2960; Usiwauzie, wafundishe.
Rafiki yangu mpendwa,
Mauzo yanakuwa magumu kwa wengi kwa sababu wamekuwa wakikazana kuwalazimisha watu kununua.
Wanachosahau watu hao ni kwamba hakuna mteja anayependa kuona amelazimishwa kununua.
Kuuza ni kufundisha na kufundisha ni kuuza.
Wauzaji ambao wamekuwa wanaweka mbele kipaumbele cha kufundisha badala ya kuuza, wamekuwa wanaingiza kipato kikubwa sana.
Wafundishe wateja wako jinsi ambavyo unachouza kina manufaa kwao. Wajengee picha ya kitaswira kwenye akili zao ambayo wanajiona kabisa wakiwa na matokeo tofauti kwa kutumia unachouza.
Wafundishe wateja wako juhudi kubwa mnazoweka ili kuhakikisha wanapata kile ambacho wanaahidiwa. Wateja wanaweza wasielewe ni kazi kubwa kiasi gani inayowekwa kwenye kile wanachonunua na hivyo kutokukipa uzito mkubwa.
Lakini kwa kuwafundisha wanaelewa vizuri na wanajenga uaminifu mkubwa kwenye biashara.
Wakati mwingine wateja wanaweza kuwa tayari kulipa zaidi pale wanapojua nini hasa kinachofanyika kwenye kile wanachonunua.
Kama mteja hajawa tayari kununua kwako, jiulize ni kitu gani ambacho bado hujawafundisha na wakaelewa. Ukishajua hilo, unaweza kuboresha zaidi mchakato wako mzima wa mauzo, kwa kuhakikisha watu wanapata elimu sahihi itakayowasaidia kufanya maamuzi.
Mteja aliyeelimika ni mteja mzuri sana kununua, anakuwa mwaminifu na balozi mzuri wa biashara yako.
Ni wajibu wako kibiashara kuwaelimisha wateja wako wote kuhusu biashara yako na manufaa wanayokwenda kupata kwa kununua kwako.
Kuna mambo mengi kuhusu biashara zetu ambayo tunayachukulia poa kwa sababu tayari tumeshayazoea.
Lakini kwa upande wa wateja hawaoni kile tunachoona na mengi hawana uelewa sahihi kuhusu biashara yako.
Unapojenga msimamo wa kufundisha na kuonyesha, unajenga imani kwa wengi zaidi.
Ni kitu gani kikubwa unachowafundisha wateja wako ili washawishike kununua kwako?
Ni kwa namna gani wateja wanaona tofauti wakinunua kwako wanapolinganisha na kununua kwa wengine?
Hayo ni maswali ya kujiuliza kila wakati na kujipa majibu sahihi, kama unataka kufanya mauzo makubwa.
Kumbuka, usiuze bali fundisha, usiseme bali onyesha.
#NidhamuUadilifuKujituma
#AfyaUtajiriHekima
#KaziUpendoHuduma
#UpekeeUdadisiUbunifu
#UshirikianoUtegemeanoUwajibikaji
#NajengaBiashara
#HakunaKingineMuhimu
#BilioneaMafunzoni
#LazimaNitoboe
#NawekaKaziNifanikiwe
Wateja wanahitaji kufundishwa zaidi na sio kulazimishwa kununua.
LikeLike
Nikweli kabisa kabla ya kununua wanahitaji kifundishwa
LikeLike
Asante sana Kocha, nimejifunza kitu muhimu sana. Kuuza ni kufundisha na kufundisha ni kuuza.
LikeLike
Sitauza bali nitafundisha
LikeLike
Ahsante sana Kocha kwa makala hii muhimu sana hasa kwenye biashara tunavyofanya sisi MK NUTRITION.
Katika kupambana na magonjwa yanayowafanya wanawake washindwe kupata ujauzito (uzazi), kiukweli huwa tunatumia muda mwingi katika kufundisha na baada ya hapo huwa tunatoa ushauli.
Yaani tunauza kupitia ushauli, hili la Kufundisha badala ya kuuza linasaidia sana na mtu ananunua kwa ghalama utakayomwambia maana ushampa uelewa anajua tayari shida yake nini.
💥🔥✅
LikeLike
Tuwafundishe wateja wetu manufaa ya kile tunachowauzia ili waendelee kununua kwetu na kuwa mabalozi wazuri wa biashara zetu.
LikeLike
Kufundisha mteja kunajenga kuaminika.
LikeLike
usiuze bali fundisha, usiseme bali onyesha.
LikeLike
Kuelimisha wateja kunasaidia kutengeza wateja wa uhakika
LikeLike
Nitajiuliza maswali hayo mawili kila siku na kujipa majibu sahihi ili niweze kufanya mauzo yangu kuwa makubwa zaidi.
LikeLike
Muuzaji ni mwalimu, nitafundisha wateja wangu kuhusu juhudi zinazowekwa Ili kuwapatia kilicho Bora, nitawaonesha jinsi Gani wanakwenda kunufaika Kwa kununua bidhaa ninayouza…
LikeLike
Shukran, nitàjitahid kufundsha kadr niwezavyo ili niuze Zaid
LikeLike
Asante sana, nitaendelea kujifunza zaidi kuhusu biashara yangu ili niweze kuwafundisha wateja wangu
LikeLike
Usikazane kuuza bali elezea ubora kwanza, usiongee sana maneno bali waoneshe wateja mifano na wajaribu.
LikeLike
Ni ukweli mtupu kwamba kufundisha wateja wako kunawajengea imani ambayo ni ngumu kuivunja.
LikeLike
Asante sana Kocha, nitaendelea kutoa elimu na ushauri kwa wateja wangu ili wawe wateja wazalendo kabisa. Be blessed Dr Amani Makirita
LikeLike
Kutoa elimu Kwa wateja ndivyo zawadi kubwa ya kuwapatia wateja wetu.
LikeLike
Kweli nguvu ya kufundisha ni kubwa sana na ifanya mteja akuone wewe kama mshauri
LikeLike
Ni kitu gani ninachowafundisha wateja ili washawishike kununua kwangu?
Hili ni swali ambalo nitakuwa najiuliza kila mara ninapokuwa katika mchakato wa mauzo
LikeLike
Nahitaji kuwafundisha wateja badala ya kukazana kuwauzia. Asante Sana kocha.
LikeLike
Ni kweli kuuza ni kufundisha na kufundisha ni kuuza thanks kocha
LikeLike
Tufundishe ili kuuza.
LikeLike
Nitawafundisha wateja wangu badala ya kuwauzia tu. Asante kocha
LikeLike
Kuuza ni kufundisha na kufundisha ni kuuza.
Ahsante sana Kocha.
LikeLike
Tufundishe kuuza na tuuze kufundisha.
LikeLike