‎Mpendwa Rafiki,

‎Hii Ndiyo Siri Ya Kuacha Kuishi Kwa Bahati Nasibu.

‎Kama umewahi kujiuliza, “Hivi mshahara wangu unaishia wapi?” au unashangaa kila mwezi hela yako inakatika bila hata kununua kitu kikubwa,

‎…basi hii makala ni yako. Watu wengi wanapambana na kitu kimoja, kutokujua kutumia na kusimamia pesa zao binafsi kwa mpangilio.

‎Na matokeo yake, kila mwezi unakuwa kama sinema ile ile ya huzuni.

‎Hebu fikiria… unafanya kazi kama punda, unapata mshahara au kipato fulani, lakini mwisho wa mwezi unaomba mpaka nauli.

‎Akiba huna, mikopo unayo, na kila hela ikija ni kama upepo unapuliza.

‎Hali kama hii inavunja moyo. Inakufanya uanze kuamini kuwa labda “mimi sina bahati na pesa,” kumbe tatizo si pesa,

‎…ni usimamizi wako.

‎Watu wengi huamini kwamba ili uweze kujiwekea akiba au kupanga matumizi yako, lazima uwe na kipato kikubwa.

‎ Uongo mtupu.

‎Hakuna hela ndogo, kuna matumizi mabaya.

‎Hata ukiwa unapata elfu kumi kwa siku, ukiwa na mpango, unaweza kuweka akiba, ukawekeza, na ukaishi kwa amani bila presha.

‎Tatizo ni kuishi bila bajeti, kutumia kwa mazoea, na kuiga maisha ya watu mitandaoni.

‎Sasa sikiliza: Suluhisho la kweli ni kujifunza kusimamia kipato chako kwa nidhamu.

‎Andika mapato na matumizi.

‎Tengeneza bajeti ya wiki au mwezi.

‎Anza kuweka akiba kila unachopata – hata kama ni buku kwa siku.

‎Epuka matumizi yasiyo na tija, kama vile vinywaji, usafiri wa kifahari, au mlo wa kila siku unaoweza kupunguzwa.

‎Jifunze pia kuwekeza kidogo, hata kwenye maarifa kama vitabu au kozi za fedha.

‎ Usimamizi wa fedha sio ugumu ni maamuzi.

‎Nakumbuka mshikaji wangu Sule kutoka Tabata.

‎Alikuwa anapata mshahara wa laki tatu, lakini alikuwa hana akiba hata ya elfu tano.

‎Nilimshauri aanze kutumia app ya kufuatilia matumizi yake, na kila siku aweke buku moja kwenye bahasha ya akiba.

‎Mwaka mmoja tu baadaye, alikuwa ameweka zaidi ya laki tatu na nusu, akajifunza kupitia kozi ya NGUVU YA BUKU, na leo ana ka-biashara ka kuuza vocha na bidhaa za mtandaoni.

‎Sasa ananiambia, “Bro, kumbe shida yangu haikuwa mshahara, ilikuwa nidhamu.”

‎Sasa ni wakati wako.

‎Anza kuzitawala fedha zako.

‎Jifunze kusimamia fedha zako mwenyewe.

‎Hatua ndogo leo, ni uhuru mkubwa kesho.

‎Kama ungependa kujifunza zaidi kuhusu usimamizi wa fedha binafsi na kupata tools kali kama app, vitabu na kozi.

‎Basi Bonyeza  Hapa:

‎👉 https://wa.link/pxqntw

‎Au piga: 0756 694 090

‎Karibu Tujenge Maisha Bila Presha.

Imeandikwa Na Bwana Ramadhan Amir