2999; Mlango wa kutokea.
Rafiki yangu mpendwa,
Kazi ya kujenga timu ambayo ndiyo kipaumbele chetu kikubwa kwa sasa siyo kazi rahisi.
Ina changamoto za kila aina.
Kuna makosa madogo madogo ambayo ukiyafanya yanakuwa kikwazo kikubwa kwako kujenga timu bora.
Ili kuepuka makosa hayo kwenye kujenga timu, ni muhimu kuwa na hatua unazozifuata kwenye zoezi zima.
Zipo hatua tano muhimu za kufuata kwenye zoezi la kujenga timu ili kupunguza changamoto mbalimbali zinazojitokeza.
Hatua ya kwanza ni kuajiri kwa mchakato sahihi.
Hapa unapaswa kutangaza nafasi za kazi, kuwataka watu watume maombi na kuwafanyia usaili.
Kosa kubwa ambalo watu hufanya kwenye hatua hii ni kuajiri watu wa karibu wanaowajua, tena kwa kigezo kwamba hawana cha kufanya. Mwishowe wanakuja kupata matokeo mabaya, kwa sababu hao wasiokuwa na cha kufanya, hushindwa kufanya wanachopaswa kufanya.
Hatua ya pili ni kuwapa majukumu ya kazi wale ambao wameshinda kwenye usaili.
Hapa unapaswa kuwaambia kwa hakika nini wanapaswa kufanya na wanapimwaje kwenye ufanyaji.
Kila unayemwajiri ayaelewe majukumu yake vizuri na jinsi ya kuyatekeleza.
Hatua ya tatu ni kuwapa mafunzo ya kutekeleza majukumu yao.
Pamoja na kuwapa majukumu, bado kuna ambao yatakuwa magumu kwao kutekeleza.
Hivyo unapaswa kutoa mafunzo kwa wafanyakazi wako ya jinsi ya kutekeleza majukumu yao kwa viwango vya juu.
Hatua ya nne ni kupima matokeo ya yale wanayofanya na kuwasaidia namna ya kuboresha ili kupata matokeo bora zaidi.
Wapo wafanyakazi ambao pamoja na kuchukua hatua, bado matokeo watakayopata yanakuwa siyo mazuri.
Kwa kuwa wewe tayari una uzoefu kwenye biashara yako, wasaidie kwa kuwaelekeza namna ya kuboresha ufanyaji wao.
Hapa unaenda hatua ya ziada ya kuhakikisha huwapotezi watu ambao wanaweza kuwa bora.
Hatua ya tano ni kuwaonyesha mlango wa kutokea.
Kama utafuata hatua zote nne hapo juu, lakini bado mfanyakazi akashindwa kufanya kile anachopaswa kufanya, kuna hatua moja tu ya kuchukua, ambayo ni kumwonyesha mlango wa kutokea, yaani kumfukuza kazi.
Hii ndiyo hatua ngumu kabisa na ambayo wengi huikwepa.
Mwishowe wanabaki na watu wengi kwenye biashara, ambao hawana uzalishaji wala ufanisi wowote.
Watu hao wanaishia kuwa mzigo kwenye biashara, kitu kinachoigharimu sana biashara.
Kama umemwajiri mfanyakazi kwa mchakato sahihi.
Ukamweleza kwa kina majukumu anayopaswa kutekeleza.
Ukampa mafunzo ya namna ya kutekeleza majukumu yao.
Ukamfuatilia kwenye utendaji na kumsaidia kuboresha zaidi.
Lakini bado akawa anashindwa kutekeleza majukumu yake.
Hatua sahihi ni kumwondoa mfanyakazi huyo kwenye biashara.
Huwa kuna hali ya kuamua kuwaacha wafanyakazi wa aina hiyo kwa kuamini huenda watabadilika.
Lakini hicho huwa hakitokei, kadiri wanavyoendelea kubaki ndivyo wanavyofanya uharibifu mkubwa kwenye kazi na hata kwa wengine pia.
Inakuwa vigumu kuchukua hatua ya kuwaondoa wafanyakazi wasiofaa kama hukutumia mchakato sahihi kwenye kuwaajiri.
Kama uliajiri watu wa karibu ambao hawana cha kufanya, itakuwa vigumu kuwaondoa kwa sababu hawatakuwa na cha kwenda kufanya.
Utawaonea huruma wataenda wapi, lakini huruma haitakuwa na manufaa kibiashara.
Upo kwenye biashara kufikia maono makubwa uliyonayo.
Kila aliyepo kwenye biashara hiyo anapaswa kuwa na mchango kwenye kuyafikia hayo maono.
