3164; Uchumi wa biashara.
Rafiki yangu mpendwa,
Biashara nyingi sana zinazoanzishwa huwa zinaishia kufa ndani ya muda mfupi tangu kuanzishwa kwake.
Na hata zile ambazo hazifi, nyingi zimekuwa hazipati ukuaji mkubwa, badala yake zinabaki kuwa ndogo.
Sababu nyingi zimekuwa zinatolewa juu ya biashara kufa.
Na ya kwanza kabisa ambayo imekuwa inasemwa sana ni ushindani mkali.
Karibu wote ambao biashara zao zimeshindwa wamekuwa wakitaja ushindani mkali kuwa chanzo kikuu cha biashara zao kufa.
Hali mbaya ya uchumi pia imekuwa inatumiwa kama sababu ya biashara nyingi kufa.
Lakini sababu zote hizo ambazo zimekuwa zinatolewa, zimekuwa siyo kiini hasa cha biashara kufa.
Zinaweza kuwepo, lakini zinakuwa zimemalizia tu, chanzo halisi kinakuwa kingine.
Chanzo halisi kinachopelekea biashara kufa ni kuwa na uchumi mbaya.
Hapa haimaanishi uchumi kwa ujumla, bali uchumi wa biashara moja moja.
Maana halisi ya uchumi ni udhibiti wa rasilimali haba.
Inapokuja kwenye biashara, jinsi rasilimali haba kwenye biashara zinavyodhibitiwa, ndiyo inapelekea biashara kufa au kupona.
Kuna rasilimali haba nyingi kwenye biashara. Kuanzia fedha, watu, muda na hata vitendea kazi mbalimbali.
Katika rasilimali hizo nyingi, ya kwanza na yenye athari kubwa zaidi kwenye biashara ni mzunguko wa fedha.
Mzunguko wa fedha ndiyo rasilimali yenye madhara makubwa kwenye biashara kama haitadhibitiwa vizuri.
Kifo cha biashara karibu zote huwa kinaanzia kwenye udhibiti mbaya wa mzunguko wa fedha.
Uchumi sahihi wa biashara kwenye mzunguko wa fedha ni fedha zinazoingia zinapaswa kuwa nyingi kuliko zinazotoka kwenye biashara.
Kuingia ni kupitia mauzo na kutoka ni kupitia matumizi.
Biashara yoyote ile yenye mapato makubwa kuliko matumizi, ina nguvu ya kuendelea kuwepo sokoni na kukabiliana na changamoto nyingine za soko.
Lakini biashara ambayo matumizi ni makubwa kuliko mapato, hiyo tayari ipo kwenye shimo la kifo, ni swala la muda tu kabla haijazikwa.
Huwezi kulaumu ushindani pale mzunguko wa fedha kwenye biashara unapokuwa hasi, yaani matumizi kuzidi mapato.
Hapo ni kwamba tu biashara imeshindwa kufanya kazi.
Ushindani utamalizia tu kile ambacho tayari kimeshaanza.
Kwa maana hiyo basi, ushindani wa kwanza kwenye biashara ya aina yoyote ile ni mauzo madogo na matumizi makubwa.
Pale mauzo yanapokuwa madogo na matumizi yakawa makubwa, ni uhakika biashara imeshindwa na haitaweza kudumu kwa muda mrefu, hata kama ipo yenyewe kwenye eneo ambapo ipo.
Lakini biashara inapokuwa na mauzo makubwa huku matumizi yakiwa madogo, inakuwa na nguvu ya kuweza kupambana sokoni.
Kabla hujahangaika na mambo mengi ya nje ya biashara yako, hebu anzia ndani.
Hebu anzia kwenye uchumi wa biashara yako.
Je kwa mauzo yanayofanyika, biashara inaweza kuendelea kujiendesha yenyewe?
Na je kwa matumizi yaliyopo, biashara itaweza kwenda kwa muda mrefu kiasi gani?
Unaweza kuwa na mauzo makubwa sana, lakini kama gharama za uendeshaji ni kubwa, bado biashara itashindwa.
Hili ndilo wafanyabiashara wengi wadogo wamekuwa hawalielewi na hivyo kusema kuna chuma ulete.
Kadhalika kama gharama za kuendesha biashara zipo chini, hata kwa mauzo ambayo siyo makubwa, bado biashara inaweza kuwa na nguvu kubwa ya kushindana sokoni.
Unaweza kuhangaika na mengi sana kwenye biashara yako, lakini kama hutapatia kwenye uchumi wa msingi wa biashara, bado tu itashindwa.
Weka umakini wako mkubwa kwenye kujenga uchumi sahihi wa biashara yako, kwa kuhakikisha kila wakati mapato ni makubwa kuliko matumizi.
Kwa kusimamia vizuri mzunguko wa fedha, changamoto nyingine nyingi zinazoua biashara nyingi zinakosa nguvu kwenye biashara yako.
