3022; Kushindwa kabla ya kuanza.
Rafiki yangu mpendwa,
Kufanya jambo lolote jipya na kubwa kwenye maisha yako, huwa kunaambatana na hatari ya kushindwa.
Hatari ya kushindwa huwa inakuwa kubwa pale mtu unapokuwa unafanya kwa mara ya kwanza.
Kukosa uzoefu kunapelekea mtu kufanya makosa mengi yanayomuathiri.
Lakini kushindwa huwa kunakuwa ni kwa uhakika, kabla hata ya kuanza, pale ambapo mtu anaiga na kutaka kuwa kama mtu au watu fulani.
Iko hivi rafiki, wakati unaanza kufanya kitu chochote, kuna watu ambao huwa unajifunza kutoka kwao.
Wengi, kutokana na ubobezi wa yule wanayejifunza kutoka kwake, wanatamani sana wangekuwa kama yeye.
Kinachotokea ni mtu kupoteza muda na nguvu kutaka kuwa kama mtu fulani, kitu ambacho hakiwezi kutokea.
Ukianza tu ukiwa na lengo la kutaka kuwa kama mtu fulani, unaanza ukiwa umeshindwa.
Hiyo ni kwa sababu pamoja na ufanano wetu binadamu, kila mmoja ana kitu ambacho ni cha kipekee kabisa, ambacho hakiingiliani na vitu vingine vyovyote.
Wajibu wako mkubwa ni kujua kile ambacho ni cha kipekee kwako na kisha kukitumia kwenye mambo yote unayofanya.
Lile eneo ambalo uko bora kuliko wengine, unapaswa kulitumia vizuri kujitofautisha kwenye chochote unachofanya.
Weka utu na utofauti wako kwenye kila unachofanya, lengo likiwa ni kujitofautisha na wengine wanaofanya kitu hicho.
Usiingie kufanya chochote kwa lengo la kuwa kama wale unaowakubali.
Bali ingia ukiwa na lengo la kufanya kwa ubora wa hali ya juu kabisa, ukiwa umeweka upekee ulio ndani yako.
Kitu kingine kinachofanya kuiga kuwe hatari ni mabadiliko yanayokuwa yanaendelea.
Kitu chochote kilichofanya kazi vizuri jana, kinaweza kisifanye kazi vizuri leo au kufika hatua ya kutokufaa kabisa kesho.
Mambo yanabadilika kwa kasi kubwa kiasi kwamba mtu asipobadilika anaachwa nyuma haraka sana.
Hata wale unaowaona wamefanikiwa sana na kutaka kuwa kama wao, kama wakifilisika na kuhitajika kuanza upya, hawatarudia yote waliyofanya huko nyuma.
Badala yake watabadili na kuboresha ili kuendana na hali halisi ilivyo.
Hivyo ndivyo mafanikio yanavyojengwa kwenye kila ngazi ya maisha, kuendana na hali halisi ilivyo.
Kutaka kurudia kile ambacho tayari ni cha uhakika ni kuchagua kushindwa kabla hata hujaanza, kwa sababu mambo hayaendi jinsi ambavyo unataka wewe yaende.
Ni vizuri sana kuwa na mashujaa kwenye maisha yetu,
Watu ambao kwa kuwaangalia tunapata matumaini kwamba chochote kikubwa tunachotaka kukifikia kinawezekana.
Ubaya ni pale tunapotaka kuwa kama mashujaa wetu, hapo ndiyo tunakuwa tumeshindwa kabla hata ya kuanza.
Kila mtu ana upekee wake ambao hauwezi kuigwa na wengine.
Unapowaangalia mashujaa wako, angalia jinsi ambavyo kila mmoja kuna kitu cha kipekee anacho.
Matumizi sahihi ya kitu hicho cha kipekee ndiyo yanakuwa yamemweka mtu kwenye nafasi ya kufanya makubwa kuliko wengine.
Anza na ushindi, siyo kwa kuwa kama wengine, bali kwa kujitambua na kuwa wewe.
Kuna nguvu kubwa sana kwenye kuwa wewe, nguvu ambayo wengi hawaifikii na kuweza kuitumia.
Ifikie na kuitumia nguvu hiyo ili uweze kufanya makubwa kwenye maisha yako.
Na hapo ndipo mafanikio yanapokuwa magumu kwa wengi, hawapati nafasi ya kujitambua wao wenyewe na kufikia na kutumia uwezo mkubwa wa ndani.
Wanachokuwa wanafanya ni kuiga yale wengine wanafanya, kwa namna wanavyoyafanya na hilo kuwa kikwazo kwao.
Unaweza kuiga njia mbalimbali zinazofanya kazi kwa watu wengine.
Lakini mwisho wa siku lazima uzifanyie kazi kwa namna ya kipekee kwako ili uweze kupata matokeo yaliyo bora kabisa.
#NidhamuUadilifuKujituma
#AfyaUtajiriHekima
#KaziUpendoHuduma
#UpekeeUdadisiUbunifu
#UshirikianoUtegemeanoUwajibikaji
#BilioneaMafunzoni
#NajengaBiashara
#HakunaKingineMuhimu
#LazimaNitoboe
#NawekaKaziNifanikiwe
Ni jambo jema kuwa na mashujaa lakini kuwaiga na kushindwa kabla hujaanza.
