2991; Tutashinda.
Rafiki yangu mpendwa,
Kwenye hii safari ya ubilionea, ni lazima tupate ushindi.
Na hilo litawezekana kama tu tutaufanya mchakato wa safari hii kuwa kipaumbele cha kwanza kwenye maisha yetu.
Safari yenyewe siyo rahisi, lakini kwa kuifanya kuwa kipaumbele cha kwanza, tunajiweka kwenye nafasi ya kushinda.
Kuna mambo mengi yanayotaka muda, nguvu na umakini wetu. Mengi yataonekana kuwa muhimu sana.
Kama tutayapa mambo hayo kipaumbele kuliko mchakato wetu, tayari tunakuwa tumekubali kushindwa.
Tunajipa uhakika wa kushinda kwa sababu tunatimiza vigezo vikubwa vitatu kwenye huu mchakato.
Kwanza kabisa tumejitoa moja kwa moja kwenye huu mchakato. Ndiyo kipaumbele namba moja kwetu na hatutauacha hata iweje. Hata tukutane na magumu kiasi gani, hatutaacha huu mchakato kwa sababu tumejitoa kweli kweli, hatuna mbadala mwingine.
Hebu fikiria, utakosaje ushindi kama huna mbadala? Ni lazima ushinde au ufe ukiwa unapambana, kitu ambacho ni ushindi pia.
Mbili ni kuupenda kweli mchakato, kutoka ndani ya mioyo yetu.
Hatukai kwenye huu mchakato ili kuonekana, wala hatukai kwa kuigiza na kufuata mkumbo.
Bali tunakaa kwenye huu mchakato kwa sababu tunaupenda kweli kweli.
Ndiyo kitu pekee ambacho tupo tayari kuendelea kukifanya kwenye maisha yetu, bila kujali matokeo au tumefika ngazi gani.
Ushindi kwetu ni matokeo tu, lakini mchakato ni sehemu ya maisha yetu, ambapo tutaendelea nao kwa maisha yote, iwe tumeshinda au la.
Mchakato kwetu ni kama pumzi, ndiyo maana tunajiambia ushindi ni lazima.
Hakuna siku unasema umechoka kupumua na hivyo upumzimke.
Kama unatama kupumzika kwenye mchakato, umeshajiondoa kwenye ushindi.
Tatu ni uaminifu, hatufanyi tu kwa ajili yetu, bali tunafanya kutimiza ahadi yetu kwa wale tunaoambatana nao.
Tumekubaliana kusafiri pamoja kwenye hii safari, tunashirikiana kwa mambo mbalimbali, watu wamejitoa kwa ajili yetu, hivyo ni wajibu wetu pia kujitoa kwa ajili yao.
Hata pale unapoona wewe binafsi hutaki tena kukaa kwenye mchakato, hebu kuwa mwaminifu kwa wale waliokuamini na kukushirikisha mengi muhimu, hebu fanya kwa ajili yao.
Kwenye safari yetu tuna Kocha na pia tuna klabu zetu. Hata pale unapoona hutaki tena kufanya, hebu fanya kwa ajili ya Kocha na Klabu, hebu kumbuka jinsi watu hao wamewahi kujitoa kwa ajili yako na hebu tamani usiwaangushe.
Kwa kuwa mwaminifu kwa wale unaoambatana nao, unalazimika kufanya hata kama hutaki na hilo ndiyo linalokupa uhakika wa ushindi.
Kunaweza kuwa na sababu mbalimbali zinazotaka kukusababisha usikae kwenye mchakato, kama utazingatia hayo matatu, hutaipa sababu yoyote nguvu ya kukuzuia.
Na kama kuna sababu yoyote ile itakayoweza kukutoa kwenye mchakato, basi mchakato siyo kipaumbele cha kwanza kwako na hutaweza kupata ushindi.
Kukaa mguu mmoja nje na mguu mwingine ndani, kusikilizia kama kuna dalili za ushindi au la haitakusaidia. Utashindwa vibaya sana na utakuwa umepoteza muda, nguvu, umakini na maisha yako.
Ushindi unakutaka ujitoe mzima mzima, hata kama wakati mwingine hutaki, inakulazimu kufanya kwa ajili ya wengine, lakini mwisho wa siku unanufaika sana wewe.
Na kama kuna kitu kingine unachokipenda zaidi ya mchakato, kama unajiambia ukishashinda hutaendelea tena na mchakato, hutashinda. Yaani hilo lifakuwa kikwazo kikubwa mno kwako kupata ushindi unaoutaka.
Kama unauona mchakato mzima ni mateso, umeshashindwa kabla hata ya kuanza.
Kama unatafuta njia ya kuutoroka mchakato, umeshashindwa vibaya sana.
