Moja ya changamoto kubwa inayowazuia wengi kupiga hatua kwenye maisha, ni kutokuwa na uhakika.

Mtu anataka kitu, lakini hana uhakika kama anakitaka kweli na kama atakipata. Hivyo anakuwa kama anabahatisha, anakuwa kama anajaribu.

Kwa kuwa hana uhakika, kwa kuwa anabahatisha, haweki juhudi zote anazoweza kuweka, na hivyo matokeo anayopata ni madogo.

Ulinzi

Kitu kimoja unachopaswa kuwa nacho kwenye maisha ni uhakika, unaposema unataka kitu fulani, kuwa na uhakika hicho ndiyo unachotaka na kuwa na uhakika kwamba utakipata.

Weka kila aina ya juhudi na hata mara moja usijiulize kama kweli utakipata, jua utakipata na unachohitaji kuweka ni juhudi tu.

SOMA; UKURASA WA 1002; Kujua Kila Kitu Na Kujifunza Kila Kitu…

Wakati mwingine watu wanashindwa kuwa na uhakika kwa sababu wanafikiria kama wanakosea basi kuwa na uhakika ni sumu.

Hata kama unakosea, hata kama hujui vizuri kile unachotaka, unapaswa kuwa na uhakika kwamba unakitaka na uwe na uhakika kwamba utakipata.

Hata kama unakosea, ukiwa na uhakika utajifunza kuliko kukosea huku huna uhakika, utakuwa umepoteza tu muda wako na usipate chochote unachotaka.

Kuwa na uhakika, kila wakati kwenye maisha yako, weka mipango ya nini unataka kisha weka kazi kuhakikisha unapata kile unachotaka. Isiwe wewe au yeyote akufanye uanze kuwa na wasiwasi juu ya kile unachotaka.

Kila la Kheri Rafiki Yangu.

Rafiki na Kocha wako,

Dr. Makirita Amani,

Kwa kupata vitabu vya biashara na mafanikio tembelea www.kisimachamaarifa.co.tz/vitabu

Kupata blog ya kitaalamu unayoweza kuitumia kutengeneza kipato tembelea www.mtaalamu.net/patablog