LikeLike
Nitafanya kazi kipekee siku zote ili kuwa mimi
LikeLike
Nakua mimi na kufanya kwa upekee ili niweze kujitofautisha na wengine.
LikeLike
Asante kocha,kila mtu ana upekee,hivyo nitafanya kwa ubora zaidi kuliko kuiga wengine.
LikeLike
Kwenye biashara yangu,najitafuta ili niweze kufanya biashara yangu kwa upekee wangu kama sasa kuwahi kufungua,kuchelewa kufunga,kutoa huduma siku zote bila kujali siku za wikendi au siku kuu yoyote,kutoa huduma bora kila siku.
LikeLike
Hatari ya kuiga ni kwamba
Kilichofanya kazi vizuri jana, kinaweza kisifanye vizuri leo au kesho kisifae kabisa. Asante sana kocha.
LikeLike
Nitaiga njia mbali mbali zinazofanya kazi kutoka kwa wengine,lakini sitolazimishia kuwa kama shujaa maana nitakua nimejiandikia kushindwa.
LikeLike
Nitakuwa mimi katika kile ninachofanya na kujifunza kwa wengine ili kuepuka makosa yao
LikeLike
Ni muhimu kujifunza kutoka kwa wengine lakini mwisho wa siku tunapaswa kuwa sisi yaani kuwa na upekee ambao haufanani na wengine.
Asante sana
LikeLike
Asante kocha kwa somo hili. Nitajitahidi kufanya kazi zangu na biashara kwa upekee
LikeLike
Tuwaangalie mashujaa lakini kwa lengo la kuwa bora zaidi yao tuige njia zao na kuziboresha ili zilete matokeo bora zaidi kwetu
LikeLike
Kabisa
LikeLike
Mimi ni wa tofauti sifanani na mwengine.
Napaswa kufanya kwa namna ya tofauti ambayo inanitofautisha mimi na wengine. Hata kama kuna makubwa waliofanya lakini sipaswi kufuata kila kitu kutoka kwa wengine
LikeLike
Vizuri sana.
LikeLike
Ahsante sana kocha kwa Uzi Bomba sana wa Leo.
Hapa nimejifunza kuwatumia wengine na kuwa mbunifu katika kazi zangu.
Naenda kulifanyia KAZI hili.
LikeLike
Kila la kheri.
LikeLike
Kujifunza Kwa wengine ni jambo jema. Kujifunza huko kuwe kunaamsha uwezo WA kipekee uliopo ndani yetu.
LikeLike
Hakika.
LikeLike
Kuwa na mashujaa kwa lenig la kuhamasika kwamba inawezekana lakini usiwaige kwani kila mtu ni tofauti na mabadiliko ni kila wakati
LikeLike
Tukae humo.
LikeLike
Asante Sana kocha nikweli kunz kitu ambacho ni cha kipekee kabisa kitu hicho nitakitumia vizuri ili kuwa bora kabisa na sio kuwaiga wengine ili kuwa kama wao
LikeLike
Vizuri sana.
LikeLike
Kuwa na role model lakini kuwa wewe
Asante
LikeLike
Ushindi mkubwa upo kwenye kuwa wewe.
LikeLike
Anza na ushindi, siyo kwa kuwa kama wengine, bali kwa kujitambua na kuwa wewe.
Kuna nguvu kubwa sana kwenye kuwa wewe, nguvu ambayo wengi hawaifikii na kuweza kuitumia.
Asante sana Kocha, nitakutumia nguvu na upekee ulio ndani yangu kuvuta mafanikio kuja kwangu.
LikeLike
Kila la kheri.
LikeLike
Huu ndio ukweli
LikeLike
Hakika
LikeLike
Mafanikio ya uhakika ni kuwa wewe na si kuiga wengine.Siku zote nitafanya mambo kwa utofauti na ubora kwa kuwa mimi.
LikeLike
Vizuri sana.
LikeLike
Kwa kutumia upekee wangu , nitatimiza majukumu yangu kwa ubora wa Hali ya juu kabisa.
Shuklani kocha
LikeLike
Kila la kheri.
LikeLike
Upekee ndio njia pekee ya kuwa Bora, naweza kujifunza Kwa mashujaa wangu lakini si Kwa Kuiga Bali Kwa kuwa Mimi.
Asante Kocha
LikeLike
Vizuri sana.
LikeLike
Nimejifunza kutokufanya chochote kwa kuwa sawa na wale ninaowakubali bali kwa lengo la kufanya kwa ubora wa hali ya juu na kuweka upekee ulio ndani yangu.
Asante.
LikeLike
Vizuri sana.
LikeLike
Weka utu na utofauti wako kwenye kila unachofanya, lengo likiwa ni kujitofautisha na wengine wanaofanya kitu hicho.
LikeLike
Hakika.
LikeLike
Najaribu kuwa mimi na sitaki kuwa kopi wa yeyote.
LikeLike
Kila la kheri.
LikeLike
Asante Sana Kocha.
Ubilionea au mafanikio yapo kwenye UPEKEE,kila mtu ana upekee wake. Kuiga hakuna mafanikio ya muda mrefu. Nitaongeza maarifa ili niongeze ubunifu na UPEKEE wangu
LikeLike
Kila la kheri.
LikeLike