Ambaye hana mchango anapaswa kuonyeshwa mlango wa kutokea ili asiwe kikwazo cha kufikiwa kwa maono yaliyopo.
Kuwaondoa watu wasiofaa kwenye biashara, siyo tu manufaa kwa biashara husika, bali pia ni manufaa kwa watu wenyewe.
Hakuna kitu kinawaumiza na kuwadumaza watu kama kuwa kwenye kazi ambayo hawawezi kuifanya vizuri.
Wakati mwingine inakuwa ni kazi isiyoendana na vipaji vyao au uwezo walio nao.
Kwa kuendelea kukaa kwenye biashara hiyo wanakuwa wanapoteza muda, kwa sababu hakuna hatua zozote wanazopiga.
Kuwaondoa inawasaidia kwenda kufanya kile kilicho sahihi kwao.
Zoezi la kujenga timu ni mchakato endelevu ambapo kama hatua hizo muhimu zifafuatwa, tutaweza kujenga timu imara.
Ni zoezi linalohitaji muda na uvumilivu kwa sababu utawapitia wengi wasio sahihi kabla hujawafikia wachache sahihi.
Kadiri unavyokwenda na huo mchakato unajifunza baadhi ya tabia zinazokuwepo kwa wale wanaokuja kufanya vizuri.
Moja ya tabia hizo ni kuwa na msukumo wa ndani wa kufaka kufanikiwa, hivyo kuwa tayari kujisukuma zaidi kwenye kazi.
Kwenye biashara, ukiwa na timu sahihi una uhakika wa kufanya makubwa sana.
Weka juhudi kubwa kwenye kujenga timu sahihi na matokeo yatakwenda kuwa mazuri sana.
#NidhamuUadilifuKujituma
#AfyaUtajiriHekima
#KaziUpendoHuduma
#UpekeeUdadisiUbunifu
#UshirikianoUtegemeanoUwajibikaji
#NajengaBiashara
#HakunaKingineMuhimu
#BilioneaMafunzoni
#LazimaNitoboe
#NawekaKaziNifanikiwe
Asante sana kocha kwa hizi hatua hatua Tano zaidi mlango wa kutokea, nahitaji kusizoma zaidi kwa utulivu na kurudi rudia mara nyingi.
LikeLike
Karibu.
LikeLike
Notafuata mchakato ikishindikana nimuonesha muhusika mlango wa kutokea
LikeLike
Haina maana kubeba mizigo isiyo na manufaa.
LikeLike
Asante kocha,kwenye biashara yangu ntajitahidi kujenga timu sahihi ambayo itanifikisha kwenye mafanikio.
LikeLike
Kila la kheri.
LikeLike
Asante Kocha.
Napaswa kuweka juhudi kubwa kwenye kujenga timu sahihi na matokeo yatakwenda kuwa mazuri sana.
LikeLike
Kila la kheri.
LikeLike
Hatua ya uajiri ndio hatua tunayoikosea zaidi
LikeLike
Kabisa.
LikeLike
Asante Kocha,
Umefuata taratibu zote sahihi za kuajiri, Kupanga majukumu, mafunzo, ushauri, lakini mfanyakazi/Msaidizi hana tija, mwonyeshe mlango wa kutokea kwa faida ya biashara yako na kwa faida yake pia.
LikeLike
Hakika,
Maana kumchelewesha haimsaidii
LikeLike
Asiyezalisha anapaswa kupitia mlango wa kutokea.
LikeLike
Maana akibaki anakuwa kikwazo kwa wengine kuzalisha.
LikeLike
Kwenye biashara nikiwa na timu sahihi,wataniwezesha kufanya makubwa.
LikeLike
Hakika
LikeLike
Kwa kujenga timu sahihi yenye watu Bora Nina uhakika Wa kufanya makubwa sana.
Hakuna mtu anayeweza kufanya makubwa peke yake tunahitaji watu sahihi Wa kushirikiana nao.
LikeLike
Kweli
LikeLike
Mfanyakazi anapojua kwamba anaweza kuondolewa au kufukuzwa huongeza sana umakini.
LikeLike
Kabisa, maana uhakika unaleta mazoea ambayo yanaharibu kazi.
LikeLike
Shukrani kocha
Kweli kabisa kwenye kupata watu sahihi wa kufanya nao kazi kwa Zama hizi inahitaji uvumilivu na muda kupima kila eneo la tabia na kujenga mfumo ulio imara wa kuendesha biashara
LikeLike
Karibu
LikeLike
Kama umemwajiri mfanyakazi kwa mchakato sahihi.