#NidhamuUadilifuKujituma
#AfyaUtajiriHekima
#KaziUpendoHuduma
#UpekeeUdadisiUbunifu
#UshirikianoUtegemeanoUwajibikaji
#BilioneaMafunzoni
#NajengaBiashara
#HakunaKingineMuhimu
#LazimaNitoboe
#NawekaKaziNifanikiwe
Uchumi sahihi wa biashara ni msingi mkuu wa biashara kuendelea kuwepo na kukua.
LikeLike
Hakika
LikeLike
Asante kocha nitaweka umakini Wangu wote kwenye mzunguko wa biashara yangu hasa kwenye fedha kwasababu hapa ndiyo kwenye hatari kubwa ya biashara kufa kwakuhakikisha mapato yawe makubwa kuliko matumizi
LikeLike
Kila la kheri
LikeLike
Kusimamia vizuri mapato na matumizi ili mauzo yawe makubwa kuliko matumizi ili biashara iweze kudumu muda mrefu sokoni
LikeLike
Hakika
LikeLike
Ahsante sana kocha, ushindani wa kwanza kwenye biashara ya aina yoyote ile ni mauzo madogo na matumizi makubwa. Nitajitahidi kudhibiti matumizi
LikeLike
Vizuri
LikeLike
Naweka nguvu kubwa katika kujenga uchumi sahihi wa biashara yangu.
Matumizi kidogo lakini mauzo Makubwa.
LikeLike
Kila la kheri.
LikeLike
Asante sana kocha,nitaweka nguvu zaidi ktk kusimamia vzr mzunguko wa fedha inayoingia na kutoka.
LikeLike
Vizuri.
LikeLike
Kwa maana hiyo ushindani wa kwanza kwenye Biashara ni matumizi makubwa kulinga na mauzo
LikeLike
Ndiyo
LikeLike
Nitahakikisha uchumi wa biashara yangu unakuwa vizuri kwa Mapato kuwa makubwa kuliko matumizi.
LikeLike
Kila la kheri.
LikeLike
Nitahakikisha gharama za kuendesha biashara zinakuwa ndogo zaidi kuliko mapato kwa kuuza zaidi ili biashara iweze kukua.
LikeLike
Vizuri
LikeLike
Nitaendelea kukuza mapato, huku nikitafuta njia nzuri za kupunguza gharama kwenye biashara.
Asante Kocha.
LikeLike
Zingatia
LikeLike
Asante kocha,Nitajitahidi kudhibiti uchumi kwenye biashara ikiwa ni kukuza mapato na kupunguza matumizi ili biashara ijiendeshe yenyewe na kupata mafanikio.
LikeLike
Vizuri
LikeLike
Weka umakini wako mkubwa kwenye kujenga uchumi sahihi wa biashara yako, kwa kuhakikisha kila wakati mapato ni makubwa kuliko matumizi.
LikeLike
Hakika.
LikeLike
Mapato yanapaswa kuwa makubwa kuliko matumizi.
Asante sana Kocha Dr Makirita Amani.
LikeLike
Ndiyo.
LikeLike
Asante Kocha,
Nimejifunza maana halisi ya uchumi ni udhibiti wa rasilimali haba.
LikeLike
Vizuri.
LikeLike
Ni kitu ambacho Kiko wazi kabisa , lakini kimejificha
Kitu hicho ni : kifo Cha biashara karibu zote huwa kinaanzia kwenye udhibiti mbaya wa mzunguuko wa fedha kwenye biashara.
Hivyo ni muhimu kuhakikisha fedha nyingi inaingia ktk
biashara kuliko inayotoka.
Asante kocha.
LikeLike
Karibu
LikeLike
Hakika mapato makubwa matumizi kidogo na ukiweka muda na kazi mafanikio ni uhakika
Asante sana
LikeLike
Karibu.
LikeLike
Vizuri kabisa
LikeLike
Karibu.
LikeLike
Chanzo halisi kinachopelekea biashara nyingi kufa Ni kuwa na uchumi mbaya wa Mzunguko wa fedha.
Nitajitahidi kusimamia Mzunguko wa fedha kwa kuongeza mauzo na matumizi ili matumizi yasizidi mapato .
Asante sana Kocha.
LikeLike
Vizuri, tukae humo.
LikeLike
Vizuri sana.
LikeLike
Nitafanya mauzo makubwa Na nitapunguza matumizi ili biashara iyendelee kukuwa
LikeLike
Kila la kheri
LikeLike
Ni kweli kocha kuweka umakini wako mkubwa kwenye kujenga uchumi sahihi wa biashara yako, kwa kuhakikisha kila wakati mapato ni makubwa kuliko matumizi. Tunaweza kuudhibiti anguko la biashara zetu.
LikeLike
Ndiyo.
LikeLike
Asante sana Kocha. Uchumi WA biashara yangu ukikaa sawa basi biashara yangu haiwezi kufeli
LikeLike
Ndiyo
LikeLike