3223; Jipe dakika tano.
Rafiki yangu mpendwa,
Huwa ni kawaida kwetu binadamu tunaposikia kitu kipya kwa mara ya kwanza kukikataa na kukipinga kwamba hakifai au hakiwezekani.
Lakini mara nyingi hayo huwa ni maamuzi ya haraka ambayo pia siyo sahihi.
Unakuwa umefikia hitimisho la haraka kabla hata ya kutafakari kwa kina.
Kuepuka hali hiyo ya kufikia maamuzi ya haraka na ambayo siyo sahihi, jijengee utaratibu wa kujipa muda wa kutafakari kila jambo jipya kabla ya kufikia hitimisho.
Jipe angalau dakika za kukitafakari kitu kabla ya kufanya maamuzi juu ya kitu hicho.
Unafanya hivyo pia kabla hujakubaliana na kitu fulani unachoombwa.
Kwa sababu maamuzi yoyote ya haraka hayajawahi kuwa sahihi.
Kuna namna baadaye utakuja kujutia kwamba uliyaharakisha maamuzi hayo.
Ni sawa kukubali au kukataa kitu,
Kuona kinafaa au hakifai,
Kuchukulia ni rahisi au ngumu.
Lakini kwanza jipe muda wa kutafakari kitu kabla ya kufikia maamuzi hayo.
Dakika tano ni kiwango cha chini unachopaswa kujipa kutafakari jambo kwa kina kabla hujafanya maamuzi.
Na hapo ni kama maamuzi yanapaswa kuwa ya haraka.
Kama maamuzi hayana uharaka, jipe muda zaidi wa kutafakari jambo.
Tena hapa chukua zoezi la kuandika kabisa.
Andika pande mbili za jambo husika; upande wa kukubaliana na jambo husika na kuona manufaa yake na upande wa kukataa jambo hilo na kuona madhara yake.
Unapokaa chini na kuandika, unakuwa umeipa akili yako kazi ya kufikiri kwa kina juu ya kitu. Huwezi kuandika kama hujafikiri.
Na kwa kujipa wajibu wa kuandika kuhusu pande mbili za jambo, unakuwa umeliangalia kwa upana wake kabla ya kufikia maamuzi.
Kuna makosa mengi umeyafanya kwenye maisha yako kwa kukimbilia kufanya maamuzi juu ya jambo ulilosikia.
Kuna fursa nyingi umezikosa kwa kufanya maamuzi kabla hujatafakari kwa kina.
Usikubali kuendelea hivyo, bali jipe muda wa kutosha wa kutafakari kabla hujafikia maamuzi.
Na kama unalazimishwa ufanye maamuzi kwa haraka kabla ya kufikiri kwa kina shtuka, kuna kitu hakipo sawa.
Mara nyingi watu wanapokuwa wanataka kukuhadaa au kukutapeli huwa wanakushinikiza ufanya maamuzi ya haraka kabla hujafikiri sawasawa.
Jiwekee sera ya kufikiri kitu kwa angalau dakika 5 kabla ya kukifanyia maamuzi ya kudumu.
Na kama kitu hakiwezi kusubiri kwa dakika 5, siyo kitu sahihi kwako.
Na unapojipa dakika 5 za kufikiri kuhusu kitu, usikifikiri kwa mazoea ambayo tayari unayo. Badala yake jilazimishe kwenda nje ya mazoea hayo.
Ndiyo maana ni muhimu kuangalia pande mbili za jambo lolote kabla ya kulifanyia maamuzi.
Kufikiri kwa angalau dakika 5 kabla ya mufanya maamuzi kutakuepusha na makosa mengi ambayo umekuwa unayafanya kwa kukimbilia maamuzi ya haraka.
Kujifunza kufikiri haraka badala ya kujibu haraka ni hitaji muhimu kwa maisha ya mafanikio.
Hivyo basi rafiki yangu, wakati mwingine unaposikia kitu kwa mara ya kwanza, jipe dakika tano za kukifikiria kwa kina kabla ya kukifanyia maamuzi yoyote yale.
Kabla ya kukubali au kukataa kitu, hebu jipe muda wa kukitafakari kwa kina pande zake mbili.
Zoezi hili litakupa fursa ya kukielewa kitu kwa kina na kuona namna sahihi ya kwenda nacho.