Ukamweleza kwa kina majukumu anayopaswa kutekeleza.
Ukampa mafunzo ya namna ya kutekeleza majukumu yao.
Ukamfuatilia kwenye utendaji na kumsaidia kuboresha zaidi.
Lakini bado akawa anashindwa kutekeleza majukumu yake.
Hatua sahihi ni kumwondoa mfanyakazi huyo kwenye biashara.
LikeLike
Kufanya hivyo ni kumsaidia pia asiendelee kupoteza muda.
LikeLike
Ili upate wafanyakazi sahihi, unatakiwa ufuate mchakato sahihi wa kuajiri.
LikeLike
Kila kitu kinaanzia kwenye mchakato.
LikeLike
Kama umempa mtu ajira kupitia hatua sahihi na kumuelekeza majukumu yake, vile vile ukampa mafunzo
ya jinsi Bora ya kuyatekeleza majukumu hayo kwa ubora.
Kwa kumfanya hayo yote mtu huyo Kama atashindwa kutimiza majukumu yake basi hatua sahihi kwa mtu huyo ni kumfungulia MLANGO aondoke.
Asante Sana , ninajisikua raha Sana kupokea
Miongozo huu.
LikeLike
Tuitumie miongozo hii kujenga timu imara.
LikeLike
Ni muhimu kufuata mchakato na kuacha kuajiri mashemeji na marafiki ili kuleana.
LikeLike
Ukisikia tu kuna huyu mtoto wa mjomba wako hana cha kufanya mweke ajishikize kwenye biashara yako, jua kinachofuata ni majanga.
LikeLike
Kama Hana uwezo wa kufanya kazi na kuleta matokeo mazuri anaondolewa mara Moja
Asante
LikeLike
Kumwacha ni kumchelewesha, huenda akaweza kufanya vizuri pengine.
LikeLike
Asante kocha, kwenye biashara yangu ntajitahidi kujenga timu sahihi ambayo itanifikisha kwenye ndoto yangu. Kweli hatua ya kufukuza hasa ninapokuwa Nimewekeza mie huwa inaniwia vigumu Sana. Nataka kulishinda Hilo huenda ndiyo kikwazo kwangu.
LikeLike
Kuna ile huruma ya kibinadamu kwamba nikimtoa ataenda wapi.
Kuishinda huruma hiyo, kumbuka tu kwamba biashara ikifa hatabaki hapo, ataendelea na maisha yake, hivyo anapokuwa hana manufaa, asicheleweshwe.
LikeLike
Vijana wa kuwaokota mtasni ni shida maana utashindwa kuwatoa ni kama ndg kumtoa inahitaji moyo sana
LikeLike
Lazima kuwa na roho ngumu ili kujenga na kukuza hizi biashara.
LikeLike
Kwenye biashara, nikiwa na timu sahihi nina uhakika wa kufanya makubwa sana.
Natakiwa kuweka juhudi kubwa kwenye kujenga timu sahihi na matokeo yatakwenda kuwa mazuri sana.
Ahsante Sana Kocha.
LikeLike
Hakika.
LikeLike
Asante sana Kocha , nitafuata hizi hatua zote kila baada ya kuwapata wafanyakazi kwa njia ya usahili
LikeLike
Kila la kheri.
LikeLike
Kweli ni ngumu kubadilishab tabia za watu kama umepitia hatua zote hizo
LikeLike
Kwa jitihada zote hizo, kama mtu hajaweza kuleta matokeo, hakuna namna ataweza.
LikeLike
Kweli ni ngumu kubadilishab tabia za watu kama umepitia hatua zote hizo na mtu akawa hajabadilika mlango wa kutokea ni hatua muhimu
LikeLike
Ni beyond repair.
LikeLike
Kama biashara inashindwa kufukuza wabovu itakufa yenyewe au itadumaa
LikeLike
Hakuna namna nyingine.
LikeLike
Tujkfunze kuwaontesha watu mlango wa kutokea kama hawana tija kwenye biashara
LikeLike
Hakika
LikeLike
Ni kweli kabisa Kocha,
Tukiwa na Mchakato sahihi wa kuajiri tutapunguza matatizo mengi na itakuwa rahisi kwetu kumwachisha kazi maana utamfunguliamlango wa kutokea akijua ni kweli hajakidhi vigezo.
Asante
LikeLike
Kabisa, na itapunguza lawama pia.
LikeLike
Asante Sana kocha kwa njia hizi tano za msingi kabisa wakati wa kuajiri , binafsi nimeziandika Ili nianze kuzitumia kupata wafanyakazi
LikeLike
Zifanyie kazi
LikeLike