Kuna wengi wanajikuta kwenye huu mchakato kwa kufuata mkumbo, wakiwa hawajui ni kwa kiasi gani wanahitajika kujitoa kukaa kwenye huo mchakato.
Ushindi utakuwa ni wa uhakika kabisa kwako kama mchakato utakuwa kipaumbele cha kwanza kabisa kwako, utaupenda sana mchakato kutoka ndani yako na hata kama hujisikii kuendelea kukaa kwenye mchakato, unafanya kwa heshima ya wengine ulioambatana nao au kuwaahidi.
Nje ya nayo usijidanganye kwamba utaweza kupata ushindi.
Andika kwenye maoni hapo chini kwa nini wewe una uhakika kwamba utashinda.
#NidhamuUadilifuKujituma
#AfyaUtajiriHekima
#KaziUpendoHuduma
#UpekeeUdadisiUbunifu
#UshirikianoUtegemeanoUwajibikaji
#NajengaBiashara
#HakunaKingineMuhimu
#BilioneaMafunzoni
#LazimaNitoboe
#NawekaKaziNifanikiwe
Nina uhakika kwamba nitashinda kwa sababu ninakaa kwenye mchakato.Ni swala la muda tu mimi kufanikiwa.Kila mara nitaangalia namna kocha unavyokaa kwenye mchakato bila kuweka sababu yoyote na namna wenzangu kwenye klabu wanavyokusukuma na kunisukuma pia.
LikeLike
Nina uhakika nitashonda kwa sababu kadri ninavyoendelea kukaa kwenye mchakato kuna matokeo ninayoyaona na naendelelea kuukaribia ubilionea
LikeLike
👏
LikeLike
💪
LikeLike
Nitaendelea kukaa kwenye mchakato yawepo magumu au la bado nitasonga mbele na kuendelea kuufurahia mchakato.
LikeLike
👏
LikeLike
Mimi nina uhakika kuwa nitashinda kwasababu nimeamua kujitoa kukaa kwenye mchakato
LikeLike
🔥
LikeLike
Nina uhakika wa kushinda kwa sababu nimejitoa kweli kweli kwenye mchakato wa Bilionea Mafunzoni.
Na mchakato kwangu ni kama pumzi, nitaendelea kujisukuma Ili nisijiangushe Mimi mwenyewe hata wana Klabu na dunia kwa ujumla.
Asante sana
LikeLike
❤️
LikeLike
nitashinda kwa sababu sina mbadala mwingine.
do or die. ahsante
LikeLike
💯
LikeLike
Nina uhakika wa kushinda kwa sababu niakiamua Jambo nimeamua, sirudi nyuma
LikeLike
👏
LikeLike
Mm Naamini nitahsinda kwa sababu najua kile kilicho sahihi ni kigumu siyo rahisi, pia matokeo hayapo kwenye udhibiti wangu, kilicho kwenye udhibiti wangu ni kukaa kwenye mchakato. Pia kikubwa zaidi kwa kukaa kwenye mchakato ni najenga tabia ambayo mbali na kuninufaisha mimi binafsi itakwenda kuwanufaisha watotot wangu baadaye kwa kujifunza kwa matendo kutoka kwangu na siyo maneno. Na watu wengine kwenye jamii na nchi kwa ujumla.
LikeLike
🔥
LikeLike
Nina uhakika wa kushindwa kwasababu nakaa kwenye mchakato na nimezungukwa na watu sahihi ambao wanapenda kuona nafanikiwa
LikeLike
👏
LikeLike
Nitashinda kwa sababu, nimeambatana na watu wanaojisukuma Sana kufanya makubwa, watu ambao hawabweteki na Mafanikio kidogo waliyonayo, watu wenye maono makubwa, watu wanaojisukuma kufikiri kwa ukubwa Zaidi na kuacha kufanya kwa mazoea .Nimezungukwa na watu wenye Kiu kubwa ya kufanikiwa, kuanzia Kocha na wanaclub wenzangu, watu wenye mtazamo WA ukuaji na KUJIFUNZA, watu waliotayari kushirikisha hata mambo ambayo ni ya Ndani Zaidi ili Tu kuhakikisha tunakwenda pamoja. Siendeshwi na mazoea, nachukua hatua hata nje ya uzoefu binafsi..ninayohakika ya kushinda. Nimewahi kufanya biashara kadhaa zingine hazikuleta matokeo niliyoyatarajia lakini kukata Tamaa ni mwiko kwangu..mwaka huu nimepata kuomba Ushauri mara kadhaa kutoka kwa Wana club wenzangu…Mimi nakwenda kufanyia Kazi moja ya Ushauri niliopewa kutoka kwa mwanaclub Mwenzangu Jackson…nitafanya kama ishara ya kuwa Mimi siendeshwi na Yale tu niliyoyazoea(mazoea) Niko tayari kuchukua hatua mpya…zitanifanya kuwa imara na kunipa utofauti katika maisha yangu..pesa ni matokeo ambayo sio kikwazo kwangu iwe zitapotea zote…naamini kama katika mchakato nilizipata na pengine katika mchakato nikapoteza kila kitu hata mavazi ninachokiamini bila Shaka yoyote ni Kuwa ipo siku mchakato utazileta tena kwa utele Sana.
