2977; Furahia kushindwa.
Rafiki yangu mpendwa,
Kwenye safari ya mafanikio ambayo tupo, hakuna kitu kizuri ambacho kila mmoja anakitaka kama ushindi.
Tunapenda sana ushindi, uwe ni mdogo mdogo au mkubwa, kwa sababu ni kiashiria kizuri kwamba tunaelekea kule tunakotaka kufika.
Japokuwa kushinda kunaleta hali ya kujisikia vizuri wakati huo wa ushindi, huwa pia kunaleta hali ya mazoea, kujiamini kupitiliza na kudumaa.
Ushindi unaleta mazoea kwa sababu mtu anaendelea kurudia yale yale yaliyompa ushindi, kitu kinachokuja kumpa anguko kubwa.
Kujiamini kupitiliza kunakotokana na ushindi ni pale mtu anapoona kwa kuwa amepata ushindi kwenye jambo moja, basi anaweza kupata ushindi kwenye kila jambo. Hiyo hupelekea kujaribu vitu ambavyo vipo nje ya uwezo wao na kupata anguko.
Ushindi pia unaleta kudumaa, kwani mtu anaposhinda anaona tayari anajua kila kitu na hahitaji tena kujifunza wala kujaribu vitu vipya. Ni udumavu huo ndiyo unaopelekea anguko kubwa la baadaye.
Upande wa pili wa kushinda ni kushindwa.
Hakuna anayependa kushindwa, kwa sababu huwa kunaonekana ni kiashiria cha uvivu, uzembe na ujinga.
Lakini kushindwa kuna faida zake, ambazo ni ustahimilivu, unyenyekevu na mabadiliko.
Kushindwa kunamjengea mtu ustahimilivu wa kuvuka magumu anayokutana nayo ili aweze kupata anachotaka. Anayeshindwa anakuwa imara zaidi kuliko anayeshinda.
Unyenyekevu ni zao jingine muhimu la kushindwa, ambapo watu wanakumbushwa kwamba pamoja na jitihada unazoweza kuweka, bado kuna mambo nje ya uwezo wako yanaweza kuathiri ushindi wako. Unyenyekevu unakufanya uweze kujifunza na kuendelea kuwa bora.
Kushindwa pia kunaleta hali ya mabadiliko. Kwa kufanya kitu kwa namna fulani na hatimaye ukashindwa, inakulazimu kuangalia nini kimesababisha ushindwe na hapo kubadili baadhi ya vitu ili kuweza kupata ushindi baadaye.
Kushindwa pia ni kiashiria kwamba unajaribu vitu vipya na vikubwa. Maana kama unapata ushindi kila mara, ni dhahiri unafanya vitu vidogo na vya kawaida.
Furahia kushindwa, jiwekee malengo na mipango mikubwa ambayo unaweza kushindwa na hilo litakupa funzo kubwa.
Na pale unaposhinda, haraka sana weka malengo mengine makubwa zaidi badala ya kubaki kwenye ushindi huo ambao utakufanya uwe mzembe.
Tunapenda sana ushindi, lakini kwa bahati mbaya sana hakuna tunachojifunza kwenye ushindi, zaidi ya kujenga uzembe.
Tufurahie kushindwa, maana ndipo penye somo kubwa sana kwetu.
Ni kushindwa ndipo panatusukuma tuwe bora zaidi ya tulivyokuwa.
Unaposhinda usiridhike na kujipa usingizi mnono, badala yake badili lengo liwe kubwa zaidi ili likusukume na kukunyima usingizi.
Nimalizie kwa usemi huu maarufu sana ambao huwa unasema nyakati ngumu huwa zinatengeneza watu imara, watu hao imara wanatengeneza nyakati rahisi, nyakati hizo rahisi zinatengeneza watu dhaifu na watu hao dhaifu wanatengeneza nyakati ngumu.
Ushindi mfululizo ni laana, siyo baraka. Inahitaji mtu uweze kupuuza sana ushindi ndiyo uweze kufanya makubwa kwenye maisha yako.
#NidhamuUadilifuKujituma
#AfyaUtajiriHekima
#KaziUpendoHuduma
#UpekeeUdadisiUbunifu
#UshirikianoUtegemeanoUwajibikaji
#NajengaBiashara
#HakunaKingineMuhimu
#BilioneaMafunzoni
#LazimaNitoboe
#NawekaKaziNifanikiwe
Kushindwa kunatusaidia kukaa nyikani na kujitafakari na kisha kuja tukiwa wapya.
