“Those who are not grateful soon begin to complain of everything.” — Thomas Merton
Watu wanaolalamikia kila kitu kwenye maisha yao, ni watu ambao hawana shukrani.
Ukiwa mtu wa shukrani, kuna mambo mengi ya kushukuru kwenye maisha kuliko kulalamika.
Hata pale unapokutana na magumu, ukiwa mtu wa shukrani, hutakosa cha kushukuru kwenye magumu hayo uliyokutana nayo.
Unapokuwa mtu wa shukrani unatafuta uzuri kwenye kila hali unayopitia.
Na kwenye maisha, huwa tunapata kile tunachotafuta.
Ukitafuta cha kulaumu lazima utakipata.
Kadhalika ukitafuta cha kushukuru pia utakipata.
Kuwa mtu wa shukrani, shukuru kwa kila jambo na hilo litakupelekea wewe kuziona fursa nyingi na nzuri kwako.
Usiwe mtu wa kulalamika na kulaumu wakati wote,
Kuwa mtu wa shukrani na kwenye kila hali unayopitia utayaona mazuri na kuweza kunufaika zaidi.
#NidhamuUadilifuKujituma
#AfyaUtajiriHekima
#KaziUpendoHuduma
Ukurasa wa kusoma leo ni kuhusu kurudia rudia, soma hapa; http://www.kisimachamaarifa.co.tz/2020/11/23/2154
Rafiki yako anayekupenda sana,
Kocha Dr Makirita Amani.
Asante sana kocha,tuna vingi kuvifanya kufikia ndoto zetu za mafanikio,kuiishi malengo yetu,dira na msimamo utokao ndani yetu,kujua nini unaenda kufanya bila kuangalia nini unaenda kupata,kurudia rudia hadi kieleweke,kuacha kulalamikia kila kitu, kitu,kuwa mtu wa shukrani ili uweze kuyaona mazuri yaliyojificha ndani yetu.
LikeLike
Karibu Beatus.
LikeLike