LikeLike
❤️
LikeLike
Mimi nina hakika kwamba nitashinda kwasababu nimejitoa kwenye mchakato kufa na kupona hakuna namna nyingine
LikeLike
👍
LikeLike
Mimi nitashishinda kwasababu nipo kwenye MCHAKATO sahihi na kikamilifu.
LikeLike
👍
LikeLike
Nina uhakika kuwa nitashinda kwa sababu kuu mbili:
Moja; Ninamheshimu sana Kocha Dr. Amani Makirita kutokana na nguvu kubwa anazoziweka kwetu sisi ili tuweze kufanikiwa, ni watu wachache sana kwenye ulimwengu huu wa kukushika mkono na kutaka kuona unapiga hatua.
Mbili; Naheshimu sana wale wanaonizunguka hasa wanaclub wenzangu kwa ushirikiano mkubwa uliyopo miongoni mwetu. Kwa kutafakari circle hii ya watu ninaoshirikiana nao kwa uwazi mkubwa basi najiona nina kila sababu ya kuendelea kukaa kwenye mchakato ili nisiwaangushe wale walioniamini. Hili linanipa uhakika kuwa nitashinda.
#Tutashinda!
LikeLike
❤️
LikeLike
Asante kocha,Imani yangu ni kubwa kuwa nitashinda kwa sababu tayari ninafahamu kusudi langu la maisha, hivyo ili nishinde lazima nikae kwenye mchakato hamna namna yoyote ile ya ushindi bila kukaa kwenye mchakato.
LikeLike
👏
LikeLike
Ushindi ni uhakika ndani ya mchakato, nitakaa kwenye mchakato kama nilivyoahidi tangu mwanzo.
LikeLike
👏
LikeLike
Mchakato kwangu ni pumzi. Ninaishi kwa kuwa Ninapumua. Mchakato kwangu ni maisha ambayo yanafaywa bora kila kukicha na Kocha na wana KCM ninaoambatana nao. Mchakato tayari ni ushindi.
LikeLike
💯
LikeLike
Mchakato ndio kupaombele cha kwanza kwenye maisha yangu.Kwenye mchakato lazima ushindi upatikane. Niwe kwènye mchakato au niwe nje ya mchakato, kubaki mguu nje ndani ni dallili za kushindwa
LikeLike
🔥
LikeLike
Ni uhakika nitashinda kwa sababu ya Focus kwenye kitu kimoja ninachoweza kukuhakikishia ambacho ni mchakato kamili. Pia malengo yangu yapo clear kabisa sijawahi kuyumba hata siku moja toka nilipo tambua kile ambacho ninakipenda zaidi
LikeLike
👏
LikeLike
Kwa hakika kabisa nitashida!
nitadumu katika mchakato si kwaajili yangu na ndoto zangu pekee, lakini pia kwa heshima ya wale niliyopo nao katika mchakato bila kuwaangusha.
LikeLike
👍
LikeLike
Nitashinda safari hii kwa sababu mchakato huu ndiyo unaonisukuma kuishi ndoto nilizonazo
Pili nimefanya mchakato huu kama sehemu ya maisha yangi. Nitaendelea kupumua.
Tatu Najisukuma kwa sababu kuna watu wameshawekeza muda wao kwangu ili mimi nifanikiwe. Kuna watu wananitegemea. Hivyo sitaki kuwaangusha
LikeLike
👏
LikeLike
Nina uhakika nitashinda,kwa sababu ushindi pekee ndiyo kitu nahitaji kwenye maisha yangu.
LikeLike
👍
LikeLike
Asante sana kocha kwa Makala hii.
Mimi lazima nishinde kwa sababu
1. Mchakato kwangu ni kipaumbele cha kwanza kabisa, 2. Napenda sana mchakato kutoka ndani yangu na hata kama sijisikii kuendelea kukaa kwenye mchakato na lazimika kukaaa kwenye mchakokato. 3. Nakuwa mwaminifu na kufanya kwa heshima ya wengine nilioambatana nao au kuwaahidi kwenye KCM, klabu na mabilionea wenzangu. Hivyo kufanikiwa ni lazima kwangu.
Asante
LikeLike
❤️
LikeLike
Mimi nina uhakika kuwa nitashinda kwa sababu;
Moja; nimejitoa moja kwa moja kwenye huu mchakato.
