
Watu wamekuwa wanatumia njia zisizo sahihi ili tu kupata matokeo wanayoyataka.
Wakiamini kilicho muhimu ni matokeo na siyo njia iliyoleta matokeo hayo. Wanaamini matokeo yakiwa mazuri basi njia itakuwa sahihi.
Lakini hilo siyo kweli, tumeona wengi wakianguka baada ya kupata matokeo waliyotaka kwa sababu njia walizotumia hazikuwa sahihi.
Hakikisha unaanza na njia sahihi na kukaa kwenye njia sahihi, matokeo utakayoyapata yatakuwa sahihi na kudumu kwa muda mrefu.
Matokeo hayahalalishi njia, kama njia siyo sahihi, matokeo hayawezi kuwa sahihi.
Ushindi wowote unaoutafuta kwenye maisha yako, tumia njia zilizo sahihi.
Ukurasa wa kusoma ni kuhusu tatizo la mawasiliano ya mbali, fungua; http://www.kisimachamaarifa.co.tz/2021/01/26/2219
#NidhamuUadilifuKujituma #AfyaUtajiriHekima #KaziUpendoHuduma
Asante sana kocha kwa tafakari, ni muhimu kujenga msingi sahihi wa tabia zetu,uimara wa nyumba hutegemea msingi wake,sio kukimbizana na kila fursa na kuona umeachwa nyuma,ni kujifunza na kuchukua kila hatua sahihi,kila mara huwa naukumbuka mfano wako huu,’fursa ni sawa na kusafiri wa daladala,ipo itakuja imejaa itapita,ipo itakuja ina nafasi utapanda,tuchangamkie fursa ila tusikurupukie,tujifunze na kuelewa.
LikeLike
Karibu Beatus.
LikeLike