Habari za asubuhi ya leo rafiki yangu?
Hongera kwa siku hii nyingine nzuri sana ya leo.
Ni nafasi ya kipekee kwetu kwenda kuweka juhudi kubwa ili kuweza kupata matokeo bora sana.


Msingi wetu ni NIDHAMU, UADILIFU NA KUJITUMA ambapo tunakwenda kufanya makubwa leo na kila siku.

Asubuhi ya leo tutafakari kuhusu BORA KUKOSEA…
Kwenye maisha, yapo mambo mengi ambayo tunapaswa kuyafanya ili kuweza kupiga hatua na kufanikiwa.
Lakini pia yanakuwa ni mambo mapya, ambayo hatujazoea kuyafanya.
Na hivyo wengi huhofia kufanya, kwa kuogopa kukosea.
Wanaendelea kufanya kile walichozoea kufanya, mpaka pale wanapojikuta wameshaachwa nyuma.

Ili uweze kuzitumia vizuri fursa zinazokuzunguka,
Ili uweze kupiga hatua,
Il uweze kufanya makubwa na kufanikiwa,
Lazima uwe tayari kukosea.
Ndiyo, lazima ukosee kwenye mambo unayojaribu.
Ni katika kukosea ndipo tunapata nafasi nzuri ya kujifunza na kuwa bora zaidi.
Unapokosea, hutabaki pale ulipo sasa, bali utakuwa umejifunza njia gani siyo sahihi kufanya.
Wakati mwingine utahitaji kukosea mara nyingi mno, ili kuweza kujifunza vitu vingi.
Wakati mwingine unapaswa kujifunza kupitia makosa y wengine.
Kwa vyovyote vile, kuwa tayari kukosea, kuwa tayari kupoteza.

Ni vitu vichache sana kwenye maisha ambavyo ukikosea utakufa,
Vingine vingi, hasa kweye kazi na biashara, mambo ya taken days vizuri tu. Nanutajifunza mengi mno kupitia kukosea kwako.
Lakini pia usifanye jambo la kijinga kabisa kwa sababu umejiruhusu kukosea, hutanufaika kwa chochote.

Nenda kakosee leo, utakuwa bora zaidi kuliko jana.
Uwe na siku njema sana ya leo.
Rafiki yako,
Kocha Makirita Amani,
MAFANIKIO NI HAKI YAKO YA KUZALIWA,
http://www.makirita.info