uwezo wangu hivyo nitavitekeleza.
Asante Sana.
LikeLike
Vizuri.
LikeLike