Kushindwa ni mchakato wa kuwa bora ZAIDI.
Asante sana Kocha Dr Makirita Amani.
LikeLike
Ni kweli kabisa kuwa wakati mwingine ushindi unakuwa kukwazo sana kwetu.
LikeLike
Hilo liko wazi kweli kocha kuna wakati tunabweteka na kaushindi kumbe ni ajili ya kalengo kadogo na kutengeneza nyakati mbaya mbele ajili ya watu kuridhika na kaushindi mwishowe tunafeli na kushtuka tena ahsante sana kocha
LikeLike
Unyenyekevu ni zao jingine muhimu la kushindwa. Asante sana Kocha Dr. Makirita Amani
LikeLike
Ni kweli ushindi unaduma akili tuwe makini nao.
LikeLike
Unadumaza akili.
LikeLike
Ushindi mfululizo ni ulevi
LikeLike
Ushindi mfululizo ni laana, inahitaji ustahimilivu mkubwa wa kuupuuza ushindi ili uweze kufanya makubwa.
LikeLike
Duh ni kweli ukifikia lengo Kila mara unabweteka.
Ahsante sana Kocha
LikeLike
Napuuza ushindi unaoleta kulemaa, nafurahia kushindwa maana ni funzo kubwa kwangu.
Mara zote naweka lengo kubwa zaidi Ili na lakunitisha, sitaogopa kushindwa maana ni kujifunza.
Sikubali kuwa mtu dhaifu na kutengeneza nyakati ngumu.
LikeLike
Kushindwa kunaibua swali moja muhimu sana la kujiuliza kila wakati ” KWA NINI?” …..”WHY?”
LikeLike
Ni wazi ushindi unajenga kujiamini pia kushindwa unaweza kudhani ni uzembe, uvivu na ujinga . Lakini sio
Kweli kwamba kushindwa ni uzembe, ujinga na nk.
Pia sio kweli kwa kushindwa Jambo moja basi utashinda
kila Jambo, KUMBUKA Kuna Mambo ambayo yako nje ya uwezo wako.
Furahia kushindwa , kushindwa kunakuimalisha, kunakujengea ustahamilivu, pia kunakupa mbinu mpya,
(SHUKLANI ZA DHATI KOCHA ) ni Somo fupi lakini KALI MNO.
LikeLike
MAONI YA JUU NI KWA ( kwa kushinda Jambo moja sio kwamba utashinda kila Jambo)
LikeLike
ahsante kocha.
LikeLike
Anayeishindwa anaimarika zaidi,Nyakati ngumu huwa zinatengeneza watu imara, naimani haya yote yangu japo mapambano ya mafanikio ktk maisha ni vita isiyoisha
LikeLike
Asante,,,mazoea yanamfanya mtu atatue tatizo kwa mbinu alizo zoea na hiyo mazoea ndiyo huleta anguko kubwa.
LikeLike
Asante kocha,kwa makala hii kweli ukilewa ushindi uwezi kuwa imara na ukishindwa ndo unaimarika zaidi.
LikeLike
Nyakati ngumu huwa zinatengeneza watu imara, watu hao imara wanatengeneza nyakati rahisi, nyakati hizo rahisi zinatengeneza watu dhaifu na watu hao dhaifu wanatengeneza nyakati ngumu.
Ahsante sana Kocha.
LikeLike
Kushindwa kunakupa wewe nafasi ya kufanya vizuri zaidi
Asante
LikeLike
Ushindi mfululizo ni laana, siyo baraka. Inahitaji mtu uweze kupuuza sana ushindi ndiyo uweze kufanya makubwa. Asante Kocha.
LikeLike
Duh! Kumbe Ushindi mfululizo ni uchuro,inahitaji mtu kujielewa sana ili tusiridhike. Asante sana Kocha.
LikeLike
Ushindi mfululizo ni laana, siyo baraka. Inahitaji mtu uweze kupuuza sana ushindi ndiyo uweze kufanya makubwa kwenye maisha yako.
LikeLike
Nyakati ngumu zinanipa nafasi ya kutafakari na kijifunza,nyakati ngumu zinanifanya niwe mtu imara na kuona namna sahihi ya kufanya vitu.
Asante kocha.
LikeLike