Hakuna anayepanga kuwa kawaida, bali wengi wanaishia kuwa kawaida kwa kutokupanga.
Kama huna mpango wa nani unataka kuwa, unaishia kuwa wa kawaida, utakuwaje kitu ambacho hukijui.
Kama huna mpango wa nini unataka kupata, unaishia kupata vitu vya kawaida, utapataje kitu ambacho hukijui.
Kama hupangi vitu vya tofauti, maana yake uko tayari kupokea vitu vya kawaida, hivyo usishangae pale unapopata hiyo kawaida, ndicho ulichotaka.
Kawaida ni madeni,
Kawaida ni msongo,
Kawaida ni kutokuridhika,
Kawaida ni kukosa matumaini,
Kweli unaweza kuchagua kuwa kawaida, wakati una kila unachohitaji ili kutokuwa kawaida?
Tafadhali usikubali kuwa kawaida, ni rahisi sana kuwa kawaida, wanaokuzunguka wako kawaida, na wanataka wewe pia uwe kawaida, pambana sana ili usiwe kawaida.
Huwezi kujisifu umeyaishi maisha yako kama umeishia kuwa kawaida, kupata matokeo ya kawaida.
Kila la Kheri Rafiki Yangu.
Rafiki na Kocha wako,
Dr. Makirita Amani,