#NidhamuUadilifuKujituma
#AfyaUtajiriHekima
#KaziUpendoHuduma
#UpekeeUdadisiUbunifu
#UshirikianoUtegemeanoUwajibikaji
#BilioneaMafunzoni
#NajengaBiashara
#HakunaKingineMuhimu
#LazimaNitoboe
#NawekaKaziNifanikiwe
ahsante kocha
hichi kitu nilifanya wakati wa semina baada ya mabadiliko ya kcm, ccm na bm baada ya kutafakari nikaona maamuzi ni sahihi lakini kabla ya hapo nilikuwa na wasiwasi wa kcm kufa.
katika hili nina changamoto moja.
wakati mwingine ninapojipa muda kabla ya kufanya maamuzi unakuta hata hayo maamuzi sifanyi tena. na jambo linaisha juu kwa juu.
LikeLike
Vizuri sana.
Kama jambo limeishia juu juu kwa kujipa muda, basi halikuwa muhimu kihivyo. Na maana yake kujipa muda ilikuwa sahihi, maana unakuwa umejiepusha kuhangaika na lisilokuwa sahihi.
LikeLike
Hakika mara zote nitafikiri haraka kabla ya kujibu kwa haraka.
Chochote kisichoweza kunipa dakika 5 za kufikiria siyo sahihi kulifanyia maamuzi, nitaachana nacho
Ili kufikiri vizuri, nitaandika pande zote mbili za jambo kuona faida na hasara , kabla ya kufanya maamuzi
LikeLike
Kila la kheri.
LikeLike
Ni muhimu Kuangalia pande 2 za jambo kabla kuchukua maamuzi. Pia tumia kwa kupungua angalau dakika 5 kufikiria jambo hilo kabla ya maamuzi
LikeLike
Hakika
LikeLike
Asante sana Kocha. Hii njia inafanya kazi vizuri sana, hasa kwenye kuitawala hasira na kufanya maamuzi na machaguo bora.
LikeLike
Kweli kabisa.
LikeLike
Asante kocha nimekuwa nikifanya maamuzi kwa harakaharaka hata bila kufikiria na matokeo yake hayo maamuzi yanakuwa siyo sahihi na kujutia baadaye kwa hiyo nimejifunza nakwenda kuchukua hatua yakujipa dakika 5 nakulitafakari jambo pande zote mbili
LikeLike
Kila la kheri.
LikeLike
Hii inataka kufanana na mbinu ya ukamilishaji namba 79, Ukamilishaji wa Benjamin Franklin.
Hili ni muhimu sana katika kuepuka majuto.
LikeLike
Kweli kabisa, ni humo humo.
LikeLike
Kujifunza kufikiri haraka ni hitaji namba moja la msingi, najipa angalau dakika tano za kufikiri, najenga mazoea ya kufikiri haraka walau kwa dakika tano kabla ya kufanya maamuzi.
LikeLike
Ndiyo
LikeLike
Kujipa muda kuhusu maamuzi tunayotaka kufanya ni muhimu. Angalau dakika tano.
LikeLike
Ndiyo.
LikeLike
Kujifunza kufikiri haraka badala ya kujibu haraka ni hitaji muhimu kwa maisha ya mafanikio.
LikeLike
Hakika
LikeLike
Ni jambo muhimu sana kwenye kufanya maamuzi ya jambo lolote lile nakwenda kufanyia kazi ujumbe huu kwa kila maamuzi ambayo nafanya
LikeLike
Vizuri sana.
LikeLike
Asante sana njia hii nitaitumia Kwa kuanza na mambo kadhaa ambayo yanapaswa kufanyiwa kazi mara moja
LikeLike
Kila la kheri.
LikeLike
Dakika tano ni kipimo vizuri cha kufikiri kabla hujafanya maamuzi juu ya kitu.
Hata mbinu nyingine wanayotumia matapeli ni kukusogezea kitu karibu na macho kabisa hii inakufanya ushindwe kuona vizuri kwa mfano simu.
Asante sana.
LikeLike
Hakika
LikeLike
Jipe muda Kwa jambo lolote jipya na utakuwa na majibu ya uhakika
Asante
LikeLike
Hakika
LikeLike
Asante sana kocha kwa makala hii nzuri
LikeLike
Karibu.
LikeLike
Ni vizuri kuangalia pande mbili za jambo kabla Ya kuchukuwa maamuzi na kujipa muda wa kutafakari angalau dakika tano kabla Ya kufanya uamuzi.
LikeLike
Hakika
LikeLike
Kuepuka maamuzi ya papara na kukurupuka tunahitaji muda wa kuifanya akili ichambue kwa kina mtego uliopo. Kujibu kwa haraka sio kufikiria kwa haraka. Majibu Sahihi yapo kwenye ubongo na hapo ni muda kiasi kuifanya akili iweke wazi usahihi
LikeLike
Tufikiri vyema
LikeLike