Mchakato ndiyo kipaumbele kikuu kwangu.
Mbili; naupenda kweli mchakato, kutoka ndani ya moyo wangu.
Tatu; nakuwa mwaminifu, natimiza ahadi zangu kwa wale tunaoambatana nao.
LikeLike
👍
LikeLike
Nina uhakika kabisa nitashinda mchezo huu kwa sababu nimezielewa kanuni za mchezo na kila siku naendelea kuzifanyia kazi bila kuacha, hata magumu yatokee sikati tamaa,, Nina kiu na ninachokitaka kweli nafanya hivi kwaajili yangu na dunia kwa ujumla..furaha yangu niwe bilionea.
LikeLike
👍
LikeLike
Asante sana Kocha, naamini kwenye ushindi kwa sababu nipo pahali sahihi,pahali ambapo watu wanapenda kujisukuma kufanya makubwa. Ninashinda kwa sababu nakaa kwenye mchakato sahihi na pia kwa sababu ya heshima ya watu wanaonizunguka kama Kocha na wanaklabu.
LikeLike
👏
LikeLike
Nitashinda kwa sababu jukumu langu ni kukaa kwenye mchakato na ushindi ni matokeo.
LikeLike
👏
LikeLike
Asante Kocha kwa Makala ya leo,
Ushindi utakuwa ni wa uhakika maana naweka mchakato kuwa kipaumbele cha kwanza kabisa kwangu.
Nitakuwa Mwaminifu na nitaupenda mchakato kutoka ndani yangu na kuendelea kukaa kwenye mchakato hata kama sijisikii kuendelea kwa Heshma ya Club yangu ya Arusha na Dangote na kwa ajili ya Kocha Amani Makirita
Tutashinda!
LikeLike
💯
LikeLike
Asante Kocha kwa makala murua ya leo
Nina uhakika kwamba nitashinda kwa sababu ninakaa kwenye mchakato wa Ubilionea. Ni Hira nice naupambania akuliko kutofanya kbsa au kukaa mguundani.
Ni swala la muda tu mimi kufanikiwa, naweka juhudi, maarifa na ubunifu pamoja nidhamu kwneye mchakato huu. Kila mara ninafata namna kocha anavyotaka mie niwe kwenye mchakato bila kuweka sababu yoyote. Wenzangu na familia ni kitu kinachonifanye nisiwe na mbadala kwenye mchakto. Ninasonga mbele kwa kuweka kipaumbele wenzangu wa kwenye klabu wanavyojisukuma na kunisukuma pia kufikia malengo.
Nitashida kwa uhakika.
LikeLike
👍
LikeLike
Nina uhakika nitaendelea kushinda kwa sababu kupitia mchakato tayari kuna mambo mengi nimeshinda. Hivyo nimethibitisha hakuna ushindi bila kukaa kwenye mchakato na kuzungukwa na watu sahihi.
LikeLike
🔥
LikeLike
Nitashinda tu na Nipo tayari kukaa kwenye mchakato….mchakato ni sehemu ya maisha yang hakuna kitakachonizuia kukaa kwenye mchakato
Asante
LikeLike
👏
LikeLike
Nina uhakika wa kushinda kwa sababu hizi hapa
1.nimeamua kujitoa pasipo kuwekewa kikwazo na mtu yeyote yule
2.nimehangaika na vitu vingi bila utaratibu na sasa nimeamua kukaa kwenye biashara hadi nipate ubilionea
3. Niko na kocha na staff yake
4.nitapokea mafunzo na maelekezo yote na kuyafanyia kazi
5.nitakua kwenye club hadi club ivunjike au kufutwa na kupokea ushauri wa mabilionea wenzangu
6.nitawaonyesha kuwa inawezekana hata kwa familia maskini kupata ubiliknea
LikeLike
🔥
LikeLike
Ninahakika nitafanikiwa kwa sababu mchakato ndio kipaumbele changu Cha kila siku.
LikeLike
👍
LikeLike
Ni ushindi tu pale nitakapokaa kwenye mchakato bila kujali matokeo ninayoona nahesabu ushindi wangu kila siku ndani ya mchakato
LikeLike
👏
LikeLike
Ninaamini huu ndiyo mchakato sahihi,kwa kua mambo mazuri hayaji kiupesi upesi.Ni mchakato unaoniweka kujisukuma na kuwajibika.Hata kama najisikia kukata tamaa nitafanya tuu kwa kua ninakuahidi locha na klabu
LikeLike
👍
LikeLike
god bless us.
LikeLike
👏
LikeLike
Nitashinda kwasababu najisukuma kukaa kwenye mchakato, najua ninapotaka kufika,ninapokwenda na njia ya kwenda…
Lazima nishinde.
LikeLike
Safi sana. Shinda.
LikeLike