‎Rafiki Yangu,

‎Kuna kitu cha ajabu mno kinatokea ndani ya kila binadamu

‎Watu wanahangaika, wanakimbia kila kona, wanatafuta msaada, wanatafuta bahati, wanatafuta maombi, wanatafuta connection, wanatafuta mtu wa kuwainua…

‎…lakini bado maisha yao yapo pale pale.

‎Wanaishia kujiuliza,
Mbona kila mahali ninapogusa hakufunguki?

Mbona wengine wanapiga hatua fasta, mimi bado niko pale pale?

Au mimi nimezaliwa bila uwezo?

‎Lakini ukweli haujawahi kubadilika…
‎ustawi wa mtu hauji kutokea nje,
‎unatoka ndani.

‎Hujengewi unachomolewa kutoka ndani yako mwenyewe.

‎Ila tatizo kubwa ni hili…
‎Watu wengi hawajawahi kujitambua, kujisoma, au kujiwekea utaratibu wa ndani.

‎Wanatembea na hazina,
‎lakini hawajui namna ya kuifungua.

‎Kama simu imejaa apps nzuri,
‎lakini huna password,
‎hautafanya chochote nayo.

‎Hiyo ndiyo hali ya wengi wana uwezo,
‎lakini hawajaufikia kwa sababu haufunguki kwa nje, unafunguliwa kutoka ndani.

‎Sasa hapa ndipo maumivu yanazaliwa.
‎Unajiona unakwama,
‎na kuanza kuamini labda kuna kitu kinakuwekea vizuizi.

‎Unaona wengine wanafanikiwa haraka,
‎unaamini labda wao ndio walichaguliwa.

‎Unajisemea,
Labda mimi siyo mtu wa mafanikio.
Labda bado muda wangu.
Labda Mungu hajanitazama.

‎Lakini ukweli unaouma,
‎ni kwamba haujaanza safari ya kujifungua kwa ndani.

‎Tatizo si dunia,
‎tatizo si watu,
‎tatizo si bahati,
‎tatizo ni mlango wa ndani haujafunguliwa …na hiyo funguo ipo mikononi mwako.

‎Na ndio maana unaweza kusikia mawaidha,
‎kusoma vitabu,
‎kuhudhuria semina,
‎kuomba usiku kucha,
‎lakini maisha yakabaki vile vile.

‎Si kwamba hakuna nguvu,
‎ila hakuna ufunguo wa ndani uliotumika.

‎Hakuna mtu aliyekuja duniani akiwa maskini kiakili,
‎hakuna aliyezaliwa duni,
‎hakuna aliyeumbwa bila nafasi.

‎Lakini kuna tofauti mbili:
‎Kuna wanaotafuta nje, na kuna wanaochimba ndani.

‎Wale wanaotafuta nje huhangaika.
‎Wale wanaochimba ndani huendelea,
‎hata kama hawana kitu mwanzo.

‎Kwamba hutapata ustawi kwa kutegemea msaada,
‎kwa kuomba kila wakati bila kuchukua hatua,
‎…kwa kutafuta mtu wa kukuinua kila siku,
‎hiyo ni mindset iliyokosewa.

‎Ukweli ni huu:
‎Ustawi ni uwezo uliojengwa ndani yako kwa uelewa, nidhamu, na mabadiliko ya tabia sio msaada wa nje.

‎Suluhisho halipo mbali.
‎Halihitaji safari.
‎Halihitaji cheti.
‎Halihitaji uungwe mkono kwanza.
‎Halihitaji ukubalike.
‎Halihitaji kuonekana.

‎Linahitaji uamuzi mmoja tu…
Naamua kujiendesha kutoka ndani.

‎Hapo ndipo…

‎Unabadilisha namna unavyofikiri

‎Unajenga nidhamu mpya

‎Unaweka malengo yanayotekelezeka

‎Unajifunza kutawala tamaa

‎Unajua nini cha kukubali, nini cha kuacha

‎Unatengeneza mfumo, sio matamanio


‎Ustawi hauwaki kwa miujiza,
‎unawaka kwa ufahamu na maamuzi ya kila siku.

‎Ni mchakato wa ndani inayojengwa kimyakimya,
‎lakini matokeo yake yanaonekana nje hadharani.

‎Kuna jamaa mmoja nilimfahamu,
‎alikuwa na malalamiko kila siku.
‎Alikuwa anasema,
Bahati yangu bado haijafika.

‎Alikuwa anaanza miradi mingi,
‎lakini hakuna iliyoishi miezi miwili.
‎Si kwa sababu alikuwa hafai,
‎hapana.

‎Alikuwa hana mfumo wa ndani.

‎Siku moja nikamwambia,
Bro, acha kunung’unika. ‎Jijenge ndani kwanza, ‎usipange mafanikio yako kwa kelele, ‎panga tabia zako kimya kimya.

‎Baada ya miezi kadhaa,
‎hakuwa yule wa zamani.
‎Hakuongea sana,
‎hakujitangaza,
‎lakini mfumo wake wa ndani ulianza kunukia.

‎Mapato yakabadilika.
‎Mahusiano yakatulia.
‎Maono yake yakapanuka.

‎Leo ananiambia,
Nimegundua siku zote nilikuwa na uwezo, ‎nilikosa ufunguo tu.

‎Ustawi wako hauko mjini.
‎Hauko kwa watu.
‎Hauko kwa bahati.
‎Uko ndani yako.
‎Na unapochimba,
‎unauona.

‎Kujifunza zaidi soma kitabu kipya cha
FALSAFA YA USTOA – Jitawale Mwenyewe, Uitawale Dunia.

‎Kwa sababu mafanikio hayafunguki kwa dua tu,
‎yanachomolewa na ufahamu wa ndani.

‎Kukipata anzia hapa 👇

https://wa.link/524kl0

‎Karibu.
‎0756694090.