2965; Siamini.
Rafiki yangu mpendwa,
Kumekuwa na sababu moja pendwa kwa watu wengi wanaoshindwa kufanya yale wanayopaswa kufanya.
Sababu hiyo ni; “SIna muda.”
Karibu kila mtu anatumia kauli hiyo kama sababu ya kushindwa kufanya makubwa.
Lakini niseme ukweli kabisa, mimi siamini kabisa kwamba hakuna muda.
Naamini bila ya shaka yoyote kwamba muda tayari upo.
Najua kwamba muda huwa haupatikani, bali unatengwa.
Kila mmoja wetu ana masaa 24 pekee kwa siku. Hakuna aliyeongezewa au kupunguziwa.
Hiyo ina maana kwamba iwe unafanya makubwa au madogo, muda wako wa siku ni ule ule.
Siiamini sababu ya sina muda kwa sababu nina uhakika kila mtu kwenye siku yake kuna muda mwingi anaoupoteza.
Katika masaa 24 ya siku, kuna muda ambao mtu anapoteza kwa kufanya mambo yasiyokuwa na mchango kwenye mafanikio anayoyatafuta.
Mtu anasema kwa kujiamini kabisa kwamba hana muda.
Lakini mtu huyo huyo unamkuta akizurura kwenye mitandao ya kijamii na wakati mwingine akibishana mambo yasiyokuwa na tija kabisa.
Ujumbe wangu kwako leo ni wewe kuikataa sababu unayojipa ya kwamba huna muda.
Kila unapotoa sababu ya mambo yako kutokwenda vizuri ni kukosa muda, ifute haraka.
Jiambie wazi kwamba muda unao mwingi tu, ni jinsi ya kuupangilia ndiyo kunakupa changamoto.
Kwenye maisha na mafanikio, unaweza kuzalisha sababu au ukazalisha matokeo.
Kwa wengi, sababu ni rahisi kuzalisha, lakini chochote rahisi huwa hakina manufaa. Ni bora uwe mtu wa kuzalisha matokeo, ni njia ngumu, lakini yenye matokeo mazuri.
Kataa sababu unayojipa kwamba huna muda.
Dhibiti na pangilia vizuri muda ambao tayari unao.
Ndani ya masaa yako 24 una nguvu ya kufanya makubwa na yatakayoacha alama hapa duniani.
Muda unao, utumie vizuri.
#NidhamuUadilifuKujituma
#AfyaUtajiriHekima
#KaziUpendoHuduma
#UpekeeUdadisiUbunifu
#UshirikianoUtegemeanoUwajibikaji
#NajengaBiashara
#HakunaKingineMuhimu
#BilioneaMafunzoni
#LazimaNitoboe
#NawekaKaziNifanikiwe
Kwenye maisha na mafanikio, unaweza kuzalisha sababu au ukazalisha matokeo.
LikeLike
Tuchague kuzalisha matokeo, maana nguvu ni zile zile.
LikeLike
Asante sana ni sahihi muda ni Mwingi na matokeo ni muhimu sana
LikeLike
Tuzalishe matokeo.
LikeLike
Upo sahihi sana kocha na Asante sana ni sahihi muda ni Mwingi na matokeo ni muhimu sana
LikeLike
Muda tunao mwingi mpaka tumeamua kuupoteza.
LikeLike
Asili ya binadamu kutothamini kitu kinapokuwa kinapatikana kwa wingi.
LikeLike
Ni kweli muda unatosha! tunachokosea ni kushindwa kuwa na vipaumbele vya kufanyia kazi, ndio maana wengi tumekuwa tukilalamika kuwa muda hautoshi.
LikeLike
Tunaona hautoshi kwa sababu umekuwa mwingi kiasi kwamba tunafanya kila kitu ni kipaumbele.
LikeLike
Asante Sana kocha.
Rai yako ninakubaliana nayo, kwamba nikatae sababu
zote ninazojipa kwamba muda hautoshi.
Muda upo mwingi Sana ni Mimi kutenga na kuipangilia
Majukumu yangu na kuweka vipaumbele. Asante sana
LikeLike
Tutenge na kulinda muda.
Tayari tunao wa kutosha.
LikeLike
Asante sana
Muda ni uleule masaa 24 cha msingi ni kuwa na nidhamu na vipaumbele vyetu hasa vinavyo changia mafanikio yetu.
LikeLike
Hata tulalamikeje muda hautaongezeka hata dakika moja.
Tupangilie muda tulionao vizuri, unatosha kabisa kwa yale yaliyo muhimu.
LikeLike
Muda ni changamoto haujawahi kunitosha halafu saa yangu inakimbia kwa kasi sana.
LikeLike
Kinachokusumbua siyo muda, bali vipaumbele vyako.
LikeLike
Muda ninao mwingi , Ukweli ni kwamba naaribu muda huo kwa mambo yasiyo na tija!
LikeLike
Kabisa,
Ni mahali pazuri kuanzia kwa kujua muda tayari upo mwingi.
LikeLike
Muda tunao wakutosha ila hatuna vipaumbele
Asante
LikeLike
Tuanze na vipaumbele na tutaona jinsi muda ulivyo mwingi.
LikeLike
Si kweli kwamba muda ni mchache wa kufanya mambo muhimu kwani muda huwa unatengenezwa.
Kwenye maisha ya Mafanikio amua kuzalisha matokeo na sio sababu.
Asante
LikeLike
Tutenge muda kwa mambo yaliyo muhimu.
Mengine yasitupe usumbufu.
LikeLike
Hakika muda upo ni mimi nashindwa kuupangilia vizuri. Asante kocha
LikeLike
Tupangilie muda vizuri na mengine yatakaa sawa.
LikeLike
Muda ni maisha. Kilakitu kina muda na hukuna muda usiotosha. Kila mtu hana muda na kila mtu ana muda kwa yaliyo ya muhimu kwake. Hapa mtego ni vipaumbele
LikeLike
Kabisa tusipoweza kutatua la vipaumbele, muda utaendelea kuwa kitendawili.
LikeLike
Asante kocha,kwa ujumla watu wengi tunaona mda ndo njia ya kisingizio cha kujifichia.hivyo inabidi tutambue kuwa tajiri na masikini tuna mda sawa wa masaa 24 kila mtu.inabidi kujua kusudi lako ili uweke vipaumbele na kuvifanyia kazi.
LikeLike
Tusitafute pa kujificha, tuweke vipaumbele vyetu vizuri ili muda uweze kuwa wa kutosha.
LikeLike
Muda sote tunao sawa hakuna aliyepunjwa. Swali ni tunautengaje muda wetu?!
LikeLike
Kweli
LikeLike
Kinachotakiwa ni kuzalisha matokeo, siyo sababu.
Ahsante Kocha.
LikeLike
Sababu hazijawahi kumpa mtu yeyote mafanikio.
Tuziepuke.
LikeLike
Asante kocha kweli muda upo kazi kwetu kufanyaa makubwa kwenye muda huo ,tusipendi kuleta sababu
LikeLike
Kabisa.
Tatizo siyo muda, bali matumizi yetu.
LikeLike
Ni kweli kocha muda ndiyo kila kitu
LikeLike
Tuuthamini sana muda.
LikeLike